TAREHE 17-23/11
WIMBO WA SULEMANI 6-8
Wimbo 34 na Sala | Maneno ya Utangulizi (Dak. 1)
1. Ukuwe Ukuta, Hapana Mulango
(Dak. 10)
Bandugu yake ya Mushulami habakuwa napenda afanye ngono mbele ya kuolewa (Wim 8:8, 9; w15 15/1 uku. 32 fu. 15-16)
Mushulami alikuwa na amani juu hakuangukia hata kidogo mu mutego ya uasherati (Wim 8:10; yp uku. 188 fu. 2)
Aliachia vijana mufano muzuri (yp2-SW uku. 33)
UJIULIZE, ‘Namna gani naweza kusaidia Bakristo ba mu kutaniko yangu benye habayafunga ndoa juu bakuwe ukuta, hapana mulango?’
2. Mali ya Kiroho
(Dak. 10)
Wim 8:6—Juu ya nini upendo wa kweli unaitwa pia “mwali wa moto wa Yah”? (w23.05 uku. 20 fu. 1, maelezo ya chini)
Mu usomaji wa Biblia wa hii juma, ulipata mali gani ya kiroho yenye ungependa kuzungumuzia?
3. Usomaji wa Biblia
(Dak. 4) Wim 7:1-13 (th somo ya 12)
4. Kuanzisha Mazungumuzo
(Dak. 2) NYUMBA KWA NYUMBA. Tumia karte ya jw.org juu ya kuanzisha mazungumuzo. (lmd somo ya 4 nukta ya 4)
5. Kuanzisha Mazungumuzo
(Dak. 2) MAHUBIRI YA MAHALI PA WATU WENGI. Tumia trakte juu ya kuanzisha mazungumuzo fasi kwenye batu biko nafanyia biashara. (lmd somo ya 1 nukta ya 4)
6. Kuanzisha Mazungumuzo
(Dak. 2) MAHUBIRI YA WAKATI WOWOTE. Anzisha mazungumuzo mu njia ya kirafiki. Ile mazungumuzo inamalizika bila weye kupata nafasi ya kuhubiri. (lmd somo ya 2 nukta ya 4)
7. Kufasiria Mambo Yenye Unaamini
(Dak. 5) Onyesho. ijwfq-SW habari ya 43—Kichwa: Je, Mashahidi wa Yehova Wana Sheria Kuhusu Urafiki wa Kimapenzi? (th somo ya 7)
Wimbo 121
8. Kimbia Uasherati
(Dak. 15) Mazungumuzo.
Mu Wimbo wa Sulemani, muchungaji alimualika Mushulami baende pamoya mu matembezi. (Wim 2:10-14) Hata kama inawezekana ule muchungaji hakukuwa na nia ya mubaya, bandugu yake ya Mushulami balikuwa na hekima, njo maana balipatia Mushulami na batu bengine kazi yenye ingefanya Mushulami asiende mu ile matembezi. (Wim 2:15) Balielewa kama Mushulami na muchungaji bakijikuta bo peke mu ile matembezi, ingebafanya baangukie mu mutego ya uasherati.
Biblia inaambia Bakristo ‘bakimbie uasherati.’ (1Ko 6:18) Tunapaswa kuepuka kila tendo yenye inaweza kutufanya tuangukie mu ile mutego. Muandikaji wa Wimbo wa Sulemani aliandikaka pia hivi: “Mutu mwerevu anaona hatari na kujificha, lakini wenye hawana uzoefu wanaendelea mbele na kupata matokeo ya mubaya.”—Mez 22:3.
Muangalie VIDEO Mungu “Anajua Siri za Moyo.” Kisha uliza basikilizaji:
Hii video inakufundisha nini?
9. Funzo ya Biblia ya Kutaniko
(Dak. 30) lfb somo ya 36-37