Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp22 na. 1 uku. 8-9
  • 2 | Usirudishe Ubaya kwa Ubaya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 2 | Usirudishe Ubaya kwa Ubaya
  • Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2022
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Fundisho ya Biblia:
  • Ile Iko na Maana Gani?
  • Mambo Yenye Unaweza Kufanya:
  • Nilikuwa Mukali Sana na Mwenye Jeuri
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Tunaweza Kuachana na Chuki!
    Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2022
  • Namna ya Kuachana na Chuki
    Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2022
  • Utangulizi wa Sehemu ya 7
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2022
wp22 na. 1 uku. 8-9
Wanaume wawili wenye kukasirika wanaikala kwenye matawi ya muti. Kila mumoya iko nakata tawi yenye anaikalia.

NAMNA YA KUACHANA NA CHUKI

2 | Usirudishe Ubaya Kwa Ubaya

Fundisho ya Biblia:

“Musimulipe mutu yeyote uovu kwa uovu. . . . Kama inawezekana, kwa kadiri inawategemea ninyi, mukuwe wenye kufanya amani na watu wote. Musijilipizie kisasi, . . . kwa maana imeandikwa: ‘“Kisasi ni changu; mimi nitalipa,” ni vile Yehova anasema.’”​—WAROMA 12:17-19.

Ile Iko na Maana Gani?

Hata kama ni kawaida kukasirika wakati mutu fulani anatutendea mubaya, Mungu hapendi tulipize kisasi, ni kusema hapendi turudishe ubaya kwa ubaya. Lakini anatuambia tumungojee, juu hivi karibuni atamaliza ukosefu wote wa haki.​—Zaburi 37:7, 10.

Mambo Yenye Unaweza Kufanya:

Wakati wanadamu wenye hawakamilike wanarudisha ubaya kwa ubaya, ile inafanyaka tu chuki iendelee. Njo maana, kama mutu alikukosea ao alikutendea mubaya, usimurudishie. Ujikaze kujizuia na utende mu njia yenye itafanya kukuwe amani. Wakati fulani, inaweza kuwa muzuri uache ile jambo ipite. (Mezali 19:11) Ni kweli, unaweza kuamua kuzungumuzia ile jambo ikiwa unaona kama kufanya vile itasaidia. Kwa mufano, ikiwa walikutendea jambo yenye haipatane na sheria, unaweza kuripoti ile jambo ku polisi ao kwa wakubwa wengine wa serikali.

Kurudishia wengine ubaya kwa ubaya ni kufanya tu ubaya uendelee

Sasa utafanya nini kama unaona kuwa hakuna namna ya kumaliza ile tatizo kwa amani? Ao utafanya nini kama ulishafanya yote yenye unaweza juu ya kumaliza ile tatizo kwa amani, lakini haupate matokeo ya muzuri? Usirudishe ubaya kwa ubaya. Kufanya vile, kunaweza kufanya hali ikuwe mubaya zaidi. Kuliko kurudisha ubaya kwa ubaya, uzuie chuki juu isiendelee. Ukuwe hakika kama Mungu anajua namna ya muzuri ya kumaliza ile tatizo. “Umutegemee yeye, naye atatenda kwa ajili yako.”​—Zaburi 37:3-5.

Habari ya Kweli​—ADRIÁN

Aliachana na Tabia ya Kurudisha Ubaya kwa Ubaya

Adrián.

Wakati alikuwa kijana, Adrián alikuwa na kasirani mingi na alikuwa natendea watu kwa ukali. Tena, wakati watu walimutendea mubaya, alikuwa nawarudishia. Anasema hivi: “Mara mingi nilikuwa mu vikundi vya watu wenye walipigana na vikundi vingine kwa kutumia bunduki, na mara mingi nilikuwa mwenye kuyala damu na niliachwa mu barabara karibu kufa.”

Adrián alianza kujifunza Biblia wakati alikuwa na miaka 16. Anasema tena hivi: “Wakati nilikuwa najifunza Biblia, niliona kama nilipaswa kubadilisha tabia yangu.” Adrián alipaswa kuachana na chuki na kuacha kutendea wengine kwa jeuri. Mambo yenye alijifunza mu Waroma 12:17-19 juu ya kuepuka kurudisha ubaya kwa ubaya, ilimusaidia sana. Anasema hivi: “Nilifikia kukubali kama Yehova njo anajua namna ya kumaliza ukosefu wa haki, na anajua ni wakati gani atafanya vile. Polepole, nilifikia kuacha tabia ya kutendea watu kwa jeuri.”

Mangaribi moya, kikundi ya vijana wenye walizoeaka kupigana na Adrián walimushambulia. Mwenye alikuwa naongoza ile kikundi alisema hivi kwa sauti kubwa: “Kuya tupigane!” Adrián anasema hivi: “Nilijisikia kuwa inaomba tu nipigane nao.” Lakini kuliko kufanya vile, Adrián alitoa sala fupi kwa Yehova na akatoka pale.

Adrián anasema tena hivi: “Siku yenye ilifuata, nilikutana na kijana mwenye alikuwa naongoza ile kikundi, lakini pale alikuwa yeye peke. Nilisikia kasirani sana na nilipenda tu nimurudishie. Lakini nilisali tena mu moyo, na nikamuomba Yehova anisaidie nijizuie. Niliwaza kama na yeye alikuwa na kasirani, lakini nilishangala wakati alikuya kwenye nilikuwa na kuniambia hivi: ‘Unisamehe juu ya mambo yenye ilitokea jana mangaribi. Ningependa kuwa tu sawa weye. Ninapenda kujifunza Biblia.’ Nilifurahi sana juu niliweza kuzuia kasirani yangu! Ile ilinisaidia nianze kujifunza naye Biblia.”

Ukipenda kujua mambo mingi juu ya Adrián, soma Munara wa Mulinzi Na. 5 2016, ukurasa wa 14-15.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine