HABARI YA KUJIFUNZA YA 42
Uko “Tayari Kutii”?
“Hekima yenye inatoka juu ni . . . tayari kutii.”—YAK. 3:17.
WIMBO 101 Tutumike kwa Umoja
KIFUPI YA HABARIa
1. Juu ya nini inaweza kuwa nguvu kwetu kutii?
WAKATI fulani inakuwaka nguvu kwako kutii? Ile ilimufikia Mufalme Daudi, njo maana alimuomba Yehova hivi: “Uchochee ndani yangu utayari wa kukutii.” (Zb. 51:12) Daudi alimupenda Yehova. Hata vile, wakati fulani ilikuwa nguvu kwake kutii, na ni vile mambo inakuwaka pia kwetu. Juu ya nini? Kwanza, tuliriti muelekeo wa kutotii. Pili, Shetani anaendelea kujaribu kutuchochea tuasi, sawa vile yeye alifanya. (2 Ko. 11:3) Tatu, mu hii dunia tunazungukwa na watu wenye kuwa na muelekeo wa kutotii, “roho yenye sasa inatenda katika wana wa kukosa kutii.” (Efe. 2:2) Tunapaswa kujikaza sana ili kupiganisha muelekeo wetu wa kufanya zambi, lakini pia tunapaswa kujikaza ili kupiganisha roho ya kukosa kutii yenye Shetani na huu ulimwengu wanachochea. Tunapaswa kufanya yetu yote ili kumutii Yehova na wale wenye amepatia mamlaka fulani.
2. Kuwa “tayari kutii” maana yake nini? (Yakobo 3:17)
2 Soma Yakobo 3:17. Yakobo mwenye aliongozwa na roho ya Mungu aliandika kama watu wenye hekima wako “tayari kutii.” Fikiria maana ya ile maneno. Tunapaswa kupenda sana kutii wale wenye Yehova amepatia mamlaka fulani. Ni kweli kwamba, Yehova hatazamie tutii mutu mwenye anatuomba tuvunje sheria zake.—Mdo. 4:18-20.
3. Juu ya nini Yehova anapenda tutii wenye kuwa na mamlaka fulani juu yetu?
3 Inaweza kuwa mwepesi zaidi kwetu kumutii Yehova kuliko kutii mwanadamu. Kusema kweli, Yehova anatupatiaka tu muongozo wenye kukamilika. (Zb. 19:7) Lakini ni nguvu kwa wanadamu wenye mamlaka kufanya vile. Hata vile, Baba yetu wa mbinguni amepatia mamlaka fulani wazazi, wakubwa wa serikali, na wazee. (Mez. 6:20; 1 Te. 5:12; 1 Pe. 2:13, 14) Wakati tunawatii, ni Yehova njo mwenye tunatii. Tuone namna tunaweza kutii wanadamu wenye Yehova amepatia mamlaka, hata kama wakati fulani tunaweza kuona kama ni nguvu kukubali na kufuata muongozo wao.
TII WAZAZI WAKO
4. Juu ya nini vijana wengi hawatii wazazi wao?
4 Vijana Wakristo wanazungukwa na vijana wengine wenye wako na muelekeo wa ‘kutotii wazazi.’ (2 Ti. 3:1, 2) Juu ya nini vijana wengi hawatii wazazi? Wamoja wanaona kama wazazi wao ni wanafiki. Wanawaomba wafanye mambo yenye wao wenyewe wanashindwa kufanya. Wengine wanaona kama mashauri ya wazazi wao imepitwa na wakati, haifae, ao inawafunga sana. Kama uko kijana, na weye unaonaka vile? Vijana wengi wanaona kama ni nguvu kutii hii amri ya Yehova: “Mutii wazazi wenu katika umoja na Bwana, kwa maana hilo ni jambo la haki.” (Efe. 6:1) Ni nini inaweza kukusaidia kutii?
5. Juu ya nini inagusa moyo kuona kama Yesu alitii wazazi wake, sawa vile inaonyeshwa mu Luka 2:46-52?
5 Unaweza kujifunza kutii kupitia mufano muzuri zaidi wa Yesu. (1 Pe. 2:21-24) Yesu alikuwa mutu mukamilifu, lakini wazazi wake hawakukuwa wakamilifu. Hata vile, Yesu aliheshimia wazazi wake hata wakati walifanya makosa na wakati hawakumuelewa. (Kut. 20:12) Ona mambo yenye ilitokea wakati Yesu alikuwa na miaka 12. (Soma Luka 2:46-52.) Wazazi wake walimusahau Yerusalemu. Ilikuwa daraka ya Yosefu na Maria kuhakikisha kama watoto wao wote walikuwa mu kikundi ya watu wenye walikuwa wanasafiri kutoka Yerusalemu kisha sikukuu. Mwishowe wakati Yosefu na Maria walimupata Yesu, Maria alimulaumu kwa sababu ya wasiwasi yenye aliwaletea! Yesu angesema kama hawakukuwa na haki ya kumulaumu. Lakini hakufanya vile, alijibia wazazi wake kwa heshima. Yosefu na Maria, “hawakuelewa mambo yenye alikuwa anawaambia.” Hata vile, Yesu ‘aliendelea kujitiisha kwao.’
6-7. Ni nini inaweza kusaidia vijana kutii wazazi wao?
6 Kijana, inakuwaka nguvu kwako kutii wazazi wako wakati wanafanya makosa ao wakati hawakuelewe? Nini njo inaweza kukusaidia? Kwanza, fikiria namna Yehova anajisikia wakati unatii. Tena Biblia inasema kama wakati unatii wazazi wako, “hilo linamupendeza Bwana.” (Kol. 3:20) Yehova anaona wakati wazazi wako hawakuelewe ao wakati wazazi wako wanakutilia sheria zenye ziko nguvu kufuata. Lakini wakati unaamua kuwatii, unamufurahisha Yehova.
7 Pili, fikiria namna wazazi wako watajisikia wakati unatii. Wakati unatii wazazi wako, unawafurahisha na unafanya wakutumainie. (Mez. 23:22-25) Inawezekana utawakaribia zaidi. Alexandre, ndugu mwenye kuishi Belgique anasema hivi: “Wakati nilianza kutii zaidi wazazi wangu, uhusiano wetu ulibadilika, ukakuwa muzuri zaidi na tukakuwa na furaha zaidi.”b Tatu, fikiria namna kujifunza kutii kutakusaidia mu siku zenye kuya. Paulo, mwenye kuishi Brazili, anasema: “Kujifunza kutii wazazi wangu kumenisaidia kumutii Yehova na watu wengine wenye mamlaka.” Biblia inaonyesha juu ya nini ni jambo ya maana sana utii wazazi wako. Inasema hivi: “Ili mambo yakuendee muzuri na ukae wakati murefu katika dunia.”—Efe. 6:2, 3.
8. Juu ya nini vijana wengi wanaamua kutii wazazi wao?
8 Vijana wengi wameona kama wakati wanatii, mambo inawaendea muzuri. Ku mwanzo Luiza, mwenye kuishi pia Brazili, aliona kama ni nguvu kuelewa juu ya nini wazazi wake hawakumuruhusu kuwa na telefone kwa wakati fulani. Alijiuliza juu ya nini wazazi wake walimukatalia kuwa na telefone wakati vijana wengine wa miaka yake walikuwa nayo. Lakini kisha akaelewa kama wazazi wake walikuwa namulinda. Anasema sasa hivi: “Ninaona kutii wazazi sawa mipaka yenye kunilinda, hapana sawa ukuta wa gereza wenye kunifunga.” Wakati fulani Elizabeth, dada fulani wa Amerika, anaona kama ni nguvu kutii wazazi wake. Anasema hivi: “Wakati sielewe muzuri juu ya nini wazazi wangu wananitilia sheria fulani, nafikiria wakati wenye kufuata sheria ya wazazi wangu kulinilinda.” Monica, mwenye kuishi Armenia, anasema kama mambo inamuendea muzuri zaidi wakati anatii wazazi wake kuliko wakati hawatii.
TII “MAMLAKA ZENYE KUWA KUBWA”
9. Watu wengi wako na mawazo gani juu ya kutii sheria?
9 Watu wengi wanajua kama tuko na lazima ya wakubwa wa serikali na kama tunapaswa kutii sheria fulani zenye “mamlaka zenye kuwa kubwa” zinaweka. (Ro. 13:1) Lakini walewale watu wanasita kutii sheria zenye wanaona kuwa hazifae ao zenye zinawaomba mambo mingi. Kwa mufano, fikiria sheria ya kulipa kodi ao taxe. Mu uchunguzi wenye ulifanywa mu inchi fulani ya Ulaya watu wengi wenye waliulizwa waliamini kama “haiko muzuri kulipa taxe yenye unaona kama haifae.” Njo maana, mu ile inchi watu wanalipaka tu taxe fulani, hapana taxe zote zenye sheria inawaomba.
Mufano wa Yosefu na Maria unatufundisha nini juu ya utii? (Ona fungu ya 10-12)c
10. Juu ya nini tunatii hata sheria zenye hatufurahie?
10 Biblia inaonyesha kama serikali za wanadamu zinaongozwa na Shetani, zinaletea watu mateso, na kama hivi karibuni zitaharibiwa. (Zb. 110:5, 6; Muh. 8:9; Lu. 4:5, 6) Lakini inasema pia kama “mutu yeyote mwenye anapinga mamlaka amepinga mupango wa Mungu.” Kwa sasa Yehova ameruhusu serikali za wanadamu zitawale juu kukuwe utaratibu na anatuomba tutii zile serikali. Kwa hiyo, tunapaswa ‘kuwapatia wote haki zao,’ kutia ndani kulipa taxe, kuwaheshimia, na kuwatii. (Ro. 13:1-7) Tunaweza kuona sheria fulani kuwa haifae, haiko ya haki, ao iko nguvu kutii. Lakini tunamutii Yehova, na Yehova anatuomba tutii wenye mamlaka wakati hawatuombe tufanye jambo yenye inavunja sheria yake.—Mdo. 5:29.
11-12. Sawa vile Luka 2:1-6 inaonyesha, Yosefu na Maria walifanya nini ili kutii sheria hata kama haikukuwa mwepesi kufanya vile, na matokeo ilikuwa nini? (Ona pia picha.)
11 Mufano wa Yosefu na Maria unaweza kutufundisha mambo mingi. Walikuwa tayari kutii wenye mamlaka hata wakati haikukuwa mwepesi kwao kufanya vile. (Soma Luka 2:1-6.) Wakati Maria alikuwa na mimba ya karibu miezi kenda, walikutana na hali yenye ilijaribu utii wao. Mutawala wa Roma Augusto, aliamuru watu wote waandikishwe. Yosefu na Maria walipaswa kuenda kujiandikisha Betlehemu, safari ya kilometre 150 mu njia ya milima-milima. Ile safari haingekuwa mwepesi, zaidi sana kwa Maria. Pengine wangekuwa na wasiwasi juu ya usalama wa Maria na wa mutoto wao mwenye alikuwa angali mu tumbo. Mambo ingekuwa namna gani kama maumivu ya kuzala ingeanza na wako mu safari? Mu tumbo ya Maria mulikuwa mutoto mwenye angefikia kuwa Masiya. Ile ingekuwa sababu yenye ingefanya wasitii serikali?
12 Yosefu na Maria hawakuruhusu ile mambo yenye ilikuwa nawahangaisha iwazuie kutii ile sheria. Yehova alibariki utii wao. Maria alifika salama Betlehemu, akazaa mutoto mwenye afya ya muzuri, na hata akasaidia kutimiza unabii wa Biblia!—Mik. 5:2.
13. Kama tunatii, ile inaweza kuwa na matokeo gani juu ya ndugu zetu?
13 Wakati tunatii wenye mamlaka, tunapata faida na wengine pia wanapata faida. Namna gani? Kwanza, tunaepuka malipizi yenye wale wenye hawatii sheria wanapata. (Ro. 13:4) Wakati tunatii tunasaidia wenye mamlaka wakuwe na mawazo ya muzuri juu ya Mashahidi wa Yehova wote. Kwa mufano, miaka mingi yenye imepita katika inchi ya Nigeria, maaskari waliingia katika Jumba ya Ufalme wakati wa mikutano, walikuwa wanatafuta watu wenye walifanya maandamano ya kupinga kulipa taxe. Lakini mukubwa wa wale maaskari aliwaambia waondoke, alisema: “Mashahidi wa Yehova wanalipaka taxe.” Kila wakati unatii sheria, unaweza kufanya watu wakuwe na mawazo ya muzuri juu ya watu wa Mungu, na pengine siku moya ile itasaidiaka kulinda ndugu zako.—Mt. 5:16.
14. Ni nini ilisaidia dada fulani akuwe “tayari kutii” wenye mamlaka?
14 Lakini, wakati fulani tunaweza kujisikia kuwa hatupendi kutii wakubwa wa serikali. Joanna, dada mwenye kuishi Amerika, anasema hivi: “Ilikuwa nguvu sana kwangu kutii juu wakubwa wa serikali walitendeaka mubaya watu fulani wa mu familia yangu.” Lakini Joanna alijikaza kubadilisha mawazo yake. Kwanza, aliacha kusoma habari zenye zilikuwa ku site za kupashana habari zenye zilimuchochea kuwa na mawazo ya mubaya juu ya wakubwa wa serikali. (Mez. 20:3) Pili, alisali Yehova amusaidie ili amutumainie yeye kuliko kutumainia kama kutakuwa mabadiliko mu serikali ya wanadamu. (Zb. 9:9, 10) Tatu, alisoma habari mu vichapo vyetu zenye zilizungumuzia kuepuka kuunga mukono upande wowote. (Yoh. 17:16) Sasa Joanna anasema kama kuheshimia na kutii wenye mamlaka kumemufanya akuwe na “amani na mwenye kutulia kabisa.”
KUTII MUONGOZO WA TENGENEZO YA YEHOVA
15. Juu ya nini inaweza kuwa nguvu kwetu kutii muongozo wenye tengenezo ya Yehova inatutolea?
15 Yehova anatuomba ‘tutii wale wenye wanaongoza’ mu kutaniko. (Ebr. 13:17) Hata kama Kiongozi wetu Yesu ni mukamilifu, wale wenye anatumia ili kutuongoza hapa ku dunia hawako wakamilifu. Tunaweza kuona kama ni nguvu kuwatii, zaidi sana wakati wanatuomba tufanye jambo yenye hatupendi kufanya. Wakati fulani mutume Petro alisita kutii. Wakati malaika alimuambia akule wanyama wenye hawakukuwa safi kulingana na Sheria ya Musa, Petro alikatala; haiko mara moya tu, lakini mara tatu! (Mdo. 10:9-16) Juu ya nini? Aliona kama ule muongozo wa mupya haufae. Alizoea kufanya mambo mu njia tofauti. Kama ilikuwa nguvu kwa Petro kutii muongozo wa malaika mwenye ni mukamilifu, bila shaka inaweza kuwa nguvu zaidi kwetu kutii muongozo wa wanaume wenye hawako wakamilifu!
16. Hata kama pengine mutume Paulo aliona kuwa muongozo wenye alipewa haufae, alifanya nini? (Matendo 21:23, 24, 26)
16 Mutume Paulo alikuwa “tayari kutii” hata wakati alipewa muongozo wenye pengine aliona kama haufae. Wakristo Wayahudi walikuwa wamesikia habari za uongo kuhusu Paulo. Walisikia kama Paulo alikuwa nahubiria watu ‘waache sheria ya Musa’ na hakukuwa naheshimia ile Sheria. (Mdo. 21:21) Wanaume wazee katika Yerusalemu walimuomba Paulo aende pamoya na wanaume ine ku hekalu na ajitakase kulingana na desturi ili kuonyesha kama alikuwa anatii Sheria. Lakini Paulo alijua kama Wakristo hawakukuwa wanaishi tena chini ya Sheria na hakukuwa amefanya kosa yoyote. Hata vile, Paulo hakusita. “Siku yenye ilifuata Paulo akachukua wanaume hao na kujitakasa pamoja nao kulingana na desturi.” (Soma Matendo 21:23, 24, 26.) Utii wa Paulo ulifanya mu kutaniko mukuwe umoja.—Ro. 14:19, 21.
17. Mufano wa Stephanie unakufundisha nini?
17 Ilikuwa nguvu kwa dada mwenye kuitwa Stephanie kukubali uamuzi fulani wenye ndugu wenye kuongoza mu inchi yao walikamata. Yeye na bwana yake walikuwa wanatumikia kwa furaha mu kikundi ya luga ya kigeni. Kisha biro ya tawi ikasimamisha ile kikundi, na Stephanie na bwana yake wakatumwa mu kutaniko ya luga yao. Stephanie anasema hivi: “Ule uamuzi haukunifurahisha kabisa. Niliona kama mu kutaniko ya luga yetu hamukukuwa kabisa lazima kubwa ya wahubiri.” Hata vile, Stephanie aliamua kutegemeza ule muongozo mupya. Anasema hivi: “Kisha wakati nilifikia kuona kama ule uamuzi ulikuwa wa hekima. Tumefikia kuwa wazazi wa kiroho wa wengi mu kutaniko wenye watu wa familia zao hawako mu kweli. Niko najifunza Biblia na dada mwenye ameanza tena kutenda. Na sasa niko na wakati mingi zaidi kwa ajili ya funzo ya kipekee. Niko na zamiri safi juu ninajua kama nimefanya yangu yote ili kutii.”
18. Tunapata faida gani wakati tunatii?
18 Tunaweza kujifunza kutii. Yesu “alijifunza kutii,” hapana mu hali za muzuri lakini “kutokana na mambo yenye aliteseka.” (Ebr. 5:8) Kama Yesu, mara mingi tunajifunzaka kutii mu hali za nguvu. Kwa mufano, ku mwanzo-mwanzo wa ugonjwa wa Korona wakati tuliombwa kuacha kukusanyika ku Jumba ya Ufalme na kuacha kuhubiri nyumba kwa nyumba, je, ilikuwa nguvu kwako kutii? Hata vile, utii wako ulikulinda, ulisaidia mu kutaniko mukuwe umoja, na ulimufurahisha Yehova. Na sasa siye wote tumekuwa tayari zaidi kutii maagizo yoyote yenye tutapata mu kipindi ya taabu kubwa. Kutii ile maagizo kutaokoa uzima wetu!—Yob. 36:11.
19. Juu ya nini unapenda kuwa mutiifu?
19 Tumejifunza kama kutii kunaletaka baraka mingi. Lakini sababu kubwa yenye inatuchochea kumutii Yehova ni juu tunamupenda na tunapenda kumufurahisha. (1 Yo. 5:3) Hatutaweza kumulipa Yehova juu ya mambo yote yenye ametufanyia. (Zb. 116:12) Lakini tunaweza kumutii na kutii wale wenye kuwa na mamlaka juu yetu. Kama tunatii, tunaonyesha kama tuko na hekima. Na watu wenye hekima wanafurahisha moyo wa Yehova.—Mez. 27:11.
WIMBO 89 Tii juu Ubarikiwe
a Juu hatuko wakamilifu, wakati fulani inakuwaka nguvu kwetu siye wote kutii, hata wakati mwenye anatupatia muongozo iko na haki kabisa ya kufanya vile. Hii habari itazungumuzia faida zenye tutapata kama tunatii wazazi, “mamlaka zenye kuwa kubwa,” na ndugu wenye kuongoza mu kutaniko ya Kikristo.
b Ili kupata mapendekezo juu ya namna ya kuzungumuza na wazazi wako kuhusu sheria zenye unaona kama ziko nguvu kutii, ona habari yenye kuwa ku jw.org “Namna Gani Ninaweza Kuzungumuza na Wazazi Wangu Juu ya Sheria Zenye Waliweka?”
c MAFASIRIO YA PICHA : Yosefu na Maria walitii amri ya Kaisari ya kuenda kujiandikisha katika Betlehemu. Wakristo leo wanatii sheria za barabara, sheria za kulipa kodi, na sheria zenye “mamlaka zenye kuwa kubwa” zinaweka.