NAMNA YA KUJIFUNZA
Tayarisha Moyo Wako
Wakati tuko najifunza Biblia, tunapenda mawazo ya Yehova iguse kabisa moyo wetu. Ezra alituachia mufano muzuri kuhusu kufanya vile wakati ‘alitayarisha moyo wake ili kuchunguza Sheria ya Yehova.’ (Ezr. 7:10) Namna gani tunaweza kutayarisha moyo wetu?
Sali. Kila wakati unapenda kujifunza, sali kwanza. Umuombe Yehova akusaidie uelewe na utumikishe mambo yenye utajifunza.—Zb. 119:18, 34.
Ukuwe munyenyekevu. Yehova hafunulie mafundisho yake watu wenye kuwa na majivuno, wenye wanategemea akili yao. (Lu. 10:21) Epuka kufanya utafiti juu ya kupenda kushangaza wengine. Wakati mawazo yako haipatane na mawazo ya Mungu, kwa unyenyekevu badilisha mawazo yako.
Jaribu kusikiliza wimbo wa Ufalme. Muziki unagusaka sana moyo na kututayarisha kwa ajili ya ibada. Kusikiliza wimbo fulani wa Ufalme mbele ya kuanza kujifunza, kunaweza kukusaidia kutayarisha moyo wako.