HABARI YA KUJIFUNZA YA 37
WIMBO 114 “Mukuwe na Uvumilivu”
Mambo ya Kufanya Wakati Unaona Ukosefu wa Haki
“Aliendelea kutumaini haki, lakini angalia! kulikuwa ukosefu wa haki.”—ISA. 5:7.
WAZO KUBWA
Mufano wa Yesu unatusaidia tujue namna ya kutenda mu njia yenye itamufurahisha Yehova wakati tunaona ukosefu wa haki.
1-2. Batu mingi banatenda namna gani wakati banaona ukosefu wa haki, na tunaweza kujiuliza nini?
MU DUNIA ya leo munayala ukosefu wa haki. Kuko mambo mingi yenye inafanya batu batendewe mubaya. Kwa mufano batu banatendewa mubaya juu ni bamaskini, juu ya kwenye balitokea, juu ya rangi yabo ya Ngozi, ao juu ya sababu zingine. Batu mingi banateseka juu bakubwa ya politike na batajiri fulani biko naharibisha hewa na budongo juu tu ya makuta. Hii mambo yote na mambo ingine ya ukosefu wa haki, inatuletea siye bote mateso.
2 Leo batu mingi banakasirika wakati banaona ukosefu ya haki wenye uko mu dunia. Kila mutu anapendaka aishi kwa amani na atendewe kwa haki. Njo maana batu mingi banaingia mu bikundi byenye binapenda kubadilisha mambo. Banapinga batawala, banapinga sheria, na banachagula bakubwa ya politike benye banasema kama batatengeneza mambo. Lakini, sawa vile Biblia inatuambia, siye Bakristo ‘hatuko sehemu ya ulimwengu’ na tunatumainia kama Ufalme wa Mungu njo utamaliza ukosefu wote wa haki. (Yoh. 17:16) Hata vile, tunasikia huzuni na hata tunakasirika wakati tunaona mutu anatendewa bila haki. Tunaweza kujiuliza: ‘Nifanye nini? Kuko kitu yenye ninaweza kufanya leo kama ninaona ukosefu wa haki?’ Mbele tujibie ile maulizo, tuzungumuzie kwanza namna Yehova na Yesu banaona ukosefu wa haki.
YEHOVA NA YESU BANACHUKIA UKOSEFU WA HAKI
3. Juu ya nini tunasikiaka mubaya wakati tunaona ukosefu wa haki? (Isaya 5:7)
3 Biblia inatusaidia kujua juu ya nini tunachukiaka ukosefu wa haki. Ni juu Yehova alituumba kwa mufano wake na “anapenda uadilifu na haki.” (Zb. 33:5; Mwa. 1:26) Hatendeake batu bila haki, na hapendi mutu yeyote atendee mwingine bila haki! (Kum. 32:3, 4; Mik. 6:8; Zek. 7:9) Kwa mufano, wakati wa nabii Isaya, Yehova alisikiliza “kilio cha uchungu” cha Baisraeli bamingi benye balikuwa natendewa mubaya na Baisraeli benzabo. (Soma Isaya 5:7.) Yehova alipatia malipizi bale benye baliendelea kuvunja sheria yake na kutendea bengine bila haki.—Isa. 5:5, 13.
4. Yesu anajisikiaka namna gani wakati anaona mutu anatendewa mubaya? (Ona pia picha.)
4 Yesu naye anapenda haki na anachukia ukosefu wa haki. Siku moya wakati alikuwa ku dunia, aliona mwanaume fulani mwenye alikuwa na mukono wa kukauka. Yesu alimusikilia huruma na akamuponyesha, lakini viongozi wa dini walikasirika. Kuliko kufurahia vile ule mwanaume alipona, balisema kama Yesu alivunja sheria ya Sabato. Yesu alijisikia namna gani wakati Aliona vile balitenda? ‘Alihuzunika sana kwa sababu walikuwa na mioyo migumu.’—Mk. 3:1-6.
Bakubwa ba dini ya Kiyahudi habakusikilia huruma batu benye balikuwa na lazima ya musaada, lakini Yesu yeye alibasikilia huruma (Ona fungu ya 4)
5. Tunapaswa kukumbuka nini kuhusu kasirani?
5 Yehova na Yesu, bote banakasirikaka wakati banaona ukosefu wa haki. Kwa hiyo inaeleweka kama na siye tunakasirika wakati tunaona bya vile. (Efe. 4:26) Lakini, tukumbuke kama hata kama tuko na sheria ya kukasirika, haiko kasirani njo itamaliza ukosefu wa haki. Na hata, tukikasirika kwa wakati murefu tunaweza kugonjwa na kuvunjika moyo. (Zb. 37:1, 8; Yak. 1:20) Sasa tutafanya nini tukiona ukosefu wa haki? Mufano wa Yesu unaweza kutusaidia.
NAMNA YESU ALITENDA WAKATI ALIONA UKOSEFU WA HAKI
6. Wakati Yesu alikuwa ku dunia kulikuwa matendo gani ya ukosefu wa haki? (Ona pia picha.)
6 Wakati Yesu alikuwa ku dunia aliona namna batu mingi balitendewa bila haki. Aliona namna viongozi wa dini walitendea mubaya batu ya hali ya chini. (Mt. 23:2-4) Aliona pia namna viongozi wa Roma balitendea batu mubaya. Bayahudi bamingi balipenda batoke chini ya utawala ya Roma. Na hata Bayahudi fulani, sawa vile Bazeloti, balikuwa tayari kupigania uhuru wao. Lakini, Yesu hakuanzisha wala kuunga mukono kikundi yoyote yenye ilipenda kubadilisha mambo. Wakati alijua kama batu banapanga kumufanya kuwa mufalme, alitoka pale na kuenda fasi ingine.—Yoh. 6:15.
Yesu hakuitika bengine bamuingize mu mambo ya politike (Ona fungu ya 6)
7-8. Juu ya nini Yesu hakujaribu kumaliza ukosefu wa haki wakati alikuwa ku dunia? (Yohana 18:36)
7 Wakati Yesu alikuwa ku dunia, hakujiingiza mu mambo ya politike ili kujaribu kumaliza ukosefu wa haki. Juu ya nini? Ni juu alijua kama banadamu habana haki wala uwezo wa kujitawala. (Zb. 146:3; Yer. 10:23) Na alijua kama inaomba kushambulia njo mizizi ya ukosefu wa haki, ni kusema byenye binafanya kukuwe ukosefu wa haki; japo banadamu habana ule uwezo. Ni nini kabisa njo mizizi ya ukosefu wa haki? Kuko ukosefu wa haki juu ulimwengu unatawaliwa na Shetani Ibilisi, mwenye hana huruma na anachochea batu batendeane bila haki. (Yoh. 8:44; Efe. 2:2) Tena juu hatukamilike haiwezekane mutu atende kwa haki kila mara hata kama ni mutu muzuri.—Mhu. 7:20.
8 Yesu alijua kama ni Ufalme wa Mungu tu njo utaongola kabisa mizizi ya ukosefu wa haki. Njo maana alitumikisha wakati yake na nguvu yake juu ya ‘kuhubiri na kutangaza habari njema ya Ufalme wa Mungu.’ (Lu. 8:1) Alihakikishia “wale wenye njaa na kiu ya haki” kama ukosefu wa haki na mateso bitaisha. (Mt. 5:6; Lu. 18:7, 8) Lakini, haiko serikali za banadamu njo zitamaliza ile mambo, ni Ufalme wa Mungu wenye “hauko sehemu ya ulimwengu huu.”—Soma Yohana 18:36.
TUIGE YESU WAKATI TUNAONA UKOSEFU WA HAKI
9. Nini njo inakuhakikishia kama ni Ufalme wa Mungu tu njo utamaliza ukosefu wa haki?
9 Juu tunaishi mu “siku za mwisho,” tunaona mambo ya mingi ya ukosefu wa haki kupita yenye Yesu aliona wakati alikuwa ku dunia. Lakini mizizi ya ukosefu wa haki ingali ileile, ni kusema Shetani na batu babaya. (2 Ti. 3:1-5, 13; Ufu. 12:12) Sawa Yesu, tunajua kama ni Ufalme wa Mungu tu njo utaongola ile mizizi. Ufalme wa Mungu tu njo tunaunga mukono. Njo maana hatuunge mukono serikali za banadamu ao kutumainia kama zile serikali njo zitamaliza ukosefu wa haki. Fikiria mufano wa dada Stacy.a Mbele ajifunze kweli alikuwa mu kikundi fulani yenye ilijaribu kubadilisha mambo. Lakini alianza kushakia mambo yenye alikuwa nafanya. Anasema hivi: “Wakati tulikuwa napinga serikali, nilikuwa najiuliza ikiwa kufanya vile njo kutatengeneza mambo. Lakini sasa, juu ninaunga Ufalme wa Mungu mukono, niko hakika kama Ufalme wa Mungu njo utamaliza mateso yote. Ninajua kama Yehova atapigania kila mutu mwenye anatendewa mubaya kupita vile miye ningefanya.”—Zb. 72:1, 4.
10. Juu ya nini bikundi bya kupinga serikali habipatane na mafundisho ya Yesu yenye iko mu Matayo 5:43-48? (Ona pia picha.)
10 Leo batu mingi banajiunga na bikundi byenye binajaribu kubadilisha serikali. Lakini bamingi kati yabo banafikia kukasirika, kuvunja sheria, na kutendea batu bengine mubaya. Tabia za vile hazipatane na mambo yenye Yesu alifundisha. (Efe. 4:31) Ndugu mwenye kuitwa Jeffrey anasema hivi: “Ninajua kama wakati batu banafanya maandamano, mambo inaweza kuharibika haraka na banaweza kuanza kutendeana mubaya, kuiba, na kuharibisha bitu.” Lakini, Yesu alifundisha kama tunapaswa kutendea batu yote kwa upendo, hata bale benye banatupinga ao kututesa. (Soma Matayo 5:43-48.) Juu tuko Bakristo, tunafanya yetu yote juu tuepuke kufanya jambo yoyote yenye itaonyesha kama hatumuige Yesu.
Inaomba kujikaza juu mutu asijiingize mu mambo ya politike, ao kujiunga na bikundi byenye kujaribu kutetea haki za batu (Ona fungu ya 10)
11. Juu ya nini wakati fulani inaweza kuwa nguvu kuiga Yesu?
11 Tunajua kama ni Ufalme wa Mungu njo utamaliza kabisa ukosefu wa haki. Lakini inaweza kuwa nguvu kwetu kuiga Yesu wakati banatutendea bila haki. Fikiria mambo yenye ilifikia dada Janiya, mwenye balibagua juu ya rangi yake ya ngozi. Anasema hivi: “Nilisirika sana. Niliumia na nilipenda bale batu bapewe malipizi. Kisha nilifikiria kuunga mukono kikundi fulani ya kupinga ubaguzi wa rangi ya ngozi. Niliwaza kama kufanya vile kutasaidia.” Lakini kisha wakati, Janiya aliona kama iliomba abadilike. Anasema hivi: “Nilikuwa naacha bengine bachochee mawazo yangu na kunifanya nitumainie banadamu kuliko kumutumainia Yehova. Niliamua kuachana na batu benye balikuwa na mawazo ya vile.” Hata kama tuko na sheria ya kukasirika, tunapaswa kuwa baangalifu juu tusijiingize mu mambo ya politike ya hii dunia ao kuunga mukono bikundi fulani.—Yoh. 15:19.
12. Juu ya nini tunapaswa kuchagua habari zenye tutafuata?
12 Nini njo itatusaidia tubakie benye kutulia wakati banatutendea bila haki ao wakati tunaona bengine banatendewa bila haki? Jambo moya yenye inaweza kutusaidia ni kukuwa baangalifu wakati tunachagua habari za kusoma, za kusikiliza, na za kuangalia. Habari fulani zenye zinatiliwa ku Enternete, zinatayarishwa mu njia yenye itafanya batu bashituke na zinachochea batu kupinga serikali. Mara mingi batu ba kutoa habari banasemaka njo mawazo yabo, habasemake vile mambo ilikuwa kabisa. Na hata kama banasema kweli, unawaza kuendelea kufikiria sana ile mambo njo kutasaidia? Kama tunapitisha wakati mingi na tuko nasikiliza ao kusoma habari za vile, tutavunjika tu moyo na kukasirika zaidi. (Mez. 24:10) Na hata, tunaweza kusahau kama ni Ufalme wa Mungu tu njo utamaliza ukosefu wa haki.
13. Namna gani kuwa na programe ya muzuri ya kusoma Biblia kutatusaidia tujue bya kufanya wakati tunaona ukosefu wa haki?
13 Kusoma Biblia kila siku na kutafakari kunaweza tusaidia tujue bya kufanya wakati tunaona ukosefu wa haki. Dada mwenye kuitwa Alia alisikia mubaya sana wakati aliona vile batu fulani ba mu eneo yabo balikuwa natendewa mubaya. Na ilionekana kama bale benye balikuwa natendeana mubaya habakupewa malipizi. Anasema hivi: “Nilitulia kwanza na kujiuliza, ‘Niko hakika kabisa kama Yehova atatengeneza hii mambo?’ Ni ile wakati njo nilisoma Yobu 34:22-29. Ile andiko ilinikumbusha kama Yehova anaonaka kila mutu. Ni yeye tu njo anajua muzuri zaidi namna ya kuhukumu kwa haki, na ni yeye njo iko na uwezo wa kutengeneza kabisa mambo.” Lakini wakati tuko nachunga Ufalme wa Mungu utengeneze mambo, tutafanya nini leo wakati tunaona ukosefu wa haki?
MAMBO YENYE TUNAWEZA KUFANYA LEO
14. Siye tunaweza kufanya nini leo? (Wakolosai 3:10, 11)
14 Hatuna uwezo wa kubadilisha matendo ya batu, lakini tunaweza kuamua namna siye tutatenda. Sawa vile tumeona, tunaiga Yesu wakati tunaonyesha bengine upendo. Upendo unaweza kutuchochea tutendee batu yote kwa heshima, hata benye biko natendea bengine mubaya. (Mt. 7:12; Ro. 12:17) Yehova anafurahi wakati tunatendea batu yote kwa upendo na kwa haki.—Soma Wakolosai 3:10, 11.
15. Wakati tunafundisha batu kweli za Biblia ile inakuwa na matokea gani juu ya ukosefu wa haki?
15 Jambo ya muzuri zaidi yenye tunaweza kufanya wakati tunaona ukosefu wa haki ni kuhubiria bengine kweli za Biblia. Juu ya nini? Ni juu “ujuzi juu ya Yehova” unaweza kubadilisha mutu mwenye alikuwa mukali na mwenye jeuri, na kumufanya kuwa mutu muzuri mwenye anapenda amani. (Isa. 11:6, 7, 9) Kwa mufano, mbele mwanaume mwenye jina yake ni Jemal ajifunze kweli, aliingia mu kikundi yenye ilikuwa napiganisha serikali ya inchi yabo juu aliona kama ile serikali ilikuwa natesa batu. Jemal anasema hivi: “Hauwezi badilisha mutu kinguvu. Miye sikubadilikaka kinguvu, lakini ni kweli ya Biblia yenye nilikuwa najifunza njo ilinibadilisha.” Mambo yenye Jemal alijifunza ilimuchochea aache kupigana. Kwa hiyo, kama batu mingi banajifunza Biblia na kubadilika, ni kusema batu ba kutendeana bila haki batapunguka.
16. Juu ya nini unapenda kuambia bengine juu ya mambo yenye Ufalme wa Mungu utafanya?
16 Sawa Yesu, tuko na hamu ya kuambia bengine kama Ufalme wa Mungu tu njo utamaliza ukosefu wa haki. Kujua vile kunatia moyo benye bametendewa bila haki. (Yer. 29:11) Stacy, mwenye tulizungumuzia, anasema hivi: “Kujifunza kweli kunanisaidia nibakie mwenye kutulia wakati bananitendea bila haki ao wakati ninaona bengine banatendewa bila haki. Yehova anatumikisha Biblia juu ya kutufariji.” Inaomba tujitayarishe muzuri juu tuweze kuhubiria bengine ujumbe wenye kufariji wenye kuwa mu Biblia. Kama unaamini kabisa mambo yenye Biblia inasema juu ya ukosefu wa haki yenye tumejifunza mu hii habari, itakuwa mwepesi zaidi kwako kuizungumuzia na bengine, ikuwe ku masomo ao ku kazi.b
17. Namna gani Yehova anatusaidia kujua namna ya kutenda wakati tunaona ukosefu wa haki?
17 Tunajua kama wakati wote wenye Shetani ataendelea kuwa “mutawala wa ulimwengu huu” tutatendewa bila haki. Lakini Yehova hatuachilie, anatusaidia na anatupatia tumaini, anatuambia kama Shetani “atatupwa inje.” (Yoh. 12:31) Kupitia Biblia, Yehova anatuambia juu ya nini kuko mambo mingi ya ukosefu wa haki na namna anajisikia wakati tunateseka juu ya ukosefu wa haki. (Zb. 34:17-19) Kupitia Mwana wake, Yehova anatufundisha namna ya kutenda wakati tunaona ukosefu wa haki na namna, hivi karibuni, Ufalme wake utamaliza kabisa-kabisa ukosefu wa haki. (2 Pe. 3:13) Tuendelee basi kuhubiri kwa bidii habari njema kuhusu ule Ufalme, na kungoya kwa hamu wakati wenye dunia yote itayala “haki na uadilifu.”—Isa. 9:7.
WIMBO 158 “Itafika tu!”
a Majina fulani imebadilishwa.
b Ona pia Nyongeza ya A nukta ya 24-27 mu broshua Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi.