‘Tuendeleze Umoja wa Roho’
MUTUME Paulo aliambia Bakristo Baefeso baendelee ‘kuvumiliana katika upendo, bajikaze sana kuendeleza umoja wa roho katika kifungo chenye kuunganisha cha amani.’—Efe. 4:2, 3.
“Umoja” wenye tunafurahia ni “wa roho.” Ile inamaanisha kama ni nguvu ya utendaji ya Mungu njo inatuwezesha kuwa na umoja. Lakini, sawa vile Paulo alionyesha, tunapaswa kujikaza sana juu ya kuendeleza ao kulinda umoja wetu. Ni kusema, kila Mukristo anapaswa kufanya sehemu yake juu ya “kuendeleza umoja wa roho.”
Wazia hii jambo: Mutu fulani anakupatia zawadi ya gari ya mupya. Unawaza kazi ya kuihangaikia itakuwa ya nani? Jibu iko wazi. Hautamulaumu ule mwenye alikupatia ile gari kama ile gari inaharibika juu haukuihangaikia.
Vilevile, umoja wetu wa Kikristo ni zawadi ya Mungu. Ni daraka ya kila mumoya wetu kuilinda. Kama hatupatane na ndugu ao dada yetu, tunapaswa kujiuliza hivi: ‘Ninafanya yangu yote juu ya kulinda umoja wa roho kwa kurudisha amani?’
‘TUJIKAZE SANA KUENDELEZA UMOJA’
Sawa vile mutume Paulo alionyesha, wakati fulani inaomba kujikaza sana juu ya kulinda umoja wetu, zaidi sana wakati ndugu ao dada anatukosea. Juu ya kulinda umoja, ni lazima tuongee na mutu mwenye alitukosea na kumuambia vile tuko najisikia? Wakati fulani haiko lazima. Ujiulize hivi: ‘Kama ninaongea naye, ile itatengeneza mambo ao itafanya mambo ikuwe mubaya zaidi?’ Wakati fulani, ni jambo ya hekima kuacha tu bipite vile ao kusamehe tu ule mutu.—Mez. 19:11; Mk. 11:25.
Ujiulize hivi: ‘Kama ninaongea naye, ile itatengeneza mambo ao itafanya mambo ikuwe mubaya zaidi?’
Sawa vile Paulo aliandika, tuendelee ‘kuvumiliana kwa upendo.’ (Efe. 4:2) Kitabu moya inasema kama ile maneno inaweza kutafsiriwa hivi: “Kukubali bengine vile biko.” Ile inamaanisha kama tunakubali kama baamini benzetu banafanyaka makosa sawa vile tu siye. Njo maana, siye bote tunajikaza kuvala “utu mupya.” (Efe. 4:23, 24) Hata vile, hakuna mutu kati yetu mwenye anaweza kufanya mambo yote muzuri bila kukosea. (Ro. 3:23) Kama tunaelewa ile, itakuwa mwepesi kwetu kuvumiliana na kusameheana, na ile itafanya ‘tuendeleze umoja wa roho.’
Tunaweza kuwa na “kifungo chenye kuunganisha cha amani” mu kutaniko, kama tunasamehe na kusaabu makosa ya bengine. Neno ya kigiriki yenye kutafsiriwa “kifungo chenye kuunganisha” mu Waefeso 4:3 inatafsiriwa “mishipa” mu Wakolosai 2:19. Sawa vile tu mishipa inaunganishaka mifupa, amani na pia upendo kwa bandugu na badada yetu itasaidia tulinde uhusiano wetu pamoya nabo, hata kama wakati fulani banatukosea.
Wakati baamini benzetu banatukosea ao banatusirikisha, tujikaze kubaelewa kuliko kukazia tu makosa yabo. (Kol. 3:12) Siye bote hatukamilike, wakati fulani na siye tunaweza kukosea bengine mu njia fulani. Kukumbuka ile kutatusaidia tufanye sehemu yetu juu ya “kuendeleza umoja wa roho.”