Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mrt habari 48
  • Dini na Vita mu Ukraine—Biblia Inasema Nini?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Dini na Vita mu Ukraine—Biblia Inasema Nini?
  • Habari Zingine
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Historia ya dini kuhusu mambo ya vita
  • Wakristo wanapaswa kuunga mukono vita?
  • Nini njo itapata dini zenye zinaunga mukono vita?
  • Mawazo ya Wakristo juu ya Vita—Biblia Inasema Nini?
    Habari Zingine
  • Mwaka Moya Inaenea Tangu Vita Ianze mu Ikrene​—Ni Tumaini Gani Yenye Biblia Inatoa?
    Habari Zingine
  • Urusi Inashambulia Ukraine
    Habari Zingine
  • 2022: Mwaka wa Wasiwasi​—Biblia inasema Nini?
    Habari Zingine
Ona Habari Zaidi
Habari Zingine
mrt habari 48
Picha: 1. Patriarche Kirill wa Moscou, Urusi. 2. Askofu Mukubwa wa Kiev, Ukraine.

MUENDELEE KUKESHA!

Dini na Vita mu Ukraine—Biblia Inasema Nini?

Fikiria mambo yenye kufuata kuhusu viongozi wa dini wenye kuheshimiwa na kuhusu vita mu Ukraine:

  • “Kiongozi mukubwa wa Dini ya Ortodoksi ya Urusi, Patriarche Kirill, hayasema kitu kuhusu Urusi kushambulia Ukraine. . . . Kanisa yake imeendelea kueneza habari za uongo kuhusu Ukraine na Poutine ametumia zile habari juu ya kuonyesha kama iko na sababu ya kushambulia Ukraine.”—EUobserver, tarehe 7, Mwezi 3, 2022.

  • “Patriarche Kirill . . . ametetea sana Urusi kushambulia Ukraine kwa kusema kama ile vita ni kati ya mambo yenye inaomba kufanya juu ya kupiganisha zambi.”—AP News, tarehe 8, Mwezi wa 3, 2022.

  • “Siku ya Kwanza, kiongozi mukubwa wa Kanisa ya Ortodoksi ya Ukraine, Askofu Mukubwa wa Kiev, alibariki watu wake juu ‘wapigane na maaskari wa Urusi’ . . . [Alisema] pia kama kuua maaskari wa Urusi haiko zambi.”—Jerusalem Post, tarehe 16, Mwezi wa 3, 2022.

  • “Siye [Baraza ya Makanisa na Matengenezo ya Kidini ya Ukraine (UCCRO)] tuko ngambo ya Jeshi ya Ukraine na wale wote wenye kutupigania, tunawabariki juu wako napigania Ukraine, na tuko nawaombea kwa Mungu.”—Maneno ya UCCRO,a tarehe 24, Mwezi wa 2, 2022.

Unawaza nini? Dini zenye zinasema kama zinamufuata Yesu Kristo zinapaswa kuchochea waamini wake waende ku vita? Biblia inasema nini?

Historia ya dini kuhusu mambo ya vita

Historia inaonyesha kama, mara mingi dini imekubali, imetetea, ao hata kutia watu moyo waende kupigana vita hata kama dini inasema iko pale juu ya amani. Kwa miaka mingi, Mashahidi wa Yehova wameonyesha waziwazi matendo ya vile ya unafiki wa Kidini. Ona mifano fulani yenye kuzungumuziwa mu vichapo vyetu.

  • Habari “Zile Krusedi—‘Uwongo Wenye Msiba’” inaonyesha namna Kanisa Katoliki ya Roma ilishiriki mu mauaji na ilisema kama ile yote ni kumutumikia Mungu na Kristo.

  • Habari “Kanisa Katoliki Katika Afrika” inaonyesha namna dini ilishindwa kuzuia vita ya kikabila, na hata mauaji.

  • Habari “Je, Dini Inapaswa Kulaumiwa?,” “Fungu la Dini Katika Vita vya Binadamu,” na “Dini Yajiunga” zinafasiria namna viongozi wa dini ya Katoliki, Ortodoksi, na Kiprotestanti wameunga mukono pande mbili za vita mingi.

Wakristo wanapaswa kuunga mukono vita?

Mambo yenye Yesu alifundisha: “Unapaswa kumupenda jirani yako kama wewe mwenyewe.” (Matayo 22:39) “Muendelee kupenda maadui wenu.”—Matayo 5:44-47.

Waza kidogo: Dini inaweza kusema kama iko natii amri ya Yesu ya kupendana wakati iko natia waamini wake moyo waue wengine mu vita? Juu ya kupata jibu, soma habari “Wakristo wa Kweli na Vita” na “Je, Inawezekana Kuwapenda Adui Zako?”

Mambo yenye Yesu alisema: “Ufalme wangu hauko sehemu ya ulimwengu huu. Kama Ufalme wangu ungekuwa sehemu ya ulimwengu huu, watumishi wangu wangepigana ili nisitiwe katika mikono ya Wayahudi.” (Yohana 18:36) “Wote wenye wanatumikisha upanga watakufa kwa upanga.”—Matayo 26:47-52.

Waza kidogo: Wakristo hawakupaswa kupigana hata juu ya kulinda Yesu. Sasa, unawaza kuko kabisa sababu yenye inaweza kufanya wapigane? Soma habari “Je, Ukristo Unaunga Mkono Vita?” juu ya kuona namna Wakristo wa kwanza-kwanza walifuata kwa uaminifu mufano wa Yesu na mafundisho yake.

Nini njo itapata dini zenye zinaunga mukono vita?

Biblia inafundisha kama Mungu hafurahie wale wenye wanasema kama wanamufuata Yesu, lakini hawafuate mafundisho yake.—Matayo 7:21-23; Tito 1:16.

  • Kitabu ya Ufunuo inaonyesha kama Mungu anaona kuwa zile dini ziko na deni ya damu “ya wale wote wenye wameuawa katika dunia.” (Ufunuo 18:21, 24) Juu ya kujua sababu, soma habari “Babiloni Mkubwa Ni Nani?”

  • Yesu alionyesha kama dini zote zenye hazimufurahishe Mungu zitaharibiwa juu ya matendo yao ya mubaya, sawa vile tu muti wenye kuoza wenye unazala matunda ya kuoza “unakatwa na kutupwa katika moto.” (Matayo 7:15-20) Soma habari “Mwisho wa Dini ya Uwongo Unakaribia!” juu ya kujua namna ile mambo itatokea.

Mashahidi wa Yehova wako tofauti

Mu Urusi na mu Ukraine, sawa vile mu sehemu zingine za dunia, Mashahidi wa Yehova wanatii amri ya Yesu ya kutounga mukono upande wowote mu mambo ya politike na ya kutojiingiza mu vita. Njo maana, hatuendake ku vita ao kuunga mukono vita yoyote. Mashahidi fulani wa Yehova wako wanateswa juu ya kushikamana na mambo yenye wanaamini. (Yohana 15:19, 20; 2 Timoteo 3:12) Kwa mufano, serikali ya Urusi imefunga Mashahidi wengi na hata kutesa wamoja. Imenyanganya majengo yetu ya ibada. Juu ya kupata habari zaidi, fungula www.jw-russia.org.

  • Angalia video ya dakika ine Les Témoins de Jéhovah d’Irkoutsk restent fidèles malgré des perquisitions brutales juu ya kuona namna Mashahidi wa Yehova mu Urusi wako nateswa juu ya imani yao.

  • Mashahidi wa Yehova wanajulikana kuwa watu wenye hawaunge mukono upande wowote mu mambo ya politike. Angalia video Fermes face à l’opposition juu ya kuona namna hawakuunga mukono upande wowote hata kama waliteswa sana mu Alemanye ya Wanazi na mu Muungano wa Sovieti.

Tafazali, fungula site yetu ya Enternete juu ujifunze mambo mingi kuhusu imani yetu, na pia ahadi (ao malako) ya Biblia yenye kuonyesha kama kuko siku vita itaishaka. (Isaya 2:4; Yeremia 29:11) Tunakuomba upashane habari na siye juu ya kujua mambo mingi zaidi.

Kwenye tulitosha picha, kushoto kuenda kuume: Picha ya Sefa Karacan/Anadolu Agency/Getty Images; Maxym Marusenko/NurPhoto via Getty Images

a UCCRO, ao Baraza ya Makanisa na Matengenezo ya Kidini ya Ukraine, iko na makanisa 15. Kuko kanisa ya Ortodoksi, ya Katoliki ya Ugiriki, ya Katoliki ya Roma, ya Kiprotestanti, makanisa ya Kievanjeli, ya Wayahudi na ya Waislamu.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine