MUENDELEE KUKESHA!
Dini na Vita mu Ukraine—Biblia Inasema Nini?
Fikiria mambo yenye kufuata kuhusu viongozi wa dini wenye kuheshimiwa na kuhusu vita mu Ukraine:
“Kiongozi mukubwa wa Dini ya Ortodoksi ya Urusi, Patriarche Kirill, hayasema kitu kuhusu Urusi kushambulia Ukraine. . . . Kanisa yake imeendelea kueneza habari za uongo kuhusu Ukraine na Poutine ametumia zile habari juu ya kuonyesha kama iko na sababu ya kushambulia Ukraine.”—EUobserver, tarehe 7, Mwezi 3, 2022.
“Patriarche Kirill . . . ametetea sana Urusi kushambulia Ukraine kwa kusema kama ile vita ni kati ya mambo yenye inaomba kufanya juu ya kupiganisha zambi.”—AP News, tarehe 8, Mwezi wa 3, 2022.
“Siku ya Kwanza, kiongozi mukubwa wa Kanisa ya Ortodoksi ya Ukraine, Askofu Mukubwa wa Kiev, alibariki watu wake juu ‘wapigane na maaskari wa Urusi’ . . . [Alisema] pia kama kuua maaskari wa Urusi haiko zambi.”—Jerusalem Post, tarehe 16, Mwezi wa 3, 2022.
“Siye [Baraza ya Makanisa na Matengenezo ya Kidini ya Ukraine (UCCRO)] tuko ngambo ya Jeshi ya Ukraine na wale wote wenye kutupigania, tunawabariki juu wako napigania Ukraine, na tuko nawaombea kwa Mungu.”—Maneno ya UCCRO,a tarehe 24, Mwezi wa 2, 2022.
Unawaza nini? Dini zenye zinasema kama zinamufuata Yesu Kristo zinapaswa kuchochea waamini wake waende ku vita? Biblia inasema nini?
Historia ya dini kuhusu mambo ya vita
Historia inaonyesha kama, mara mingi dini imekubali, imetetea, ao hata kutia watu moyo waende kupigana vita hata kama dini inasema iko pale juu ya amani. Kwa miaka mingi, Mashahidi wa Yehova wameonyesha waziwazi matendo ya vile ya unafiki wa Kidini. Ona mifano fulani yenye kuzungumuziwa mu vichapo vyetu.
Habari “Zile Krusedi—‘Uwongo Wenye Msiba’” inaonyesha namna Kanisa Katoliki ya Roma ilishiriki mu mauaji na ilisema kama ile yote ni kumutumikia Mungu na Kristo.
Habari “Kanisa Katoliki Katika Afrika” inaonyesha namna dini ilishindwa kuzuia vita ya kikabila, na hata mauaji.
Habari “Je, Dini Inapaswa Kulaumiwa?,” “Fungu la Dini Katika Vita vya Binadamu,” na “Dini Yajiunga” zinafasiria namna viongozi wa dini ya Katoliki, Ortodoksi, na Kiprotestanti wameunga mukono pande mbili za vita mingi.
Wakristo wanapaswa kuunga mukono vita?
Mambo yenye Yesu alifundisha: “Unapaswa kumupenda jirani yako kama wewe mwenyewe.” (Matayo 22:39) “Muendelee kupenda maadui wenu.”—Matayo 5:44-47.
Waza kidogo: Dini inaweza kusema kama iko natii amri ya Yesu ya kupendana wakati iko natia waamini wake moyo waue wengine mu vita? Juu ya kupata jibu, soma habari “Wakristo wa Kweli na Vita” na “Je, Inawezekana Kuwapenda Adui Zako?”
Mambo yenye Yesu alisema: “Ufalme wangu hauko sehemu ya ulimwengu huu. Kama Ufalme wangu ungekuwa sehemu ya ulimwengu huu, watumishi wangu wangepigana ili nisitiwe katika mikono ya Wayahudi.” (Yohana 18:36) “Wote wenye wanatumikisha upanga watakufa kwa upanga.”—Matayo 26:47-52.
Waza kidogo: Wakristo hawakupaswa kupigana hata juu ya kulinda Yesu. Sasa, unawaza kuko kabisa sababu yenye inaweza kufanya wapigane? Soma habari “Je, Ukristo Unaunga Mkono Vita?” juu ya kuona namna Wakristo wa kwanza-kwanza walifuata kwa uaminifu mufano wa Yesu na mafundisho yake.
Nini njo itapata dini zenye zinaunga mukono vita?
Biblia inafundisha kama Mungu hafurahie wale wenye wanasema kama wanamufuata Yesu, lakini hawafuate mafundisho yake.—Matayo 7:21-23; Tito 1:16.
Kitabu ya Ufunuo inaonyesha kama Mungu anaona kuwa zile dini ziko na deni ya damu “ya wale wote wenye wameuawa katika dunia.” (Ufunuo 18:21, 24) Juu ya kujua sababu, soma habari “Babiloni Mkubwa Ni Nani?”
Yesu alionyesha kama dini zote zenye hazimufurahishe Mungu zitaharibiwa juu ya matendo yao ya mubaya, sawa vile tu muti wenye kuoza wenye unazala matunda ya kuoza “unakatwa na kutupwa katika moto.” (Matayo 7:15-20) Soma habari “Mwisho wa Dini ya Uwongo Unakaribia!” juu ya kujua namna ile mambo itatokea.
Kwenye tulitosha picha, kushoto kuenda kuume: Picha ya Sefa Karacan/Anadolu Agency/Getty Images; Maxym Marusenko/NurPhoto via Getty Images
a UCCRO, ao Baraza ya Makanisa na Matengenezo ya Kidini ya Ukraine, iko na makanisa 15. Kuko kanisa ya Ortodoksi, ya Katoliki ya Ugiriki, ya Katoliki ya Roma, ya Kiprotestanti, makanisa ya Kievanjeli, ya Wayahudi na ya Waislamu.