Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g 10/15 uku. 3-6
  • Maulizo Tatu Watu Wangependa Kuuliza Mungu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo Tatu Watu Wangependa Kuuliza Mungu
  • Amuka!—2015
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • 1 “SABABU GANI UNAACHA WATU WATESEKE?”
  • 2 “SABABU GANI DINI INAJAA UNAFIKI?”
  • 3 “SABABU GANI TUKO HAPA DUNIANI?”
  • Biblia Inafundisha Nini juu ya Mungu?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Biblia Inasema Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Mungu Ni Nani?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2015
g 10/15 uku. 3-6
Mwanaume mumoja anaangalia maisha ya wanadamu, dini, na ulimwengu wote

HABARI KUBWA

Maulizo Tatu Watu Wangependa Kuuliza Mungu

MAULIZO ya Susan juu ya Mungu yalianza alipokuwa na miaka saba; Al, rafiki yake wa miaka kenda, aliingizwa katika hospitali kwa sababu ya polio na aliwekwa katika mashini ya kusaidia kupumua. Susan aliandika juu ya mambo alijionea maishani katika gazeti The New York Times la tarehe 6 Mwezi wa 1, 2013.

Kisha kutembelea Al katika hospitali, Susan aliuliza mama yake hivi: “Sababu gani Mungu anaweza kutendea hivyo mutoto mudogo?”

Mama yake akamujibia hivi: “Padri anaweza kusema kama Mungu anapaswa kuwa na sababu zake, lakini sijue sababu hizo.”

Miaka mbili kisha hapo, katika mwaka wa 1954, Jonas Salk alivumbua ndui ya polio, na mama ya Susan akasema pengine ni Mungu alimuongoza katika uchunguzi huo.

Susan alijibu hivi: “Mungu angepaswa kuongoza waganga zamani ili Al asikuwe katika mashini ya kusaidia kupumua.”

Susan alieleza kwa kifupi jambo alijionea alipokuwa mutoto. Aliandika hivi: “[Al] alikufa miaka munane tu kisha hapo, wakati huo nilikuwa nimeamini kabisa kama hakuna Mungu.”

Kama Susan, watu wengi wenye wamepatwa na taabu ao wenye wameona wengine wanapatwa na taabu, wanashindwa kupata majibu ya kufurahisha juu ya maulizo yao kuhusu Mungu. Hilo linafanya wengine waamini kama hakuna Mungu. Watu wengine hawawezi kuamini kabisa kama hakuna Mungu, lakini wanakuwa na mashaka juu yake.

Haiko kusema kama watu wanaoamini kama hakuna Mungu na watu wenye mashaka juu yake hawajue kabisa mambo ya dini. Lakini, mara nyingi ni mambo wanaona katika dini ndiyo yanafanya waache kuamini Mungu. Wanaweza kuwaza kama dini kubwa zimeshindwa kujibia maulizo magumu juu ya maisha. Ni maulizo ya namna gani? Jambo la kushangaza ni kwamba, mara nyingi ni maulizo yaleyale yenye kuhangaisha watu wenye kusema kama wanaamini Mungu. Ona maulizo tatu watu wengi wangependa kuuliza Mungu ikiwa wangepewa nafasi ya kufanya hivyo, na uone majibu ya Biblia.

1 “SABABU GANI UNAACHA WATU WATESEKE?”

Sababu gani kuuliza ulizo hilo?

Watu wengi wanasema, ‘Mungu mwenye upendo angezuia taabu zenye kutokea katika maisha.’

JAMBO LA KUFIKIRIA: Tunaweza kuona tabia na desturi za watu wa mahali pengine kuwa zenye kushangaza, ao hata kuwa zenye kuchukiza. Kwa vyepesi tunaweza kuelewa mubaya matendo yao. Kwa mufano, katika desturi fulani, watu wanaona kuwa kuangalia mutu kwenye macho wakati munazungumuza ni alama ya kuonyesha kama mambo unasema ni ya kweli; lakini katika desturi ingine ni alama ya kukosa heshima. Hata katika hali hizo, hakuna sababu ya kusema kuwa desturi hizo ni mbaya. Lakini, tunapaswa tu kuzijua muzuri.

Inaweza kuwa pia hivyo juu ya kumujua Mungu? Watu wengi wanaamini kuwa mateso yanaonyesha kama hakuna Mungu. Lakini watu wengine wenye wameelewa sababu gani Mungu anaacha watu wateseke, wako hakika kama Mungu iko.

MAMBO BIBLIA INASEMA: Mawazo ya Mungu na njia zake ni tofauti na zetu. (Isaya 55:8, 9) Ndio maana matendo yake na sababu zenye kufanya angoje mbele ya kutenda, zinaweza kwanza kutushangaza.

Hata hivyo, Biblia haituombe tukubali maneno yasiyokuwa na maana, maneno kama vile “Mungu anatenda katika njia zenye hazieleweke.” Lakini, inatutia moyo tujifunze mambo mengi zaidi juu ya Mungu, na inatusaidia kuelewa sababu gani na wakati gani anatenda kwa njia fulani.a Tunaweza hata kumukaribia.—Yakobo 4:8.

2 “SABABU GANI DINI INAJAA UNAFIKI?”

Sababu gani kuuliza ulizo hilo?

Watu fulani wanaweza kuwaza, ‘Ikiwa Mungu anapenda uaminifu, hakungekuwa unafiki (udanganyifu) mwingi kati ya watu wenye kusema kuwa wanamuabudu.’

JAMBO LA KUFIKIRIA: Wazia mutoto mwenye anakataa mafundisho yenye baba yake alimupatia tangu utoto wake na anatoka nyumbani ili aishi maisha mabaya. Hata kama baba yake hafurahie jambo hilo, anaacha mutoto wake akamate uamuzi huo. Wale wenye watamuona mutoto huyo wako na haki ya kusema kama alikuwa na baba mubaya, ao hata kusema kama hakukuwa na baba? Hapana kabisa! Vilevile, unafiki wenye kuwa katika dini unahakikisha tu kuwa Mungu anaacha watu wajiamulie njia yenye watafuata katika maisha.

MAMBO BIBLIA INASEMA: Mungu anachukia unafiki wa dini. (Yeremia 7:29-31; 32:35) Wakati huo huo, anaacha watu watumie uhuru wao wa kuchagua. Watu wengi wenye kusema kuwa wanaamini Mungu, wanachagua kufuata mafundisho ya dini yenye wanadamu wamejitungia na kanuni za mwenendo zenye wamejiwekea wenyewe.—Mathayo 15:7-9.

Lakini, dini yenye Mungu anakubali haina unafiki.b Yesu alisema hivi: ‘Kwa jambo hili wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu, mukiwa na upendo kati yenu wenyewe.’ (Yohana 13:​35) Upendo huo unapaswa kuwa “bila unafiki.” (Waroma 12:⁠9) Dini nyingi zimeshindwa kuonyesha upendo huo. Kwa mufano, katika inchi ya Rwanda, wakati wa mauaji makubwa ya 1994, watu wengi wa dini waliua watu wa dini yao wenyewe, kwa sababu tu hawakukuwa wa kabila lao. Lakini, Mashahidi wa Yehova hawakujiingiza katika mauaji hayo, na wengi wao walificha waamini wenzao na watu wengine, na hata walitia maisha yao katika hatari ili kufanya hivyo. Matendo kama hayo ya kujitoa kwa ajili ya wengine yanaonyesha kama dini inaweza kuwa bila unafiki.

3 “SABABU GANI TUKO HAPA DUNIANI?”

Sababu gani kuuliza ulizo hilo?

Watu fulani wanaweza kujiuliza, ‘Sababu gani wanadamu wanaishi tu miaka 80 ao 90 na kisha wanakufa? Kusudi la maisha mafupi kama hayo ni gani?’

Mwanaume mumoja anasoma Biblia

JAMBO LA KUFIKIRIA: Hata watu wengi wenye hawaamini Mungu wanatambua kama kuko sababu yenye kufanya vitu vyenye kuwa katika ulimwengu vikuwe vigumu kueleweka, vya kushangaza, na vyenye mupangilio muzuri. Wanatambua kama sayari (planète) yetu, sayari zingine, na mwezi zimefanywa kwa njia ya muzuri ili kutegemeza uzima duniani. Wanasema kama sheria za asili zenye kuongoza ulimwengu zimewekwa na kupangwa kwa njia ya muzuri sana; hata mabadiliko madogo tu yanaweza kufanya kusikuwe tena uzima katika dunia.

MAMBO BIBLIA INASEMA: Hata kama watu wengi wanawaza kuwa hakuna Mungu kwa sababu ya maisha yetu mafupi, vitu vyenye kuwa katika ulimwengu vinahakikisha kabisa kama kuko Muumbaji. (Waroma 1:20) Alikuwa na kusudi la kufanya vitu hivyo, na sababu yenye kufanya tukuwe hapa duniani inapatana sana na kusudi lake. Mungu aliumba wanadamu ili waishi milele katika dunia, na kusudi lake halijabadilika.—Zaburi 37:11, 29; Isaya 55:11.

Tunaweza kutambua kama Mungu iko, na hata kuona sifa zake fulani kupitia vitu vyenye kuwa katika ulimwengu, lakini Mungu hakupanga tujue kusudi lake kupitia njia hiyo. Ili tujue kusudi la Mungu na sababu gani tuko hapa duniani, inaomba azungumuze na sisi. Katika Biblia, anazungumuza na sisi kwa kutumia maneno mepesi na ya moja kwa moja.c Mashahidi wa Yehova wanakuomba uchunguze majibu yenye kuwa katika Biblia.

a Ili kujua sababu yenye kufanya Mungu aache watu wateseke, soma sura ya 11 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? chenye kilichapishwa na Mashahidi wa Yehova. Unaweza pia kupata kitabu hicho kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org/swc.

b Ili kupata habari zingine, soma sura ya 15 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? chenye kilichapishwa na Mashahidi wa Yehova. Kitabu hicho kinapatikana pia kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org/swc

c Ili kupata habari zingine, soma sura ya3 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? chenye kilichapishwa na Mashahidi wa Yehova. Kitabu hicho kinapatikana pia kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org/swc..

ALIPATA MAJIBU YA MAULIZO YAKE

Harry anavaa nguo za kiaskari wakati alikuwa kijana

Wakati Harry alikuwa mutoto, hakuelewa sababu gani Mungu mwenye upendo anaacha watu wateseke. Wakati alikuwa kijana, alijionea mambo yenye kuchukiza ya vita na akauliza hivi: “Kama kuko Muumbaji mweza yote, sababu gani anaweza kuacha hali hizo zitese watu wengi, zaidi sana watoto wenye hawana kosa?”

Hata kama Harry alisoma masomo ya juu na alichunguza dini mbalimbali, hakupata jibu. Kisha kuhangaishwa na ulizo hilo kwa miaka mingi, aliamua kama “pengine hakuna Mungu kabisa.”

Harry

Harry

Harry alikuwa tayari kujifunza mambo mapya wakati alisikia mambo Biblia inasema juu ya ulizo lake. Alijifunza kama haiko Mungu ndiye analeta mambo mabaya; lakini, Mungu anachukia mambo mabaya na anaumia moyoni wakati anaona watu wanateseka. (Methali 6:16-19; Isaya 63:9; Yakobo 1:13) Harry alielewa kama maumivu na mateso yote yalianza kwa sababu wanadamu walikataa mamlaka ya Mungu, na walitumia uhuru wao wa kuchagua ili kujiamulia wenyewe mema na mabaya. (Kumbukumbu la Torati 32:4, 5; Yakobo 1:14, 15) Tena, alielewa kama Mungu hakuwaachilia na kusema, ‘Si niliwaambia.’ Lakini, mara moja Mungu alifanya mipango ili kumaliza mambo mabaya na mateso. Mungu ataondoa kabisa matokeo yote mabaya yenye yamepata watu kwa sababu ya kukataa mamlaka yake. Harry alifikia kutambua kama mbele wakati huo ufike, Mungu ametoa kitulizo na musaada ili watu wavumilie.—Mwanzo 3:15; Waroma 8:20, 21; Ufunuo 21:4.

Majibu hayo yalitimiza hamu ya Harry ya kutaka kujua mengi juu ya ulizo la maana. Tena, yalimusaidia avumilie wakati alivurugika moyoni kwa sababu ya taabu zenye zilimufikia yeye mwenyewe.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine