Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • yc somo 4 uku. 10-11
  • Binti Aliyemufurahisha Baba Yake na Pia Yehova

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Binti Aliyemufurahisha Baba Yake na Pia Yehova
  • Uwafundishe Watoto Wako
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Alipendwa na Mungu na Rafiki Zake Pia
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Tunakubaliwa na Mungu Ikiwa Tunabakia Waaminifu Kwake
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Ahadi ya Yefta
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Yefta Alikuwa Mutu wa Kiroho
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2021
Ona Habari Zaidi
Uwafundishe Watoto Wako
yc somo 4 uku. 10-11
Yefta anapitisha wakati pamoja na binti wake wakati iko mudogo

SOMO LA 4

Binti Aliyemufurahisha Baba Yake na Pia Yehova

Yefta anasali kwa Yehova wakati jeshi la Israeli liko linapigana vita na maadui wao

Yefta anamupatia Yehova ahadi gani?

Kisha kutoka kupigana vita, Yefta anamukumbatia binti wake mwenye anakuja kumupokea

Hata kama haikukuwa mwepesi, binti wa Yefta alitimiza ahadi yenye baba yake alimupatia Yehova

Unamuona binti huyu ku picha hii?— Ni mutoto wa bwana moja anayeitwa Yefta. Biblia haitaje jina lake, lakini tunajua kama alimufurahisha baba yake na pia Yehova. Ni vizuri tuzungumuze sasa juu ya binti huyu na baba yake.

Yefta alikuwa mutu muzuri. Alikuwa anapitisha wakati mwingi na mutoto wake ili kumufundisha habari za Yehova. Yefta alikuwa pia mutu mwenye nguvu na kiongozi muzuri. Siku fulani, Waisraeli walimuomba awapeleke kupigana vita na maadui wao.

Yefta alimuomba Mungu amusaidie ili ashinde vita hiyo. Yefta alimuambia Yehova hivi: ‘Nikishinda vita hiyo, wakati nitarudi, mutu wa kwanza mwenye atatokea mu nyumba yangu ili kunipokea, nitakupatia mutu huyo.’ Ni kusema, mutu huyo anapashwa kuishi na kumutumikia Mungu maisha yake yote ku hema ya ibada. Wakati huo, watu walikuwa wanakutana ku hema ya ibada ili kumuabudu Mungu. Habari ya kufurahisha ni hii: Yefta alishinda vita hiyo! Wakati anarudi, unajua ni nani mutu wa kwanza mwenye anatokea mu nyumba yake ili kumupokea?—

Ni ule binti wake! Yefta alikuwa na mutoto huyo mumoja tu, lakini sasa inamuomba amutume aende kuishi mbali ku hema ya ibada. Yefta anahuzunika sana. Lakini kumbuka, Yefta alikuwa amekwisha kumupatia Yehova ahadi. Bila kusita, binti wake anamuambia hivi: ‘Papa ulimupatia Yehova ahadi, kwa hiyo unapashwa kutimiza ahadi yako.’

Binti wa Yefta iko anatafuta kuni kwa ajili ya hema ya ibada; marafiki wake wanakuja kumutembelea

Kila mwaka, marafiki wa binti wa Yefta walikuja kumutembelea

Binti wa Yefta, alihuzunika pia. Juu kule ku hema ya ibada, hangeolewa wala kuzaa watoto. Hata hivyo, binti huyo alipenda sana kutimiza ile ahadi ya baba yake na pia alipenda kumufurahisha Yehova. Aliona kama kufanya vile ndio jambo la maana sana kuliko kuolewa na kuzaa watoto. Kwa hiyo, aliacha nyumba yao na kuenda kuishi maisha yake yote ku hema ya ibada.

Unawaza tendo hilo lilimufurahisha baba yake na vilevile Yehova?— Tendo hilo liliwafurahisha! Ukimutii Yehova na kumupenda kama vile binti wa Yefta alifanya, weye pia unaweza kufurahisha sana wazazi wako na vilevile Yehova.

SOMA KATIKA BIBLIA YAKO

  • Kumbukumbu la Torati 6:4-6

  • Waamuzi 11:30-40

  • 1 Wakorintho 7:37, 38

MAULIZO:

  • Yefta alikuwa nani? Alimupatia Yehova ahadi gani?

  • Ni juu ya nini haikuwa mwepesi kwa binti wa Yefta kutimiza ahadi yenye baba yake alimupatia Yehova?

  • Binti wa Yefta alipenda kufanya tendo gani la maana sana kuliko mambo mengine?

  • Namna gani unaweza kufuata mufano wa binti wa Yefta?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine