Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 36 uku. 88-uku. 89 fu. 1
  • Ahadi ya Yefta

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ahadi ya Yefta
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Binti Aliyemufurahisha Baba Yake na Pia Yehova
    Uwafundishe Watoto Wako
  • Alipendwa na Mungu na Rafiki Zake Pia
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Tunakubaliwa na Mungu Ikiwa Tunabakia Waaminifu Kwake
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Yefta Alikuwa Mutu wa Kiroho
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2021
Ona Habari Zaidi
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 36 uku. 88-uku. 89 fu. 1
Yefta anapasua nguo zake wakati binti yake anakuja kumupokea

36

Ahadi ya Yefta

Waisraeli walimuacha tena Yehova na kuanza kuabudu miungu ya uongo. Lakini, ile miungu haikuwasaidia hata kidogo wakati Waamoni walipigana nao. Waisraeli waliteseka kwa miaka mingi. Ku mwisho, wakamuambia Yehova: ‘Tumefanya zambi. Tafazali utuokoe katika mikono ya maadui wetu.’ Kisha, wakavunja-vunja sanamu zao na wakaanza tena kumuabudu Yehova. Yehova hakupenda waendelee kuteseka.

Mupiganaji-vita mwenye kuitwa Yefta alichaguliwa juu aongoze Waisraeli. Aliambia Yehova hivi: ‘Ukitusaidia kushinda hii vita, ninakutolea ahadi kama, wakati nitarudia ku nyumba, nitakupatia mutu wa kwanza mwenye atatoka mu nyumba yangu ili kunipokea.’ Yehova alisikiliza sala ya Yefta na akamusaidia apate ushindi.

Wakati Yefta alirudia kwake, mutoto wake mwanamuke, mutoto mumoja tu mwenye alikuwa naye, njo alikuwa mutu wa kwanza mwenye alikuja kumupokea. Alikuwa anacheza dansi na kupiga ngoma. Yefta angefanya nini? Alikumbuka ahadi yake na akasema: ‘Aah, mutoto wangu! Umenivunja moyo. Nilitoa ahadi kwa Yehova. Juu niitimize, ninapaswa kukutuma mu muji wa Shilo ili utumikie ku tabenakulo.’ Binti yake akamuambia: ‘Baba, kama umetoa ahadi kwa Yehova, unapaswa kuitimiza. Ninaomba tu uniache niende ku milima na marafiki wangu wanamuke kwa miezi mbili. Kisha, nitaenda Shilo.’ Binti ya Yefta alitumikia kwa uaminifu ku tabenakulo maisha yake yote. Kila mwaka marafiki wake walikuwa wanaenda kumuona.

Marafiki wa binti ya Yefta wanaenda kumuona ku tabenakulo

“Mutu mwenye anamupenda baba ao mama kuliko mimi hanistahili.”​—Matayo 10:37

Maulizo: Yefta alitoa ahadi gani? Binti ya Yefta alifanya nini kisha kujua ahadi yenye Baba yake alitoa?

Waamuzi 10:6–11:11; 11:29-40; 1 Samweli 12:10, 11

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine