Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • yc somo 8 uku. 18-19
  • Yosia Alikuwa na Marafiki Wazuri

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yosia Alikuwa na Marafiki Wazuri
  • Uwafundishe Watoto Wako
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Yosia Alipenda Sheria ya Mungu
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Vijana, Mutakuwa na Maisha ya Namna Gani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
Uwafundishe Watoto Wako
yc somo 8 uku. 18-19
Mufalme Yosia iko anamusikiliza Yeremia, rafiki yake

SOMO LA 8

Yosia Alikuwa na Marafiki Wazuri

Unawaza ni mwepesi kufanya mambo mazuri?— Watu wengi wanawaza kama haiko mwepesi kufanya mambo mazuri. Katika Biblia muko hadisi ya kijana moja anayeitwa Yosia. Haikuwa mwepesi kwake kufanya mambo mazuri. Lakini Yosia alikuwa na marafiki wazuri wenye walimusaidia kufanya mambo mazuri. Ni vizuri tuzungumuze sasa juu ya Yosia na marafiki wake.

Baba ya Yosia anaitwa Amoni. Amoni alikuwa mufalme wa Yuda. Alikuwa anafanya mambo mabaya sana na alikuwa anaabudu masanamu. Wakati baba ya Yosia alikufa, Yosia akakuwa mufalme wa Yuda. Lakini alikuwa tu na miaka munane wakati alianza kutawala! Unawaza Yosia alikuwa mufalme mubaya kama baba yake?— Yosia alikuwa mufalme muzuri!

Nabii Sefania anaambia watu wa Yuda ujumbe wa Yehova

Sefania anawaambia watu waache kuabudu masanamu

Yosia alipenda kumutii Yehova hata wakati alikuwa kijana mudogo sana. Kwa hiyo, alichagua kufanya urafiki tu na watu wenye kumupenda Yehova. Na wale marafiki walimusaidia Yosia kufanya mambo mazuri. Unajua marafiki fulani wa Yosia?

Sefania alikuwa rafiki wa Yosia. Sefania ni nabii mwenye aliwaambia watu wa Yuda hivi: ‘Ikiwa munaendelea kuabudu masanamu, mambo mabaya yatawapata.’ Yosia alisikiliza maneno ya Sefania. Alimuabudu Yehova, wala hakuabudu masanamu.

Yeremia alikuwa pia rafiki wa Yosia. Yosia na Yeremia walikuwa karibu na miaka moja ya kuzaliwa. Na walikomalia fasi moja. Wakati Yosia alikufa, Yeremia aliandika wimbo wa pekee ili kuonyesha huzuni yake juu ya kifo cha Yosia. Ile inaonyesha kama walikuwa marafiki waliopendana. Yeremia na Yosia walisaidiana ili kumutii Yehova na kufanya mambo mazuri.

Yosia na Yeremia wanasaidiana ili kufanya mambo mazuri

Mufano wa Yosia unakufundisha nini?— Hata wakati Yosia alikuwa kijana mudogo sana, alipenda kufanya mambo mazuri. Alijua kama ni vizuri sana kuwa na marafiki wenye kumupenda Yehova. Wakati unachagua marafiki, fanya angalisho. Chagua marafiki wenye kumupenda Yehova. Marafiki wenye kumupenda Yehova watakusaidia kufanya mambo mazuri!

SOMA KATIKA BIBLIA YAKO

  • 2 Mambo ya Nyakati 33:21-25; 34:1, 2; 35:25

MAULIZO:

  • Baba ya Yosia anaitwa nani? Alikuwa anafanya mambo mazuri?

  • Yosia alipenda kufanya nini hata wakati alikuwa kijana mudogo sana?

  • Unaweza kutaja majina ya marafiki wawili wa Yosia?

  • Mufano wa Yosia unakufundisha nini?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine