SURA YA 10
Namna ya Kupanua Utumishi Wako
WAKATI Yesu alituma wanafunzi wake waende kuhubiri habari njema ya Ufalme, aliwaambia hivi: “Ndiyo, mavuno ni mengi, lakini wafanyakazi wako kidogo.” Juu kulikuwa kazi mingi ya kufanya, Yesu aliongezea hivi: “Mumuombe Bwana wa mavuno atume wafanyakazi katika mavuno yake.” (Mt. 9:37, 38) Yesu aliambia wanafunzi wake namna wangefanya ile kazi. Hii maneno inaonyesha kama alipenda ifanyike kwa uharaka sana: “Hamutamaliza kuzunguka miji ya Israeli mupaka Mwana wa binadamu afike.”—Mt. 10:23.
2 Leo pia, kuko mingi ya kufanya mu kazi ya kuhubiri. Kunabakia wakati kidogo sana, lakini tunajua kama habari njema ya Ufalme inapaswa kuhubiriwa mbele mwisho ifike! (Mk. 13:10) Juu shamba ni dunia yote, hali yetu inafanana sana na ile yenye Yesu na wanafunzi wake walikutana nayo. Lakini siye tuko na eneo kubwa kuliko yenye walikuwa nayo. Hata kama wahubiri ni wadogo sana kwa kulinganisha na mamiliare ya watu mu dunia yote, tunapaswa kuwa hakika kama Yehova atatusaidia. Habari njema ya Ufalme itahubiriwa mu dunia yote, na ile mwisho itafika kulingana na siku yenye Yehova alishakaweka. Je, tutatia Ufalme wa Mungu pa fasi ya kwanza juu tuweze kutimiza kwa ukamili utumishi wetu? Ni miradi gani ya kiroho yenye tunaweza kujiwekea juu tuweze kutimiza ile kazi?
3 Yesu alionyesha kile Yehova anaomba wale wote wenye wamejitoa kwake, wakati alisema hivi: “Unapaswa kumupenda Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote na kwa nguvu zako zote.” (Mk. 12:30) Tunapaswa kufanya kazi ya Mungu kwa nafsi yetu yote, ni kusema, kuonyesha kama tumejitoa kabisa kwake kwa kufanya yote yenye tunaweza mu kazi yake. (2 Ti. 2:15) Kuko njia mingi zenye zinaweza kutusaidia kufanya vile, zenye kila mutu anaweza kutumia kupatana na hali na uwezo wake. Uchunguze njia mbalimbali zenye kuwa hapa chini, na kisha uamue ni muradi gani unaweza kujiwekea juu ya kupanua utumishi wako.
KUWA MUHUBIRI MU KUTANIKO
4 Wale wote wenye kukubali kweli wako na pendeleo ya
kutangaza habari njema. Hii njo kazi ya maana sana yenye Yesu alipatiaka wanafunzi wake. (Mt. 24:14; 28:19, 20) Kwa kawaida, mwanafunzi wa Yesu Kristo anaanza kuelezea wengine habari njema kisha tu kuisikia. Kwa mufano, ni vile Andrea, Filipo, Kornelio, na wengine walifanya. (Yoh. 1:40, 41, 43-45; Mdo. 10:1, 2, 24; 16:14, 15, 25-34) Ile inamaanisha kama mutu anaweza kuelezea wengine habari njema hata kama hayabatizwa? Ndiyo, wakati tu mutu anakubaliwa mu kutaniko kuwa muhubiri mwenye hayabatizwa, anapewa nafasi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba. Pia, kulingana na uwezo na hali yake, anaweza kutumika mu aina zingine za mahubiri.
5 Kusema kweli, kisha tu muhubiri kubatizwa, anapendaka kufanya yake yote ili kusaidia wengine wajue habari njema. Wanaume na wanamuke wenye kubatizwa wako na pendeleo ya kuhubiri habari njema. Ni pendeleo kabisa kusaidia ili faida za Ufalme wa Mungu ziendelee, hata kama hatuna uwezo wa kufanya mingi. Kusema kweli, kila mutu mwenye anapanua utumishi wake na kufikia mapendeleo zaidi, atakuwa na furaha sana.
KUTUMIKIA FASI KWENYE KUKO LAZIMA KUBWA
6 Pengine eneo ya kutaniko yenu inahubiriwa sana, na ushahidi muzuri unaendelea kutolewa mule. Kama ni vile, unaweza kuona kama ni muzuri kupanua utumishi wako kwa kuenda kutumikia fasi kwenye kuko lazima kubwa. (Mdo. 16:9) Kama uko muzee ao mutumishi wa huduma, kunaweza kuwa kutaniko yenye itafurahi kama unaenda kuisaidia. Mwangalizi wenu wa muzunguko anaweza kukupatia mashauri yenye inaweza kukusaidia ili utumikie mu kutaniko ingine mu muzunguko yenu. Kama unapenda kuenda saidia mu eneo ingine ya inchi yako, biro ya tawi inaweza kukupatia habari zenye kufaa.
7 Unapendaka kutumikia mu inchi ingine? Kama ni vile, unapaswa kufikiria sana ile jambo mbele ya kuhamia kule. Unaweza kuizungumuzia na wazee wa kutaniko yako. Kuhamia mu inchi ingine kutaleta mabadiliko mu maisha yako na mu maisha ya mutu mwenye mutaenda naye. (Lu. 14:28) Lakini, kama haupange kukawia mu ile inchi, inaweza kuwa muzuri kufikiria tu eneo fulani mu inchi yako kwenye unaweza kutumikia.
8 Mu mainchi fulani, ndugu wenye kufanya kazi ya uangalizi mu makutaniko ni ndugu wenye hawayakawia sana mu kweli. Kwa hiyo, unyenyekevu unawasukuma kuacha wazee wenye uzoefu mingi, wenye wanahamia mu kutaniko yao waongoze mambo. Kama uko muzee na uko napanga kuhamia mu inchi ya vile, ukumbuke kama hauende kule juu ya kukamata fasi ya ndugu wa mu kutaniko, lakini kusudi yako ni kutumika pamoya nao. Uwatie moyo wajikaze kufikia mapendeleo na wakubali migawo mbalimbali mu kutaniko. (1 Ti. 3:1) Ukiona kama mambo fulani inafanyika tofauti na vile mambo inafanywa mu kutaniko ya inchi yako, ukuwe muvumilivu. Uko muzee, kwa hiyo, ni muzuri kutumia uzoefu wako ili kusaidia kabisa wale wazee. Kisha, kama kunakuwa sababu fulani yenye inakulazimisha kurudia mu inchi yako, wazee wa ile kutaniko watakuwa tayari na uzoefu wa kutosha ili kuhangaikia muzuri kutaniko.
9 Mbele biro ya tawi ikuambie makutaniko yenye kuwa na lazima ya musaada, Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko yako itaandikia ile biro ya tawi barua ya kukupendekeza. Ile barua itaonyesha kama uko muzee, mutumishi wa huduma, painia ao muhubiri mwenye kubatizwa mu kutaniko yako. Halmashauri ya Utumishi itatuma barua ya kukupendekeza na ombi yako moja kwa moja ku biro ya tawi ya inchi kwenye unapenda kuenda tumikia.
KUHUBIRI MU LUGA INGINE
10 Njia ingine ya kupanua utumishi wako ni kujifunza luga ingine, kutia ndani luga ya ishara. Kama unapanga kuhubiri mu luga ingine, unaweza kuzungumuza na wazee wa kutaniko yako na pia mwangalizi wa muzunguko. Wanaweza kukutia moyo na kukupatia mapendekezo ya lazima. Biro ya tawi imeruhusu mizunguko fulani ifanye masomo ya kujifunza luga za mupya ili kuzoeza wahubiri na mapainia wenye kustahili kuhubiri mu luga ingine.
KAZI YA UPAINIA
11 Wahubiri wote wanapaswa kujua muzuri mambo yenye kuombwa ili kuwa painia musaidizi, painia wa kawaida, na painia wa pekee ao ili kufanya aina ingine ya utumishi wa wakati wote. Painia anapaswa kuwa Mukristo mwenye kubatizwa mwenye iko na mwenendo muzuri, na mwenye hali yake inamuruhusu kueneza kila mwezi saa zenye anaombwa kupitisha mu kazi ya kuhubiri. Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko njo inachunguzaka ombi ya kuwa painia musaidizi na painia wa kawaida. Lakini, biro ya tawi njo inawekaka mapainia wa pekee.
12 Muhubiri anaweza kuwa painia musaidizi mu mwezi moya ao mu miezi fulani yenye kufuatana. Lakini kama hali yake inamuruhusu, anaweza amua kuwa painia musaidizi wa kuendelea. Wahubiri wengi wa Ufalme wanapendaka kuwa mapainia wasaidizi wakati wa matukio ya pekee, sawa vile wakati ya Ukumbusho ao mu mwezi yenye mwangalizi wa muzunguko anatembelea kutaniko. Wengine wanaamua kuwa mapainia wasaidizi wakati wa mapumuziko. Wahubiri wenye kubatizwa, wenye ni wanafunzi, wanaweza kufurahia kuwa mapainia wasaidizi wakati wa mapumuziko. Wahubiri wanaweza chagua kuwa mapainia wasaidizi mu Mwezi ya 3 na ya 4, na mu mwezi yenye mwangalizi wa muzunguko anatembelea kutaniko, juu mu ile miezi, saa za kuwa painia musaidizi zinapunguzwaka. Ikuwe uko mu hali gani, kama uko na mwenendo na tabia ya muzuri, kama unaweza kufanya programu ili kueneza saa zenye kuombwa, na ikiwa uko hakika kama unaweza kuwa painia musaidizi mu mwezi moya ao zaidi, wazee wa kutaniko watafurahia kuchunguza ombi yako ya kupenda kushiriki mu hii pendeleo ya utumishi.
13 Juu muhubiri akuwe painia wa kawaida, anapaswa kuwa na uwezo ya kueneza saa zenye mapainia wa kawaida wanaombwa kueneza kila mwaka. Painia wa kawaida, anapaswa kushirikiana sana na kutaniko yake. Mapainia wenye bidii ni baraka mu kutaniko. Wanachochea wahubiri wengine wafurahie kazi ya kuhubiri na hata wanawatia moyo wakuwe pia mapainia. Lakini, juu muhubiri astahili kuwa painia wa kawaida, anapaswa kuwa mufano muzuri kwa wengine, na lazima miezi sita ao zaidi ikuwe imepita tangu abatizwe.
14 Kwa kawaida, mapainia wa pekee wanachaguliwa kati ya mapainia wa kawaida wenye kupata matokeo ya muzuri mu kazi ya kuhubiri. Mapainia wa pekee wanapaswa kuwa na uwezo ya kutumikia kila fasi kwenye biro ya tawi inaamua kuwatuma. Mara mingi, wanatumwa mu maeneo ya mbali kwenye wanaweza kupata watu wenye kupendezwa na kuanzisha makutaniko. Wakati fulani, mapainia wa pekee wanatumwa mu makutaniko yenye iko na lazima ya musaada ili kuhubiri eneo yao yote. Mapainia fulani wa pekee wenye kuwa wazee wanatumwa pia mu makutaniko ya kidogo-kidogo, hata kama ile makutaniko haina lazima ya musaada ya pekee ya wahubiri wengi. Mapainia wa pekee wanapewa makuta kidogo ya kuwasaidia kulipia garama fulani. Mapainia fulani wanawekwa kuwa mapainia wa pekee wa muda.
KAZI YA UMISIONERE
15 Wamisionere wanawekwa na Halmashauri ya Utumishi ya Baraza Yenye Kuongoza. Kisha wao kuwekwa, Halmashauri ya Tawi ya inchi mwenye wanatumwa njo itawatuma mu maeneo yenye iko na watu wengi. Wale wamisionere wanasaidia sana makutaniko ikuwe nguvu kiroho, iendelee kuhubiri, na wanasaidia pia ili kazi zingine za kutaniko ziendeshwe muzuri. Mara mingi wamisionere wanapata mazoezi ku Masomo ya Waeneza-Injili wa Ufalme. Wanapewa fasi ya kuikala na makuta kidogo ya kuwasaidia kulipia garama fulani.
KAZI YA MWANGALIZI WA MUZUNGUKO
16 Wanaume wenye Baraza Yenye Kuongoza inaweka kuwa wangalizi wa muzunguko, wanapata kwanza mazoezi na uzoefu kwa kutumika na wako waangalizi wa muzunguko wa badala. Ni wanaume wenye wanapenda kazi ya kuhubiri na wanapenda ndugu zao. Ni mapainia wenye kuhubiri kwa bidii, wanajifunza sana Biblia, wanasema na kufundisha muzuri mu kutaniko. Wanaonyesha kwa kiasi kikubwa sifa za tunda ya roho, ni wenye kiasi, wanakubali mawazo ya wengine na ni wenye utambuzi. Kama mwangalizi iko na bibi, bibi yake anapaswa kuwa painia mwenye iko na mwenendo muzuri na mwenye anatendeaka wengine muzuri. Ni muhubiri mwenye anapata matokeo ya muzuri mu kazi ya kuhubiri. Juu yeye ni mwanamuke Mukristo, anaelewa muzuri daraka yake ya kujitiisha. Haseme mubaya juu ya bwana yake, hatawale mazungumuzo ao kusema mingi. Juu wangalizi wa muzunguko na bibi zao wako na programu yenye iko na mambo mingi, wale wenye wanapenda kufanya hii kazi wanapaswa kuwa na afya ya muzuri. Mapainia hawafanyake ombi ya kuwa wangalizi wa muzunguko. Lakini, wanaweza kuelezea mwangalizi wa muzunguko tamaa yao, naye atawapatia mapendekezo fulani yenye wanaweza kuwa nayo lazima.
MASOMO MBALIMBALI YA KITEOKRASI
17 Masomo ya Waeneza-Injili wa Ufalme: Waeneza-Injili wa Ufalme wanahitajiwa ili kutia nguvu makutaniko na kuhubiri mu maeneo yenye haihubiriwe kwa ukawaida. Kwa hiyo, ndugu wenye hawayaoa, dada wenye hawayaolewa, na ndugu na dada wenye wameoana wanaweza kupata mazoezi ya pekee ku Masomo ya Waeneza-Injili wa Ufalme. Kisha kusoma ile masomo, wanatumwa na wako mapainia wa kawaida mu maeneo yenye iko na lazima kubwa mu inchi yao. Lakini, wale wenye hali zao zinawaruhusu, wanaweza kupewa migawo ingine mu inchi yao ao mu inchi ingine. Wadogo kati yao wanaweza kutumwa kuwa mapainia wa pekee wa muda ao wa wakati wote. Mapainia wenye wanapenda kusoma hii masomo wanaweza kujua mambo yenye kuombwa kwa kuhuzuria mukutano wenye unahusu hii masomo wenye unafanywaka ku mukusanyiko wa eneo.
18 Masomo ya Biblia ya Gileadi: Ndugu wenye hawayaoa, dada wenye hawayaolewa, ndugu na dada wenye wameoana wenye wanachaguliwa ili kusoma hii masomo, wanazungumuza Kiingereza na wako mu utumishi wa pekee wa wakati wote. Wako na sifa za kusaidia makutaniko ikuwe na bidii mu kazi ya kuhubiri na ikuwe nguvu kiroho, na wanasaidia pia ili kazi ziendeshwe muzuri mu Beteli. Maisha yao inaonyesha kama wanapenda kutumikia ndugu zao na kama wanaweza kusaidia wengine kufuata mashauri ya Maandiko na muongozo wa kiteokrasi. Halmashauri ya Tawi njo inachaguaka ndugu na dada wenye wanaweza kujaza fomu ya kusoma ile masomo. Wale wenye wamemaliza ile masomo, wanatumwa ili kuhubiri mu eneo ya tawi ao ili kutumikia ku biro ya tawi ya mu inchi yao ao ya mu inchi ingine.
KAZI YA BETELI
19 Ni pendeleo ya pekee kutumika ku Beteli. Jina Beteli inamaanisha “Nyumba ya Mungu,” na inastahili kuitwa vile juu ni Beteli njo inasimamia kazi ya kuhubiri mu kila inchi. Ndugu na dada wenye wanatumika ku Beteli wanafanya kazi ya maana sana ya kutayarisha, kutafsiri, na kugawanya vichapo vyenye vinatusaidia kujifunza Biblia. Baraza Yenye Kuongoza yenye inasimamia na kuongoza makutaniko mu dunia yote, inaona kazi yao kuwa ya maana sana. Wanabeteli wengi wenye ni watafsiri wanaishi na kutumikia mu eneo ya tawi kwenye luga yenye wanatafsiri inazungumuziwa. Ile inawasaidia wakuwe nasikia namna watu wanazungumuzaka ile luga kila siku. Wanaweza pia kujionea kama watu wako naelewa muzuri maneno yenye iko natumiwa mu vichapo vyenye wako natafsiri.
20 Kazi mingi zenye kufanywa ku Beteli, zinaomba kuwa na nguvu mingi ya kimwili. Njo maana, wale wenye wanaitwa ku Beteli ni ndugu na dada vijana wenye walijitoa kwa Mungu mu sala na kubatizwa, na tena wako na afya ya muzuri na nguvu. Kama tawi yenye inasimamia kazi mu inchi yenu iko na lazima ya wanabeteli na kama unapenda kutumika ku Beteli, unaweza kuzungumuza na wazee wa kutaniko yako juu ya kujua mambo yenye inaombwa.
KAZI YA UJENZI
21 Sawa vile kazi ya kujenga hekalu ya Sulemani, ujenzi wa majengo mbalimbali ya kiteokrasi ni utumishi mutakatifu. (1 Fa. 8:13-18) Ndugu na dada wengi wanaonyesha bidii ya ajabu kwa kutoa wakati na mali yao juu ya kusaidia mu hii kazi.
22 Hali yako inakuruhusu kusaidia mu kazi ya ujenzi? Kama uko muhubiri mwenye ashakabatizwa na unapendaka kusaidia mu kazi ya ujenzi, ndugu wenye kusimamia kazi ya ujenzi mu eneo yenu watafurahia musaada wako na wako tayari kukupatia mazoezi hata kama haujue muzuri kazi yenyewe. Kama unapenda kusaidia mu kazi ya ujenzi, unaweza kuzungumuza na wazee wa kutaniko yenu. Wahubiri fulani wenye kubatizwa, wenye wanatimiza mambo yenye inaombwa, wamejitoa ili kutumika mu ujenzi wa majengo mbalimbali ya kiteokrasi mu inchi zingine.
23 Kuko nafasi mingi za kusaidia mu kazi za ujenzi. Wahubiri wenye kubatizwa, wenye kuwa mufano muzuri na wenye kuwa na ufundi mu kazi fulani, wanaweza kusaidia mu kazi za ujenzi zenye kufanywa karibu na kwenye wanaishi. Wanaitwa wajitoleaji wa watumishi wa Idara ya Kupanga/Kujenga mu Eneo la Tawi (LDC). Wengine wanaweza kusaidia kwa wakati fulani mu kazi za ujenzi zenye kufanywa mbali na kwao; wale wanaitwa wajenzi wenye kujitolea kwa muda. Ni biro ya tawi njo inawaitaka juu wasaidie mu majuma mbili ao miezi tatu. Wenye wanawekwa ili kutumikia wakati murefu, wanaitwa watumishi wa ujenzi wa wakati wote. Mutumishi wa ujenzi wa wakati wote mwenye anapewa mugawo mu inchi ingine, anaitwa mutumishi wa ujenzi kutoka inchi ya kigeni. Kikundi ya Wajenzi inafanyizwa na watumishi wa ujenzi wa wakati wote na pia wajenzi wenye kujitolea kwa muda. Inasimamiaka kila kazi ya kujenga, na inasaidiwa na wajitoleaji wa watumishi wa Idara ya Kupanga/Kujenga mu Eneo la Tawi (LDC), na pia ndugu na dada wenye kujitolea wa mu makutaniko yenye iko inajengewa. Kisha kumaliza ujenzi mu eneo fulani ya tawi, Kikundi ya Wajenzi inaenda kuongoza kazi ya ujenzi mu eneo ingine ya ileile tawi.
UKO NA MIRADI GANI YA KIROHO?
24 Kama ushakajitoa kwa Yehova, ile inaonyesha kama unapenda kumutumikia milele. Lakini, ni miradi gani ya kiroho yenye umejiwekea mu maisha yako? Kujiwekea miradi ya kiroho kutakusaidia utumie muzuri nguvu na vitu vingine vyenye uko navyo. (1 Ko. 9:26) Kujiwekea miradi ya vile, kutakusaidia ukomale kiroho na kutakusaidia ukazie mambo ya maana zaidi kadiri uko najikaza ili kufikia mapendeleo ingine ya utumishi.—Flp. 1:10; 1 Ti. 4:15, 16.
25 Paulo ni mufano muzuri wa kuiga mu utumishi wetu kwa Mungu. (1 Ko. 11:1) Alijitoa sana mu kazi ya Yehova. Alielewa kama Yehova alimupatia nafasi mingi za kumutumikia. Paulo aliandikia ndugu wa Korinto hivi: “Nimefunguliwa mulango mukubwa wenye unaongoza kwenye utendaji.” Na siye, tunaweza kusema vile leo? Ndiyo, siye pia tuko na nafasi mbalimbali za kumutumikia Yehova pamoya na kutaniko, zaidi sana mu kazi ya kuhubiri habari njema ya Ufalme. Lakini sawa vile Paulo, juu tupite mu ile “mulango mukubwa” tunapaswa kupambana na “wapinzani wengi.” (1 Ko. 16:9) Paulo alikuwa tayari kujitia nizamu. Alisema hivi: “Ninapiga-piga mwili wangu na kuuongoza kama mutumwa.” (1 Ko. 9:24-27) Na weye, uko na roho ya vile?
Kujiwekea miradi ya kiroho kutakusaidia utumie muzuri nguvu na vitu vingine vyenye uko navyo
26 Kila mutu anatiwa moyo kujiwekea miradi ya kiroho kulingana na hali yake. Leo, ndugu na dada wengi wenye wanafanya utumishi fulani wa wakati wote, walijiwekea ile miradi tangu zamani mu maisha yao. Wengine, wakati walikuwa wangali watoto, wazazi wao na ndugu na dada njo waliwatia moyo kujiwekea ile miradi. Kwa hiyo, leo wamepata furaha mingi sana mu kazi ya Yehova, na hawasikitike juu ya nini walichagua kufanya vile. (Mez. 10:22) Miradi ingine ya maana yenye unaweza kujiwekea ni kuhubiri kwa bidii kila juma, kuanzisha na kuongoza mafunzo ya Biblia, ao kujiwekea wakati mingi ya kutayarisha mikutano. Jambo ya maana ni kuendelea kuwa waaminifu na kutimiza kwa ukamili kazi yetu ya kuhubiri. Kama tunafanya vile, tutamuletea Yehova sifa na tutafikia muradi wetu mukubwa zaidi, ni kusema, kumutumikia milele.—Lu. 13:24; 1 Ti. 4:7b, 8.