Tutafute Mapainia Wasaidizi 100,000
Je! Unaweza Kuwa Painia Msaidizi Mnamo Machi? Mnamo Aprili? Mnamo Mei?
1 “Tutafute wahubiri 1,000.” Hicho ndicho kilichokuwa kichwa cha makala iliyotangazwa katika Mnara wa Mlinzi mnamo Aprili 1881. Ilikuwa inawaalika wanaume na wanawake wote waliojitoa wakfu, “kwao ambao Bwana alitoa ujuzi wa ukweli wake,” kutumia kikamilifu wakati wao ili kutangaza ukweli wa Biblia. Wale waliokuwa na uwezekano wa kutoa yapata nusu ya wakati wao kwa kazi ya Bwana tu walitiwa moyo kujitoa kwa kujipendea kuwa waenvajelisti makolpota —watangulizi wa mapainia wa leo.
2 Ikiwa nyakati zilibadilika tangu miaka ya 1800, jambo moja linadumu: watumishi waliojitoa wakfu kwa Mungu wanazingatia moyoni kuendelea kutumia kikamilifu wakati wao ili kujulisha habari njema. Kwa kuwa mapainia wasaidizi, wahubiri wa kutaniko wanajikaza kutumia wakati zaidi katika huduma ya Ufalme, jambo ambalo linawasaidia kuwa wenye matokeo zaidi.—Kol. 4:17; 2 Tim. 4:5.
3 Tangu kuundwa kwa utumishi wa painia msaidizi, mamia ya maelfu ya akina ndugu na dada wanajipatia shangwe ndani ya utumishi huo. Sehemu hiyo ya utumishi wa painia iliamsha shauku inayoendelea kukua, kwa kiasi kwamba mnamo Aprili 1985 tulirekodi kilele cha mapainia wasaidizi 100,000 katika Shirikisho ya Amerika! Tangu hapo, ilifikia mara tatu kwamba zaidi ya wahubiri 100,000 kuwa mapainia wasaidizi muda wa mwezi wa Aprili: katika 1988, katika 1989 na katika 1992. Katika Burundi, Congo na Zaïre, hatukuweza kufikia wala kupita hesabu za mwaka wa utumishi 1995. Badala yake mwelekeo ni kushuka chini tukiwa na 100 katika Burundi, 359 katika Congo na 6,016 katika Zaïre muda wa mwaka wa utumishi 1996. Bila shaka kwamba inawezekana kufanya tena bidii hiyo nzuri muda wa miezi ya Machi, Aprili na Mei. Namna iliyo bora ya kuchochea roho ya upainia ni kwamba wazee watoe kielelezo, iwe kwa kuanzisha wenyewe utumishi huo au tu, kuongeza kushiriki kwao katika huduma muda wa kipindi hicho.
4 Tunawatia moyo kujiwekea mradi wa kuwa painia msaidizi muda wa mwezi mmoja au mingi ya miezi ya Machi, Aprili na Mei. Kwa nini Machi? Kwa kuwa mwaka huu Ukumbusho wa kifo cha Kristo unaanguka Siku ya Yenga Machi 23. Jambo bora la kufanya je! si ni kufaidika na majuma yanayotangulia tukio hilo ili kujitoa kwa juhudi katika kazi ya kuhubiri ya Ufalme ambayo Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo alianzisha? Kwa kushiriki kwa bidii katika ushuhuda mnamo Machi, tutaweza kualika watu wengi waliyotayari kujiunga nasi kwa mwadhimisho wa kifo cha Kristo. Kwa upande mwingine, mwezi huu una Siku za Posho tano na Siku za Yenga tano, jambo ambalo linawezesha kujitoa kwa bidii katika mahubiri mwisho wa juma. Bila shaka, ikiwa tunaendelea kuwa na utendaji wenye juhudi muda wa miezi ya Aprili na Mei, tutaweza kukomaza kupendezwa ambako tuliamsha na kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani kwa msaada wa broshua Mungu Anataka Nini Kwetu? Tunatembelea pia eneo letu kwa undani, hasa mwisho wa juma, kwa kutolea namba za mwisho-mwisho zinazofaa za Mnara wa Mlinzi na Amkeni!
5 Nani Anayeweza Kuwa Painia Msaidizi? Kitabu Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu kinakazia kwenye ukurasa 113: “Hata uwe una hali gani za kibinafsi, kama umebatizwa, una hali nzuri ya kiadili, unaweza kufanya mpango utimize takwa la kutumia kila mwezi saa 60 katika huduma ya shambani na unaamini ungeweza kutumika kuwa painia-msaidizi mwezi mmoja au zaidi, wazee wa kundi watafurahi kufikiria ombi lako la pendeleo hili la utumishi.” Je! ungeweza kuachia nafasi pendeleo hilo mnamo Machi? mnamo Aprili? mnamo Mei?
6 Ikiwa wazee wana mwelekeo wa akili unaotazamia mema na kwamba baki la wahubiri linategemeza mpango huo kwa moyo wote, mwito huu kwa ajili ya mapainia wasaidizi 100,000 utafanikiwa. (Ebr. 13:7) Baba wote wa familia wanatiwa moyo kufikiri kwa hesabu ya wale ambao, katika nyumba zao, wangeweza kuingia katika mstari wa mapainia wasaidizi muda wa moja ya miezi ijayo. —Zab. 148:12, 13; Mdo. 21:8, 9.
7 Usiwe mwepesi kusema kwamba hauna uwezo wa kufanya utumsihi wa painia msaidizi kwa sababu ya kazi yako ya kimwili ya wakati wote, matumizi yako ya wakati ya shule, madaraka yako ya kifamilia au mapaswa mengine ya kibiblia. Kwa wamoja, haitakuwa labda rahisi kuushiriki; hata hivyo, wanaweza kufikia kuufanya kwa kupanga mambo yao vizuri na kwa baraka ya Yehova. (Zab. 37:5; Mez. 16:3) Acha nia ya kushiriki katika utumishi wa painia iwe na uvutano juu ya nia yako ya kuwa painia. (Mez. 13:19a) Hivyo, wakiwa wenye kuchochewa na upendo mwingi kwa Yehova na kwa jirani, wengi wataweza kurekebisha matumizi yao ya wakati ya juma ili kupanua huduma yao muda wa mwezi moja. (Lk. 10:27, 28) Faida nyingi zinawangoja wale wanaofanya bidii kakamavu katika utumishi wa Ufalme.—1 Tim. 4:10.
8 Matokeo ya Utumishi wa Painia Msaidizi: Bidii inayofanywa na maelfu ya watumishi wa Mungu kwa nafsi yao yote kwa kuwa mapainia wasiaidizi inafanyiza wimbo mkubwa wa sifa kwa Yehova. Kwa kuwa wahubiri hao wanajitoa ili kujulisha habari njema kwa watu wengi, wanakuwa karibu zaidi na Yehova. Hakika, wanajifunza kumtegemea yeye zaidi ili kupata roho yake na kubarikiwa.
9 Kuwako kwa mapainia wasaidizi, wa kawaida na wa pekee wanaotumika karibu nasi kunatokeza msukumo mpya wa juhudi katika kutaniko. Kama wanavyoeleza mambo yao yaliyoonwa katika mahubiri, shauku yao ni yenye kuambukiza. Hilo linawatia wengine moyo kuchunguza upya mambo yao ya kwanza maishani, uwezekano wao mbalimbali wa kushiriki zaidi katika kazi ya muhimu zaidi ya huduma yetu. Dada mmoja ambaye alibatizwa akiwa na umri wa miaka 70 alianza baadaye tu kuwa painia msaidizi kwa namna ya ukawaida. Walimuuliza miaka fulani baadaye kwa nini, kwa umri wake, aliendelea kujitoa kwa bidii hivyo katika huduma kwa kuwa painia msaidizi kila mwezi. Alijibu hivyo kwamba alikuwa mwenye hisia moyoni kwamba aliharibu miaka yake ya kwanza kwanza 70 ya maisha yake na kwamba hangependa iwe vivyo hivyo tena kwa ile inayobaki ya kuishi kwake!
10 Kila mhubiri aliye painia msaidizi anakuwa stadi zaidi katika huduma. Kijana mmoja Shahidi alitambua: ‘Nilipokuwa ningali mtoto, nilikuwa na zoezi la kuwashindikiza wazazi wangu katika utendaji wao mbalimbali wa mahubiri. Nilikuwa nikiona hilo kuwa hakika jambo lenye kufurahisha. Lakini siku nenda, nilikuja kutambua kwamba shuleni nilikuwa tofauti na wengine. Nilianza hivyo kujisikia mwenye haya ya kusema juu ya ukweli kwa marafiki zangu. Mahubiri ya nyumba kwa nyumba yaliyokuwa yananiogopesha sana kwa wazo la kwamba ningeweza kukutana na mtu fulani wa shule yangu. Ninafikiri kwamba tatizo langu lilikuwa woga wa mwanadamu. (Mez. 29:25) Baada ya kumaliza shule yangu, nilitaka kujaribu kuwa painia kwa wakati fulani. Matokeo ni kwamba mahubiri yalikuwa na uvutano tofauti juu yangu kuliko nilivyojua hapo kwanza. Sikuyaona tena tangu hapo kama vile utendaji wenye kufurahisha wala kama mzigo wenye kulemea. Kwa kuona vile wale niliokuwa nikijifunza nao Biblia wanaendelea katika ukweli, nilikuwa nikihisi kuridhika kwingi mbele ya ushuhuda ulio wazi wa kwamba Yehova Mungu alikuwa akitegemeza bidii yangu.’ Kijana mwanamume huyo aliendelea kutumikia kama painia wa kawaida.[1]
11 Kulingana na mambo ya hakika, kunapokuwa mapainia wasaidizi wengi kutanikoni, eneo linaweza kutembelewa lote kwa ujumla. Ndugu anayegawa maeneo anaweza kuomba msaada wa mapainia wasaidizi ili kuhubiri katika nafasi zinazotembelewa mara haba. Ikiwa wanabeba chakula na wanatumia mchana kutwa katika utumishi, itawezekana waweze kuhubiri hata katika sehemu za mbali zaidi za eneo.
12 Wazee Wanachukua Mipango: Kwa ajili ya miezi ya Machi, Aprili na Mei, itakuwa vizuri kupanga aina nyingi za ushuhuda kwa nyakati tofauti-tofauti za juma, kutia ndani mwishoni mwa kisha-mchana kati na mwanzoni mwa jioni, ili kwamba wahubiri wengi zaidi waweze kuushiriki. Zaidi ya mahubiri ya kawaida ya nyumba kwa nyumba, tutapanga nyakati ili kutoa ushuhuda barabarani, kuhubiri katika maeneo ya kibiashara na kukutana na wale ambao hawakuwako nyumbani kwao. Kwa kuchukua mipango kama hiyo, wazee watawasaidia mapainia kutumika pamoja na kutaniko kwa wakati unaowafaa zaidi. Kutaniko lingepaswa kujua mipango iliyochukuliwa kwa ajili ya mahubiri. Mikutano kwa ajili ya mahubiri ingepaswa kupangwa vizuri. Zaidi ya hilo, kungepaswa kuwe na maeneo ya kutosha, na tutafikiria kuagiza mbele ya wakati magazeti na vichapo vingine vya kutosha.
13 Panga Programu Yako Binafsi ya Utumishi: Ndugu mmoja ambaye, mwanzoni, alikuwa anasita kuwa painia msaidizi, alisema: “Kwa kweli ni rahisi zaidi kuliko nilivyokuwa ninafikiria. Inatosha tu kuwa na programu nzuri.” Kwenye ukurasa wa mwisho wa nyongeza hii, je! unaona kielelezo cha matumizi ya wakati ya painia msaidizi ambayo inaweza kukustahili? Ili kufikia hilo, inatosha tu kufanya saa 15 katika huduma kila juma.
14 Mara nyingi inawezekana kwa wake wa nyumbani na kwa wale wanaotumika pamoja jioni kuwa mapainia wasaidizi kwa kupanga kuhubiri asubuhi. Vijana wanaokwenda shuleni na wahubiri wanaotumika usiku wanaweza kwa kawaida kutumia mwisho wa kisha-mchana kati katika mahubiri. Wengine, wanaotumika kwa wakati wote, walifikiri kwamba ingewezekana kwao kuchukua mchana kutwa wa likizo kwa juma, au pengine kutumia miisho ya juma yote katika mahubiri, kwa kutoa ushuhuda zaidi wakati wa jioni. Kati ya wale ambao hawawezi kuhubiri isipokuwa tu mwisho wa juma, wengi wanachagua miezi ambayo ina miisho-juma yenye kujaa tano. Mwaka huu, itakuwa vivyo hivyo na miezi ya Machi, Agosti na Novemba. Kwa msaada wa programu iliyo wazi ya ukurasa wa 6, fikiri kwa makini na katika sala juu ya programu ambayo ingefaa vizuri zaidi na hali yako binafsi.
15 Mojawapo wa faida za utumishi wa painia msaidizi ni wepesi wayo. Unaweza kuchagua miezi katika hiyo utakuwa painia, na unaweza hivyo kutumikia kama painia kila mara kwa kadiri unavyotaka. Labda ungependa kuwa painia msaidizi kwa kudumu, lakini usiweze kufanya hivyo. Kwa nini kutokutumikia kama painia kila mwezi hilo linapowezekana? Tofauti na hilo, wengine wanaweza kuwa mapainia wasaidizi mwezi baada ya mwezi muda wa vipindi virefu.
16 Kikanyagio ili Kuwa Painia kwa Wakati Wote: Wengi wa wale walio na roho ya upainia wangependa kuwa mapainia wa kawaida lakini wanajiuliza ikiwa hali yao inawaruhusu na ikiwa watakuwa na wakati wa kutosha na uvumilivu ili kuufikia. Bila shaka yoyote, wengi wa wale walio kwa sasa mapainia wa kawaida hapo kwanza walikuwa mapainia wasaidizi ili kujijaribu kwa kusudi la kuanzisha utumishi wa wakati wote. Kwa mtu kuongeza matumizi yake ya wakati ya painia msaidizi saa moja tu kila siku, au ya mchana kutwa mmoja kwa juma, inawezekana kuwa painia wa kawaida. Ili kuona ikiwa hilo linawezekana kwako, kwa nini usijaribu kutumika saa 90 katika mahubiri muda wa mwezi moja ambamo wewe ni painia msaidizi? Kwa wakati huohuo, utapata ziara za kurudia na mafunzo ya Biblia, jambo ambalo litafanya huduma yako iwe yenye kubadilika na yenye kusawazika.
17 Dada mmoja alipata shangwe ya kuwa painia msaidizi kila mwezi muda wa miaka sita. Mradi wake ulikuwa kuanzisha utumishi wa painia wa kawaidia. Kwa hiyo, alijaribu matumizi manne tofauti ya wakati katika tumaini la kujitengenezea hali fulani itakayomwezesha kufikia mradi wa mapainia wa kawaida, ambao ni wa saa 90. Kila mwezi, alikuwa akipanga programu moja au mbili ili kuhesabu ikiwa ingewezekana. Lakini, alipokuwa akifikiria hilo, alikuwa akisema kwamba huduma ya wakati wote ilikuwa kwake vigumu kuifikia. Aliendelea hata hivyo kuomba uongozi wa Yehova. Ni hivyo siku moja, akiwa katika kutayarisha mkutano wake wa utumishi, alisoma katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Februari 1992 [p. 1 § 5] makala moja iliyokuwa ikisema: “Badala ya kutoa umaana mwingi mno kwenye mradi wa saa, kwa nini kutokukaza akili yako juu ya uwezekano mwingi ambao utendaji huo unatutolea wa kushiriki kwenye mavuno? (Yn. 4:35, 36)” Anaeleza: “Nilisoma sentensi hiyo mara tano au sita na nilikuwa hakika kabisa kwamba lilikuwa jibu la Yehova. Nilichukua hivyo uamuzi wa kuwa painia wa kawaida.” Ijapokuwa ratiba (programu) yake ya kazi ya nusu wakati haikuwa yenye kuambatana, alijaza ombi la upainia wa kawaida. Juma moja baadaye, ratiba yake ilibadilishwa na ile waliompa ilifaa kabisa. Anamalizia kwa kusema: “Je! si kweli kwamba ni mkono wa Yehova?” Na anaongeza: “Ikiwa unamwomba Yehova uongozi wake na kwamba anakutolea wenyewe, usiutupilie mbali: uukubali.” Ikiwa nia halisi ni kuwa painia wa kawaida, baada ya kuwa painia msaidizi muda wa mieizi mitatu mnamo Machi, mnamo Aprili na mnamo Mei labda utakuwa hakika kwamba wewe pia unaweza kuanzisha huduma ya wakati wote.
18 Hatuna shaka kwamba Yehova atabariki juhudi ya watumishi wake na kwamba atategemeza bidii yao ili kujulisha habari njema ya wokovu muda wa kipindi hiki cha utendaji wa pekee kwa kiangazi kijacho. (Is. 52:7; Rum. 10:15) Je! utaitikia mwito kwa ajili ya mapainia wasaidizi 100,000 kwa kuanzisha utumishi huo mnamo Machi? mnamo Aprili? mnamo Mei?
[Box on page 3]
Yale Inafaa Kufanya ili Kuwa Painia Msaidizi
■ Uwe mwenye kutazamia mema
■ Mwombe Yehova abariki bidii yako
■ Alika mhubiri mwingine kuwa painia pamoja nawe
■ Jipangie programu ya utumishi yenye kufaa
■ Agiza magazeti ya kutosha
■ Tegemeza mipango ambayo kutaniko linachukua kwa ajili ya mahubiri
■ Tafuta nafasi za kutoa ushuhuda kwa namna ya vivi hivi
[Examples on page 6]
Matumizi Ya Wakati Ili Kuwa Painia Msaidizi
Mifano ili Kutimiza Saa 15 kwa Juma Katika Mahubiri
Asubuhi—Tangu Siku ya Kwanza Mpaka Siku ya Posho
Siku ya Yenga inaweza kuchukua nafasi ya haidhuru siku gani
SikuWakatiHes. ya Saa
Siku ya KwanzaAsubuhi 2:30
Siku ya PiliAsubuhi2:30
Siku ya TatuAsubuhi2:30
Siku ya NneAsubuhi2:30
Siku ya TanoAsubuhi2:30
Siku ya PoshoAsubuhi2:30
Jumla ya Saa:15
Siku Mbili Zenye Kujaa
Siku mbili za kujichagulia katika juma
SikuWakatiHes. ya Saa
Siku ya TatuMchana7:30
Siku ya PoshoMchana7:30
Jumla ya Saa:15
Jioni Mbili na Mwisho-Juma
Jioni mbili za kujichagulia katika juma
SikuWakatiHes. ya Saa
Siku ya KwanzaJioni1:30
Siku ya TatuJioni1:30
Siku ya PoshoMchana8
Siku ya YengaNusu-Mchana4
Jumla ya Saa:15
Kisha-Mchana Katika Juma na Siku ya Posho
Siku ya Yenga inaweza kuchukua nafasi ya haidhuru siku gani
SikuWakatiHes. ya Saa
Siku ya KwanzaKisha-Mchana2
Siku ya PiliKisha-Mchana2
Siku ya TatuKisha-Mchana2
Siku ya NneKicha-Mchana2
Siku ya TanoKisha-Mchana2
Siku ya PoshoMchana5
Jumla ya Saa:15
Programu Yangu Binafsi ya Mahubiri
Amua hesabu ya saa utakazofanya kwa kila wakati
SikuWakatiHes. ya Saa
Siku ya Kwanza
Siku ya Pili
Siku ya Tatu
Siku ya Nne
Siku ya Tano
Siku ya Posho
Siku ya Yenga
Jumla ya Saa:15