Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • od uku. 179-uku. 184
  • Nyongeza

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Nyongeza
  • Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ubatizo Ni Hatua Inayomuongoza Mutu Kwenye Uhusiano Muzuri Pamoja na Mungu
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Mazungumuzo ya Kumalizia Pamoya na Wale Wenye Watabatizwa
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Utapata Faida Kama Unajikaza Juu Ufikie Kubatizwa?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Je, Vijana Wanapaswa Kubatizwa?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Ona Habari Zaidi
Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
od uku. 179-uku. 184

Nyongeza

Barua kwa Wazazi Wakristo:

Juu uko muzazi, unaona watoto wako kuwa wa lazima sana; na njo maana unapenda kuwasaidia wafikie kumupenda Yehova na kujitoa kwake. Unaweza kufanya nini juu ya kuwasaidia wajitayarishe ili kubatizwa? Namna gani unaweza kujua kama wanakuwa tayari kwa ajili ya ubatizo?

Yesu aliambia wanafunzi wake hivi: “Mufanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, na muwabatize.” (Mt. 28:19) Kulingana na ile maneno, tunaelewa kama mbele mutu abatizwe, inaomba kwanza akuwe mwanafunzi; ni kusema anapaswa kuelewa na kuamini mafundisho ya Kristo na kuifuata kabisa. Hata kijana mudogo anaweza kufanya vile.

Inaomba kwanza weye peke uonyeshe watoto wako mufano ya muzuri, na ujikaze kukazia mafundisho ya Yehova katika mioyo yao. (Kum. 6:6-9) Juu uweze kufanya vile, unaweza kutumia habari zenye kuwa mu kitabu Furahia Maisha Milele! ili kuwafundisha mafundisho ya musingi ya Biblia na kuwasaidia wajue namna ya kufikiri juu ya kanuni zenye kuwa mu Biblia na kuzitumikisha. Usaidie watoto wako wajue namna ya kuelezea wengine mambo yenye wanaamini kwa kutumia maneno yao. (1 Pe. 3:15) Mambo yenye utawafundisha, vitia-moyo vyenye utawapatia, mambo yenye watajifunza mu ibada ya familia ao mu funzo yao ya pekee, ku mikutano ya kutaniko, na marafiki wazuri wenye watapata, njo mambo yenye itawasaidia ili wafanye maendeleo na kufikia kubatizwa, na hata kufanya maendeleo ingine ya kiroho. Uwasaidie ili wajiwekee miradi ya kiroho.

Andiko ya Mezali 20:11 inasema hivi: “Hata mutoto anajulikana kwa matendo yake, kama tabia yake ni safi na yenye kufaa.” Ni matendo gani inaweza kuonyesha ikiwa kijana mwanaume ao mwanamuke alishakuwa mwanafunzi wa Yesu na iko tayari kubatizwa?

Mutoto mwenye kufanya maendeleo ili afikie kubatizwa, anapaswa kutii wazazi wake. (Mdo. 5:29; Kol. 3:20) Biblia inasema hivi juu ya Yesu, wakati alikuwa na miaka 12: “Akaendelea kujitiisha kwa [wazazi wake].” (Lu. 2:51) Kusema kweli, hauwezi kutazamia mutoto akuwe mukamilifu. Lakini, mutoto mwenye kupenda kubatizwa anapaswa kujikaza kufuata mufano wa Yesu, na anapaswa kutii wazazi wake.

Tena, anapaswa kuonyesha kwamba anapenda kujifunza kweli yenye kuwa mu Biblia. (Lu. 2:46) Mutoto yako anapendaka kuenda ku mikutano na kutoa maelezo? (Zb. 122:1) Anakuwaka na hamu ya kusoma Biblia kwa ukawaida na kufanya funzo ya pekee?​​​—Mt. 4:4.

Mutoto mwenye kufanya maendeleo ili afikie kubatizwa, anajikazaka kutia mambo ya Ufalme pa nafasi ya kwanza. (Mt. 6:33) Anaelewa muzuri daraka yake ya kuambia wengine mambo yenye anaamini. Anajikaza kutumia njia mbalimbali za kuhubiri na hasikie haya ya kuambia walimu wake na wanafunzi wenzake kama yeye ni Shahidi wa Yehova. Kama wanamupatia kipindi ku Mukutano Utumishi na Maisha, anakamata ile jambo kwa uzito.

Atajikaza pia kuendelea kuwa na mwenendo safi kwa kuepuka marafiki wabaya. (Mez. 13:20; 1 Ko. 15:33) Ile itaonekana wazi kupitia miziki yenye anapenda kusikiliza, filme yenye anapenda kuangalia, vipindi vya televizyo vyenye anapenda kufuata, michezo yake ya video, na namna anatumikishaka Enternete.

Watoto wengi walibatizwa hata kama walikuwa wangali vijana sana. Waliweza kufanya vile juu walifuata mashauri ya wazazi wao na juu walikamata kwa uzito mafundisho yenye walijifunza mu Biblia. Yehova akubariki kadiri unaendelea kusaidia watoto wako wafikie ile uamuzi ya maana sana katika urafiki wao pamoya na Yehova.

Barua kwa Muhubiri Mwenye Hayabatizwa:

Ni pendeleo kabisa kuwa muhubiri mwenye hayabatizwa mu kutaniko. Unastahili pongezi juu ya maendeleo ya kiroho yenye ulifanya. Kujifunza Biblia kulikusaidia umujue Mungu na uamini kabisa kama ahadi zake zitatimia.​—Yoh. 17:3; Ebr. 11:6.

Pengine mbele uanze kujifunza na Mashahidi wa Yehova, ulikuwaka mu kanisa fulani ao haukukuwaka hata mu kanisa yoyote. Pengine ulikuwa nafanya mambo fulani yenye kupingana na kanuni zenye kuwa mu Biblia. Lakini sasa unaonyesha imani yako kwa kutubu, ni kusema, unahuzunika sana juu zamani ulikuwa nafanya mambo ya mubaya; sasa ulishabadilika, maana yake, ulishaachana kabisa na matendo ya mubaya na kuamua kuendelea kufanya mambo ya muzuri yenye kumufurahisha Mungu.​—Mdo. 3:19.

Pengine ulijua maandishi matakatifu “tangu utoto wako.” Na ile njo ilikusaidia uepuke mwenendo ya mubaya na pia zambi nzito. (2 Ti. 3:15) Ulishajifunza namna ya kufanya kama marafiki ao watu wengine wanakuambia ufanye mambo ya mubaya yenye Yehova anachukia. Unaonyesha kama uko na imani kwa kushikamana na ibada ya kweli na kwa kuhubiria wengine mambo yenye unaamini. Ulishapata mazoezi juu ya namna ya kuhubiri. Sasa unakamata uamuzi wa kuwa muhubiri mwenye hayabatizwa ili umutumikie Yehova.

Kwa hiyo, ikuwe ulimujua Yehova ungali mutoto ao ulimujua na ulishakuwa mukubwa, kuko mambo mbili yenye unaweza kufikiria mu maendeleo yako ya kiroho, ni kusema, kujitoa kwa Mungu na kubatizwa. Unajitoa kwa Yehova wakati unamukaribia katika sala na kumuambia kama ulishaamua kuendelea kumutii yeye tu mu maisha yako yote. (Mt. 16:24) Kisha njo unaweza kubatizwa mu maji ili kuonyesha kama ulishajitoa kwake. (Mt. 28:19, 20) Wakati unajitoa kwa Mungu katika sala na kisha unabatizwa, njo unakuwa sasa mutumishi mwenye kukubaliwa na Yehova Mungu. Ile ni pendeleo ya muzuri kabisa!

Lakini, sawa vile ulijifunza mu Biblia, unaweza kupata magumu mbalimbali. Usisahau mambo yenye ilimufikiaka Yesu wakati mufupi tu kisha kubatizwa; Biblia inasema hivi: “Akaongozwa na roho kuenda katika jangwa ili ajaribiwe na Ibilisi.” (Mt. 4:1) Kisha kuwa mwanafunzi wa Kristo na kubatizwa, utazamie kama utapata majaribu. (Yoh. 15:20) Ile Majaribu inaweza kuya mu njia za mingi. Pengine hata watu wa familia wanaweza kukupinga. (Mt. 10:36) Wanafunzi, wafanyakazi wenzako, na marafiki wako wa zamani wanaweza kukucheka. Kila wakati, ukumbuke maneno ya Yesu yenye kuwa mu andiko ya Marko 10:29, 30: “Kwa kweli ninawaambia ninyi, hakuna mutu mwenye ameacha nyumba ao ndugu ao dada ao mama ao baba ao watoto ao mashamba kwa ajili yangu na kwa ajili ya habari njema mwenye hatapata mara mia moja (100) sasa katika kipindi hiki​—nyumba, ndugu, dada, mama, watoto, mashamba, pamoja na mateso—​na katika mupangilio wa mambo wenye unakuja, uzima wa milele.” Kwa hiyo, uendelee kufanya yako yote ili ubakie karibu na Yehova na ili uishi kulingana na kanuni zake za haki.

Kama unapenda kubatizwa, ambia muratibu wa baraza ya wazee. Kisha hii habari, utaona maulizo yenye wazee watatumia wakati watazungumuza na weye ili waone kama utastahili kubatizwa ao hapana. Unaweza kuanza kurudilia ile maulizo weye peke mu programu yako ya kawaida ya funzo ya pekee.

Wakati uko najitayarisha, ni muzuri ukuwe nasoma na kufikiri sana juu ya Maandiko yenye kutajwa na ile yenye kuonyeshwa mu ile maulizo. Kama unapenda, unaweza kuandika maelezo fulani mu hii kitabu ao hata fasi ingine. Wakati munaanza mazungumuzo pamoya na wazee, weye njo utaamua kama utatumia ile maelezo yenye uliandika ao kama utafungula hii kitabu ao hapana. Kama hauelewe muzuri maulizo fulani, unaweza kuambia ule mwenye unajifunzaka naye Biblia ao wazee ili wakusaidie.

Wakati wazee wako nauliza maulizo, haiko muzuri ukuwe natoa majibu ya murefu sana ao yenye kuwa nguvu kuelewa. Ni muzuri kutoa majibu ya mufupi, tena ya mwepesi mu maneno yako, hapana kusoma tu vile inaandikwa mu kitabu. Ku maulizo ya mingi, wakati uko najibia, ni muzuri kutaya andiko moya ao mbili ili kuonyesha kabisa kama majibu yako inategemea Biblia.

Ikiwa wazee wanaona kama bado hauyajua muzuri kabisa mafundisho ya musingi ya Biblia, watafanya mipango ili kukusaidia uielewe tena zaidi na ukuwe na uwezo wa kuifasiria mu maneno yako; na watakujulisha kama utabatizwa wakati ingine.

[Kwa wazee wa kutaniko: Maagizo juu ya namna ya kuendesha mazungumuzo na wahubiri wenye kupenda kubatizwa iko ku ukurasa wa 208-212.]

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine