MAULIZO KWA AJILI YA WALE WENYE KUPENDA KUBATIZWA
Mazungumuzo ya Kumalizia Pamoya na Wale Wenye Watabatizwa
Kwa kawaida, ubatizo unafanywaka ku mikusanyiko ya Mashahidi wa Yehova. Mu maneno ya kumalizia hotuba ya ubatizo, musemaji ataomba wale wenye watabatizwa wasimame na wajibu kwa sauti maulizo mbili yenye kuwa hapa chini:
1. Ulishatubu zambi zako, ulishajitoa kwa Yehova katika sala, na unakubali wokovu wenye anatoa kupitia Yesu Kristo?
2. Unaelewa kama wakati unabatizwa unakuwa Shahidi wa Yehova na unaingia sasa mu tengenezo yake?
Wakati wale wenye watabatizwa wanajibu ndiyo ku hii maulizo, ‘wanatangaza mbele ya watu wote’ kama wanaamini bei ya ukombozi na kama walishajitoa kabisa kwa Yehova katika sala. (Ro. 10:9, 10) Wale wenye watabatizwa wanapaswa kufikiria sana ile maulizo katika sala mbele ya wakati ili waweze kujibu kulingana na mambo yenye wanaamini kabisa.
Ulishajitoa kwa Yehova katika sala, kwa kumutolea ahadi ya kama ni yeye tu njo utaabudu na kama kitu ya lazima sana mu maisha yako itakuwa kufanya mapenzi yake?
Sasa uko hakika kabisa kama unastahili kubatizwa?
Ni manguo gani yenye kustahili yenye mutu anapaswa kuvala wakati ya kubatizwa? (1 Ti. 2:9, 10; Yoh. 15:19; Flp. 1:10)
Tunapaswa kujipamba “kwa kiasi na akili ya muzuri” ili kuonyesha kama ‘tunashikamana na Mungu.’ Kwa hiyo, wale wenye watabatizwa hawapaswe kuvala manguo yenye kuonyesha sehemu za siri za mwili ao manguo yenye kuwa na maandishi. Kuliko kufanya vile, wanapaswa kuvala manguo yenye kuwa na mupangilio muzuri, yenye kuwa safi na yenye kustahili ile tukio.
Ni mambo gani mutu hapaswe kufanya wakati ya ubatizo? (Lu. 3:21, 22)
Leo, Wakristo wanaweza kuiga namna Yesu alijiendesha wakati alibatizwa. Alijua kama ubatizo ni hatua ya maana sana, na alionyesha vile kupitia mawazo na matendo yake. Kwa hiyo, wakati ya ubatizo, haiko saa ya kuchekesha-chekesha, kucheza, kuogelea, ao kufanya mambo ingine yenye inaweza kushushia heshima ile tukio. Zaidi ya ile, mwenye anatoka tu kubatizwa, hapaswe kufanya alama fulani sawa ile mutu anafanyaka wakati anapata ushindi mukubwa. Hata kama wakati ya ubatizo ni saa ya furaha, inaomba kufurahi kwa heshima.
Juu ya nini kukusanyika kwa ukawaida na ndugu na dada kunaweza kukusaidia utimize ahadi yenye ulimutolea Yehova?
Kisha kubatizwa, juu ya nini inaomba ukuwe unahubiri kwa ukawaida na kuwa na programu ya muzuri ya funzo ya pekee?
MAAGIZO KWA WAZEE WA KUTANIKO
Wakati muhubiri mwenye hayabatizwa anasema kama anapenda kubatizwa, inaomba kumutia moyo arudilie kwa uangalifu habari yenye kichwa “Maulizo kwa Ajili ya Wale Wenye Kupenda Kubatizwa,” yenye kuwa ku ukurasa wa 185-207 wa hii kitabu. Tena, inaomba kumutia moyo asome kwa uangalifu habari yenye kichwa “Barua kwa Muhubiri Mwenye Hayabatizwa,” yenye inaanzia ku ukurasa wa 182. Ile habari inaonyesha namna anaweza kujitayarisha kwa ajili ya mazungumuzo pamoya na wazee. Sawa vile ile habari inaonyesha, mutu mwenye anapenda kubatizwa ataamua ikiwa atatumia mambo yenye aliandika na kama atafungula kitabu yake wakati wa mazungumuzo. Lakini, hapaswe kurudilia na mutu mwingine ile maulizo mbele ya kuzungumuza na wazee.
Kama muhubiri anapenda kubatizwa, anapaswa kumujulisha muratibu wa baraza ya wazee. Wakati ule muhubiri anamaliza kurudilia “Maulizo kwa Ajili ya Wale Wenye Kupenda Kubatizwa,” muratibu wa baraza ya wazee atamuuliza kama alishajitoa kwa Yehova katika sala ili kufanya mapenzi yake. Kama ule muhubiri alishajitoa kwa Yehova, sasa njo muratibu wa baraza ya wazee atafanya mipango ili wazee wawili wazungumuzie naye ile “Maulizo kwa Ajili ya Wale Wenye Kupenda Kubatizwa.” Kila muzee kati ya wale wawili atapewa sehemu yake yenye atazungumuzia na ule muhubiri mwenye anapenda kubatizwa. Haiko lazima kuchunga mupaka tarehe ya mukusanyiko itangazwe njo kuanza kuchunguza ile maulizo.
Kwa kawaida, zile sehemu mbili zinaweza kuzungumuziwa mara mbili; kila sehemu inaweza kufanya saa moya. Lakini, haiko mubaya kufanya zaidi ya saa moya, kama ni lazima. Kila sehemu itaanza na kumalizika kwa sala. Ule muhubiri na muzee mwenye atazungumuza naye hawapaswe kupitia ile maulizo haraka-haraka. Tena, wazee wenye wanapewa ile mugao ao daraka, wanapaswa kuitia pa nafasi ya kwanza mu programu yao.
Kwa kawaida, ni muzuri kurudilia ile maulizo na kila muhubiri mwenye anapenda kubatizwa na iko yeye peke, hapana mu kikundi. Kama ule muhubiri anajibia maulizo yote, ile njo itasaidia wazee waelewe muzuri zaidi kama iko na ujuzi wa kutosha na kama anastahili kubatizwa ao hapana. Zaidi ya ile, ule muhubiri anaweza kujisikia huru kujieleza muzuri zaidi kama iko tu na muzee mwenye kumuuliza maulizo. Kama ni bibi na bwana, muzee anaweza kuzungumuza nao pamoya.
Kama muhubiri mwenye anapenda kubatizwa ni dada, muzee na ule dada wanapaswa kufanyia mazungumuzo fasi kwenye watu wengine wanaweza kuwaona, lakini wasisikie ile mazungumuzo. Kama ni lazima muzee aende na ndugu mwingine, ule ndugu anapaswa kuwa muzee ao mutumishi wa huduma, na ile inategemea sehemu yenye watazungumuzia, sawa vile fungu yenye kufuata inaonyesha.
Mu makutaniko mwenye muko wazee kidogo, watumishi wa huduma wenye kustahili na wenye kuwa na hekima na utambuzi, wanaweza kuchunguza ile maulizo pamoya na mutu mwenye anapenda kubatizwa. watachunguza naye habari yenye kuwa mu “Sehemu ya 1: Mambo Yenye Mukristo Anaamini.” Ni wazee tu njo wanapaswa kuchunguza “Sehemu ya 2: Maisha ya Mukristo.” Kama mu kutaniko hamuna ndugu wenye kustahili kutimiza ile mugao, inaomba kujulisha mwangalizi wa muzunguko; yeye njo ataona kama kutaniko fulani ya karibu inaweza kuwa na wazee wenye uwezo ili kusaidia.
Kama mwenye kupenda kubatizwa ni mutoto kidogo, wazazi wake Wakristo wanapaswa kuwa pale wakati wa mazungumuzo. Kama haitawezekana wazazi wakuwe pale, wazee wawili (ao muzee na mutumishi wa huduma, ile inategemea sehemu yenye watazungumuzia) njo watakuwa mu ile mazungumuzo.
Wazee wanapaswa kuwa hakika kama, mutu mwenye anapenda kubatizwa anajua mafundisho ya musingi ya Biblia kwa kiasi ya kutosha. Zaidi ya ile, wanapaswa kujikaza kujua ikiwa ule muhubiri mwenye anapenda kubatizwa anapendezwa kabisa na kweli na anaonyesha kabisa kwamba anaheshimia sana tengenezo ya Yehova. Kama ule muhubiri hayaelewa kabisa mafundisho ya musingi ya Biblia, wazee watafanya mipango ya kumusaidia ili astahili kubatizwa hata wakati ingine. Pengine, kwa wengine itaomba kuwaachia wakati zaidi ili waonyeshe kama wanapenda kabisa kazi ya kuhubiri ao waonyeshe kama wako najinyenyekeza kwa kufuata mipango ya tengenezo. Itaomba wazee watumie akili ili kujua ikiwa mazungumuzo mu kila sehemu itafanya saa ngapi; ile itawasaidia wajue kabisa ikiwa ule muhubiri anastahili kubatizwa ao hapana. Hata kama maulizo fulani inaweza kukamata wakati mingi na ingine wakati kidogo, yote inapaswa kuzungumuziwa.
Kisha kumaliza sehemu ya pili, wazee wenye walizungumuzia maulizo na mutu mwenye anapenda kubatizwa, watakutana na kuamua ikiwa anastahili kubatizwa ao hapana. Wakati wako nakamata ile uamuzi, watafikiria hali, fasi mutu alizaliwa na kukomalia, uwezo wake, na mambo ingine. Tunapendezwa sana na wale wenye walishamupatia kabisa Yehova moyo wao na wenye walishaelewa mafundisho ya musingi ya Biblia. Musaada wenye mutatolea kwa upendo wale wenye kupenda kubatizwa, utawatayarisha muzuri ili watimize kazi yao ya maana ya kuwa wahubiri wa habari njema.
Kisha, wale wazee wawili wenye walizungumuza na ule muhubiri, ao mumoya kati yao atamujulisha kama anastahili kubatizwa ao hapana. Kama ule mutu anastahili kubatizwa, wazee wanapaswa kuzungumuza naye habari yenye kichwa “Mazungumuzo ya Kumalizia Pamoya na Wale Wenye Watabatizwa,” yenye kuwa ku ukurasa wa 206-207. Kama mwenye kupenda kubatizwa hayamaliza kujifunza kitabu Biblia Inafundisha na kitabu Upendo wa Mungu, wazee wanapaswa kumutia moyo amalizie hata kisha kubatizwa. Inaomba kumuambia kama tarehe yake ya kuzaliwa itawekwa ku Fishe ya Muhubiri ya Kutaniko yenye kuwa na jina yake. Mumukumbushe kama habari zake za kipekee zinaombwa kwa kusudi ya kusaidia tengenezo ya Mashahidi wa Yehova iweze kusimamia muzuri kazi za kidini mu dunia yote; tena ni juu ya kusaidia wahubiri wafanye muzuri kazi yao ya kidini na watiwe moyo kiroho. Zaidi ya ile, wazee wanaweza kukumbusha wahubiri wapya kama, habari yoyote ya kipekee inashugulikiwa kulingana na Kanuni za mu Dunia Yote za Kulinda Habari za Mashahidi wa Yehova zenye kuwa ku jw.org. Kwa kawaida hii mazungumuzo haipaswe kupitisha dakika kumi.
Kisha mwaka moya, wazee wawili wanapaswa kukutana na ule muhubiri mwenye kubatizwa ili kumutia moyo na kumutolea mashauri ya kumusaidia. Muzee mumoya kati ya wale wazee anapaswa kuwa mwangalizi wa kikundi ya mahubiri ya ule muhubiri. Kama ni kijana mudogo, wazazi wake Wakristo wanapaswa kuwa pale wakati wa mazungumuzo. Mazungumuzo inapaswa kuwa yenye kufurahisha sana na yenye kutia moyo. Wazee watazungumuza naye juu ya maendeleo yake ya kiroho na kumutolea mashauri yenye kufaa juu ya namna anaweza kuendelea na mazoea ya muzuri ya funzo ya pekee na kusoma Biblia kila siku, kufanya ibada ya familia ya kila juma, kuhuzuria mikutano kwa ukawaida na kutoa maelezo, na kuhubiri kila juma. (Efe. 5:15, 16) Kama hayamaliza kujifunza kitabu Biblia Inafundisha na kitabu Upendo wa Mungu, wazee wanapaswa kufanya mipango ili ndugu ao dada fulani amusaidie kuvimalizia. Wazee wanapaswa kumupongeza sana kwa upendo. Kwa kawaida, inatosha kumutolea shauri ao pendekezo juu ya jambo moya ao mambo mbili.