Utangulizi wa Sehemu ya 9
Hii sehemu itatusaidia kujua vijana, manabii, na wafalme wenye walionyesha kama wanamuamini kabisa Yehova. Mutoto mwanamuke Mwisraeli mwenye alikuwa anaishi Siria alikuwa hakika kama nabii wa Yehova angeweza kuponyesha Naamani. Nabii Elisha alikuwa hakika kama Yehova angemulinda kutokana na jeshi la maadui. Kuhani Mukubwa Yehoyada alitia uzima wake mu hatari juu ya kulinda mutoto Yehoashi, sababu Atalia, tate (nkambo) yake mwanamuke, mwenye alikuwa muovu sana, alitaka kumuua. Mufalme Hezekia alikuwa hakika kama Yehova ataokoa Yerusalemu, na hata wakati Waashuru walimuogopesha, hakujitia mu mikono yao. Mufalme Yosia alitosha ibada ya sanamu mu inchi yote. Alitengeneza tena hekalu na alitia watu moyo waanze tena kumuabudu Yehova.