WIMBO 117
Tukomalishe Sifa ya Wema
Maandishi
1. Yehova unaonyesha
Wema kwa watu wote.
Na uko mutakatifu
Tena muaminifu.
Unatusamehe zambi
Bila kuhesabia.
Sifa na ibada yetu,
Baba ikufikie.
2. Tunaona wema wako
Kila siku Yehova.
Unasaidia watu
Wajifunze Biblia.
Mambo tuko najifunza
Ni ya lazima sana.
Tupatie roho yako
Ili ituongoze.
3. Yehova tunakuomba
Ili utubariki
Kwa yote tuko nafanya
Kwa ajili ya ndugu.
Na mu kila kutaniko
Na kila familia,
Yehova tusaidie
Tuonyeshane wema.
(Ona pia Zb. 103:10; Mk. 10:18; Gal. 5:22; Efe. 5:9.)