Tuige Wema wa Yehova
1 Baada ya kufurahia kuzama kuzuri kwa jua au chakula kitamu, je, hatuchochewi kushukuru Yehova, Chanzo cha wema wote? Wema wake unatuchochea tutake kumwiga. (Zab. 119:66, 68; Efe. 5:1) Tunawezaje kuonyesha sifa ya wema?
2 Kuelekea Wale Wasioamini: Njia moja ambayo katika hiyo tunaweza kuiga wema wa Yehova ni kwa kuonyesha hangaiko la kweli kuelekea wale ambao katika imani si jamaa zetu. (Gal. 6:10) Kuonyesha wema katika njia halisi kunaweza kuwa na matokeo mazuri juu ya jinsi wanavyoona Mashahidi wa Yehova na ujumbe tunaochukua.
3 Kwa mfano, alipokuwa akingojea kwenye hospitali, kijana mmoja painia alikaa pembeni ya mwanamke mmoja mzee-mzee aliyeonekana kuwa mgonjwa zaidi kuliko wengine wote waliokuwa hapo. Wakati wake ulipofika wa kuonana na daktari, aliruhusu mwanamke huyo achukue nafasi yake. Baadaye, akakutana naye tena, mara hiyo katika soko; mwanamke huyo alikuwa mwenye furaha sana kumwona. Ijapokuwa hapo mbele hakuwa mwenye kupendezwa na habari njema, alisema kwamba alijua sasa kwamba Mashahidi wa Yehova wanapenda majirani zao kwa kweli. Akaanza kujifunza Biblia.
4 Kuelekea Ndugu Zetu: Tunaiga pia wema wa Yehova tunapojitoa ili kusaidia waamini wenzetu. Msiba unapotokea, tunakuwa kati ya watu wa kwanza kusaidia ndugu zetu. Tunaonyesha roho hiyohiyo tunaposaidia wale wanaohitaji kusafirishwa ili kwenda kwenye mikutano, tunapotembelea vilema, na tunapopanuka katika upendo kwa wale tusiowajua vizuri katika kutaniko.—2 Kor. 6:11-13; Ebr. 13:16.
5 Njia nyingine ambayo katika hiyo Yehova anaonyesha wema ni kwa kuwa kwake “tayari kusamehe.” (Zab. 86:5) Kwa kumwiga, tunaweza kuonyesha kwamba tunapenda wema kwa kuwasamehe wengine. (Efe. 4:32) Jambo hilo linasaidia kufanya ushirika wetu na waamini wenzetu uwe ‘mwema na wa kupendeza.’—Zab. 133:1-3.
6 Wema mwingi wa Yehova na utufanye tumsifu sana na kuwa wenye kung’aa kwa shangwe. Na acheni huo utuchochee tujitahidi kuiga wema wake katika mambo yote tunayofanya.—Zab. 145:7; Yer. 31:12.