Maagizo kwa Ajili ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo
Mambo Yenye Kuwa Ndani
1. Maagizo yenye kuwa mu hii dokima itasaidia kila mutu mwenye kuwa na mugao ku mukutano ya Utumishi na Maisha ya Mukristo. Wakati unapata mugao, mbele ya kuutayarisha, unapaswa kufikiria maagizo yenye inahusu mugao wako, yenye kuwa mu Buku ya Mukutano—Utumishi na Maisha ya Mukristo na yenye kuwa mu hii dokima. Inafaa kutia moyo wahubiri wote wakuwe tayari kupitisha bipindi. Bengine benye banahuzuria kwa ukawaida mikutano ya kutaniko banaweza kupitisha bipindi kama banakubali mafundisho ya Biblia na kama maisha yabo inapatana na kanuni za Kikristo. Kama mutu mwenye haiko muhubiri anapenda kukuwa napitisha bipindi, mwangalizi wa Mukutano Utumishi na Maisha anapaswa kuzungumuza naye juu ya kuona kama anatimiza sifa zenye kuombwa. Kisha kuchunguza ule mutu, mwangalizi wa Mukutano ya Utumishi na Maisha atamujulisha ikiwa anastahili ao hapana. Wakati ya ile mazungumuzo, mwalimu wa ule mwanafunzi (ao muzazi mwenye kuamini) anapaswa kuwa pale. Sifa zenye kuombwa ni zile tu zenye mutu mwenye anapenda kuwa muhubiri mwenye hayabatizwa anapaswa kutimiza.—od sura ya 8 fu. 8.
MANENO YA UTANGULIZI
2. Dakika 1. Kila juma, kisha wimbo na sala ya kwanza, musimamizi wa Mukutano Utumishi na Maisha anapaswa kusema mambo fulani yenye itapatia batu hamu ya kufuata programu ya ile siku, na atakazia sana mambo yenye italetea kutaniko faida.
UTAJIRI WA NENO YA MUNGU
3. Hotuba: Dakika 10. Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha inatoa kichwa na maelezo ya mufupi juu ya mambo makubwa mbili ao tatu ya kuzungumuzia. Hii hotuba inapaswa kupewa muzee ao mutumishi wa huduma mwenye iko na uwezo wa kuipitisha muzuri. Wakati tunaanza kitabu mupya ya Biblia mu usomaji wa Biblia wa kila juma, video ya utangulizi ya ile kitabu itaonyeshwa. Musemaji anaweza kuonyesha namna gani mambo yenye iko mu ile video inapatana na kichwa ya habari. Lakini, asikose kuzungumuzia mawazo yote yenye inaonyeshwa mu hotuba yake mu buku ya mukutano. Tena, anapaswa kuzungumuzia picha yenye imetayarishwa juu ya kukazia mawazo makubwa. Pia, kama kuko habari ingine yenye inapatana na hotuba yake, anaweza kuitia ndani.
4. Mali ya Kiroho: Dakika 10. Ni sehemu ya maulizo na majibu. Haina maneno ya utangulizi ao ya kumalizia. Inapaswa kutolewa na muzee ao mutumishi wa huduma mwenye iko na uwezo wa kuipitisha muzuri. Anapaswa kuuliza maulizo yote mbili. Tena, anaweza kuamua kama ni lazima kusoma maandiko ao hapana. Majibu ya ndugu na dada haipaswe kupitisha segonde 30.
5. Usomaji wa Biblia: Dakika 4. Mwanaume njo anapaswa kufanya hii kipindi. Mwanafunzi atasoma sehemu yake bila kusema maneno ya utangulizi ao ya kumalizia. Musimamizi wa mukutano atatafuta zaidi sana kusaidia banafunzi basome bila makosa, basome kwa njia yenye inaeleweka, basome bila kusita-sita, bakazie mambo makubwa, babadilishe sauti, bajue ni fasi gani inaomba kutua, na basome kwa njia ya kawaida. Juu sehemu fulani za usomaji wa Biblia ni za murefu na zingine ni za mufupi, mwangalizi wa Mukutano ya Utumishi na Maisha ya Mukristo anapaswa kufikiria uwezo wa kila mwanafunzi mbele ya kumupatia hii kipindi.
TUJITOE KABISA MU KAZI YA KUHUBIRI
6. Dakika 15. Hii sehemu inapatia bote nafasi ya kufanya mazoezi juu ya namna ya kuhubiri na inabasaidia bakomalishe ufundi yabo ya kuzungumuza na batu, na pia ufundi yabo ya kuhubiri na kufundisha. Kama ni lazima, bazee pia banaweza kupewa migao ya banafunzi. Kila mwanafunzi anapaswa kutumikisha somo ya mu broshua Kufundisha ao Penda Watu yenye inaonyeshwa mu paranteze chini ya kipindi yake mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha. Wakati fulani, sehemu ya mazungumuzo pamoya na basikilizaji itakuwa napangwa. Ile sehemu itakuwa naongozwa na muzee ao mutumishi wa huduma mwenye iko na uwezo wa kuipitisha muzuri.—Ona fungu ya 15 juu ya kujua namna ya kuongoza sehemu ya mazungumuzo pamoya na basikilizaji.
7. Kuanzisha Mazungumuzo: Hii kipindi inaweza kupitishwa na mwanafunzi mwanaume ao mwanamuke. Kama mwanafunzi ni mwanaume, musikilizaji wake anapaswa kuwa mwanaume ao mutu wa familia yake; na kama ni mwanamuke, musikilizaji wake anapaswa kuwa mwanamuke ao mutu wa familia yake. Mwanafunzi na musikilizaji wake banaweza kuikala ao kusimama.—Juu ya kujua habari ya kuzungumuzia na namna kipindi inaweza kupitishwa, ona fungu ya 12 na ya 13.
8. Kuendelesha Mazungumuzo: Hii kipindi inaweza kupitishwa na mwanafunzi mwanaume ao mwanamuke. Kama mwanafunzi ni mwanaume, musikilizaji wake anapaswa kuwa mwanaume; na kama ni mwanamuke, musikilizaji wake anapaswa kuwa mwanamuke. (km 5/97 uku. 2) Mwanafunzi na musikilizaji wake banaweza kuikala ao kusimama. Kusudi ya mwanafunzi ni kusaidia batu bajue namna ya kuendelesha mazungumuzo na mutu mwenye balishakahubiria.—Juu ya kujua habari ya kuzungumuzia na namna kipindi inaweza kupitishwa, ona fungu ya 12 na ya 13.
9. Kufanya Banafunzi: Hii kipindi inaweza kupitishwa na mwanafunzi mwanaume ao mwanamuke. Kama mwanafunzi ni mwanaume, musikilizaji wake anapaswa kuwa mwanaume; na kama ni mwanamuke, musikilizaji wake anapaswa kuwa mwanamuke. (km 5/97 uku. 2) Mwanafunzi na musikilizaji wake banaweza kuikala ao kusimama. Wakati iko naonyesha namna ya kuongoza funzo ya Biblia yenye ilishakaanza, haiko lazima mwanafunzi aseme maneno ya utangulizi ao ya kumalizia. Anaweza kufanya vile kama tu somo yenye alipewa inamuomba kufanya vile. Haiko lazima kusoma kwa sauti mafungu yote yenye kuonyeshwa, hata kama haiko mubaya kufanya vile.
10. Kufasiria Mambo Yenye Unaamini: Kama hii kipindi ni hotuba, mwanafunzi mwanaume njo ataipitisha. Kama ni onyesho, mwanafunzi mwanaume ao mwanamuke anaweza kuipitisha. Kama mwanafunzi ni mwanaume, musikilizaji wake anapaswa kuwa mwanaume ao mutu wa familia yake; na kama ni mwanamuke, musikilizaji wake anapaswa kuwa mwanamuke ao mutu wa familia yake. Kwa kutumia habari yenye kuwa mu referanse yenye ilitolewa, mwanafunzi anapaswa kujibia ulizo ya hotuba ao ya onyesho kwa busara na mu njia yenye kuwa wazi. Mwanafunzi iko huru kuamua kama atataya referanse saa iko napitisha kipindi yake ao hapana.
11. Hotuba: Mwanaume njo anapaswa kufanya hii kipindi na ataipitisha sawa vile hotuba mbele ya kutaniko. Kama hotuba inategemea nukta moya ya mu nyongeza ya A ya broshua Penda Watu, mwanafunzi ataonyesha namna ya kutumia ile maandiko mu mahubiri. Kwa mufano, anaweza kufasiria ni wakati gani ile andiko inaweza kutumiwa, maana ya ile andiko, na namna ya kufikiri na mutu juu ya ile andiko. Kama hotuba inategemea wazo moya ya mu broshua Penda Watu, mwanafunzi atakazia namna ya kutumikisha ile wazo mu mahubiri. Anaweza kukazia zaidi mufano yenye kuwa mu nukta ya 1 ya somo, ao kukazia maandiko ingine yenye kuwa mu somo, kama ile inaweza kusaidia.
12. Habari ya Kuzungumuzia: Habari yenye kuwa mu hii fungu na mu fungu yenye kufuata inahusu sehemu “Kuanzisha Mazungumuzo” na “Kuendelesha Mazungumuzo.” Kama hakuna maagizo ingine, kusudi ya mwanafunzi ni kuambia musikilizaji kweli fulani ya Biblia yenye inaweza kumufurahisha na kuweka kilalo kwa ajili ya mazungumuzo yenye itafuata. Mwanafunzi anaweza kuchagua habari yenye batu batafurahia mu eneo na yenye batu bako nazungumuzia sana. Iko huru kuamua kama atatumia kichapo ao video moya yenye kuwa mu Vyombo Vyetu vya Kufundishia. Kuliko kutia mu akili mambo yote yenye atasema, mwanafunzi anapaswa njo kujikaza kukomalisha sifa mbalimbali, sawa vile kujitia ku fasi ya mutu na kuzungumuza mu njia ya kawaida.
13. Aina ya Mahubiri: Mwanafunzi anapaswa kupatanisha kipindi yenye alipewa kulingana na hali ya eneo. Kwa mufano:
(1) Mahubiri ya Nyumba kwa Nyumba: Hii aina ya mahubiri inamaanisha kuhubiri nyumba kwa nyumba; ikuwe uso kwa uso, kupitia telefone ao barua. Hii aina ya mahubiri inatia ndani pia kumurudilia mutu juu ya kuendelesha mazungumuzo yenye ulianzisha wakati ulimutembelea mu mahubiri ya nyumba kwa nyumba.
(2) Mahubiri ya Wakati Wowote: Kusudi ya hii kipindi ni kuonyesha namna ya kugeuza mazungumuzo ya kawaida ikuwe mahubiri. Unaweza kuzungumuzia wazo ya andiko fulani pamoya na watu wenye unakutana nao mu kazi, ku masomo, karibu na kwenye unaikalaka, mu bisi ao fasi ingine yoyote wakati uko naenda mu kazi yako ya kila siku.
(3) Mahubiri ya Mahali pa Watu Wengi: Hii aina ya mahubiri inaweza kuwa mahubiri ya ku prezantware, fasi kwenye batu banauzishaka na kutumika, mu barabara, mu park, mu maparking ao fasi yoyote kwenye batu banaweza kupatikana.
14. Matumizi ya Video na Bichapo: Kulingana na hali, mwanafunzi ataamua kama anaweza kuonyesha video ao kutoa kichapo. Kama kipindi inatia ndani kuonyesha video ao kama mwanafunzi anaamua kutumia video, atafanya utangulizi ya ile video na kuizungumuzia na musikilizaji wake bila kuionyesha.
MAISHA YA MUKRISTO
15. Kisha wimbo, hii sehemu ya dakika 15 itakuwa na kipindi moya ao mbili ya kusaidia basikilizaji bajue namna ya kutumikisha Neno ya Mungu mu maisha yabo. Kama hakuna maagizo fulani yenye kuonyeshwa, bile bipindi binaweza kupewa bazee ao batumishi ya huduma benye bako na uwezo ya kubipitisha muzuri. Lakini kama ni mahitaji ya kutaniko, inapaswa kupitishwa na muzee. Kama sehemu yenye kutolewa ni mazungumuzo, ndugu mwenye kupewa hii sehemu anaweza kutumia maulizo ingine ili kukazia mambo makubwa yenye kuwa mu ile habari. Anapaswa kufanya utangulizi mufupi juu apate nafasi ya kuzungumuzia mawazo makubwa na kuachia basikilizaji nafasi ya kutoa maelezo. Kama kuko sehemu ya kuuliza mutu maulizo, itakuwa muzuri ndugu ao dada mwenye ataulizwa maulizo apite mbele, kama inawezekana, kuliko kubakia fasi yake.
16. Funzo ya Biblia ya Kutaniko: Dakika 30. Hii sehemu inapaswa kupewa muzee mwenye iko na uwezo wa kuiongoza muzuri. (Mu makutaniko yenye haina bazee bamingi, batumishi ya huduma benye bako na uwezo ya kuiongoza muzuri banaweza kuiongoza.) Baraza ya bazee inapaswa kuamua kama ni banani njo banastahili kuongoza Funzo ya Biblia ya Kutaniko. Bandugu benye kuchaguliwa banapaswa kuwa na uwezo wa kuongoza funzo muzuri kwa kuheshimia wakati, kukazia maandiko ya musingi, na kusaidia basikilizaji baone namna ya kutumikisha habari yenye kuzungumuziwa. Benye kuongoza batachunguza maagizo yenye inapatikana juu ya namna ya kuongoza sehemu ya maulizo na majibu. (w23.04 uku. 24, kisanduku) Kisha kujifunza kwa uangalifu habari yenye ilitayarishwa kwa ajili ya ile juma, haiko lazima kurefusha funzo. Ikiwezekana, ni muzuri kila juma kubadilisha kiongozi na musomaji. Kama musimamizi wa Mukutano ya Utumishi na Maisha anaomba funzo ifupishwe, kiongozi ataamua namna ya kufanya ili kuifupisha. Anaweza kuamua mafungu fulani isisomewe.
MANENO YA KUMALIZIA
17. Dakika 3. Musimamizi wa Mukutano ya Utumishi na Maisha atarudilia mambo fulani ya lazima yenye ilizungumuziwa ku mukutano. Kama wakati inaruhusu, anaweza kufanya vile kwa kuomba basikilizaji baseme mambo yenye balifurahia. Ataonyesha pia mambo fulani yenye itazungumuziwa ku mukutano juma ya kufuata. Kama wakati inaruhusu, anaweza kutaya majina ya banafunzi benye batakuwa na bipindi mu juma ya kufuata. Kama hakuna maagizo tofauti, musimamizi wa mukutano njo mwenye atatoa matangazo ya lazima ao kusoma barua fulani, kama ni lazima, mu maneno yake ya kumalizia. Matangazo ya kawaida, kwa mufano yenye inahusu mikutano ya mahubiri ao usafi, haipaswe kutangazwa ku jukwaa, lakini inapaswa kuwekwa ku tablo ya matangazo. Musimamizi akiona kama haitawezekana kupitisha matangazo yote ao kusoma barua zote mu dakika za kumalizia zenye amepewa, anaweza kuomba bandugu benye batapitisha migao mu sehemu Maisha ya Mukristo bapunguze wakati yabo, ikiwezekana, juu apate wakati ya kusoma ile matangazo. (Ona fungu ya 16 na ya 19.) Mukutano utamalizika kwa wimbo na sala.
KUPONGEZA NA KUTOA MASHAURI
18. Kisha kila kipindi ya mwanafunzi, musimamizi wa Mukutano Utumishi na Maisha iko na dakika moya hivi juu ya kumupongeza na kumutolea mashauri kwa kutumia somo yenye alipewa. Wakati musimamizi anaalika mwanafunzi apitishe kipindi yake, hataonyesha somo yenye alipewa. Lakini, kisha mwanafunzi kupitisha kipindi yake na kisha kumupongeza, musimamizi anaweza kuonyesha somo yenye mwanafunzi alikuwa anatumikia. Kisha, atasema mambo yenye inaonyesha kama aliitumikia muzuri, ao kumuonyesha kwa upole juu ya nini itakuwa muzuri aendelee kutumikia ile somo na namna atafanya vile. Musimamizi anaweza pia kuzungumuzia mambo ingine yenye mwanafunzi alifanya mu onyesho, yenye anawaza kama inaweza kusaidia mwanafunzi na kutaniko. Anaweza kupatia mwanafunzi mashauri ingine kipekee, yenye inatoka mu broshua Penda Watu, broshua Kufundisha, ao kitabu Shule ya Huduma. Atafanya vile kisha mukutano ao wakati ingine. Ile mashauri itahusu somo yenye alipewa ao somo ingine.—Ili kupata habari zaidi kuhusu daraka ya musimamizi wa Mukutano ya Utumishi na Maisha na daraka ya mushauri musaidizi, ona fungu ya 19, 24, na ya 25.
WAKATI
19. Hakuna sehemu yenye inapaswa kupitisha wakati, hata mashauri ya musimamizi haipaswe kupitisha wakati. Hata kama Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha inaonyesha wakati ya kila sehemu, haiko lazima mutu arefushe habari yake juu tu ya kueneza dakika kama alishazungumuzia mambo yote. Kama bandugu bengine benye kupitisha migao banapitisha wakati, mushauri musaidizi wa Mukutano ya Utumishi na Maisha anapaswa kubashauria kipekee. (Ona fungu ya 24 na ya 25.) Mukutano yote, kuchanga nyimbo na sala, inapaswa kufanya saa 1 na dakika 45.
WAKATI MWANGALIZI WA MUZUNGUKO ANATEMBELEA KUTANIKO
20. Kama mwangalizi wa muzunguko anatembelea kutaniko, programu itaendeshwa namna imeonyeshwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha, isipokuwa tu: Mu sehemu Maisha ya Mukristo, hakutakuwa Funzo ya Biblia ya Kutaniko juu kutakuwa hotuba ya utumishi ya mwangalizi wa muzunguko ya dakika 30. Mbele hotuba ya utumishi ya mwangalizi wa muzunguko ianze, musimamizi wa Mukutano Utumishi na Maisha atarudilia mambo fulani yenye ilizungumuziwa, ataonyesha mambo fulani yenye itazungumuziwa mu juma ya kufuata, atasoma matangazo ya lazima na kusoma barua zenye zinapaswa kusomewa, kisha ataalika mwangalizi wa muzunguko. Kisha hotuba ya utumishi, mwangalizi wa muzunguko atamalizia mukutano kwa wimbo yenye atachagua. Anaweza kualika ndugu mwengine amalizie kwa sala. Hakutakuwa masomo mu jumba ya pili ao ya tatu. Kama kutaniko iko na kikundi ya luga ingine, ile kikundi inaweza kufanya mikutano yake kama kawaida. Lakini, itajiunga na kutaniko juu ya kusikiliza hotuba ya utumishi ya mwangalizi wa muzunguko.
JUMA YA MUKUSANYIKO WA MUZUNGUKO AO WA ENEO
21. Hakutakuwa mukutano wowote wa kutaniko mu juma ya mukusanyiko wa muzunguko ao wa eneo. Kutaniko inapaswa kukumbushwa kama habari zenye zilipangwa kwa ajili ya mikutano ya ile juma zinapaswa kuchunguzwa wakati ya funzo ya kipekee ao wakati ya ibada ya familia.
JUMA YA UKUMBUSHO
22. Kama Ukumbusho inakuwa katikati ya juma, hakutakuwa Mukutano ya Utumishi na Maisha.
MWANGALIZI WA MUKUTANO YA UTUMISHI NA MAISHA
23. Baraza ya bazee inapaswa kuchagua muzee moya akuwe mwangalizi wa Mukutano Utumishi na Maisha. Daraka yake ni kuhakikisha kama hii mukutano inapangwa muzuri na kuongozwa kulingana na maagizo yenye iko mu hii dokima. Anapaswa kupashana habari kwa ukawaida na mushauri musaidizi. Wakati tu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha inatoka, mwangalizi wa Mukutano ya Utumishi na Maisha anapaswa kupanga bipindi byote bya ile miezi mbili. Ni yeye njo anapaswa kupanga bipindi byote, ikuwe bya wanafunzi ao byenye habiko bya wanafunzi. Anapaswa pia kupanga basimamizi ya mukutano wa katikati ya juma kati ya bale benye bamekubaliwa na baraza ya bazee. (Ona fungu ya 3-16 na ya 24.) Wakati iko napanga migao ya banafunzi, anapaswa kufikiria miaka ya mwanafunzi, uwezo wake na uhuru wa kujieleza kuhusu habari yenye atazungumuzia. Anapaswa kufanya vilevile wakati iko napanga migao ya sehemu zingine za mikutano. Kila mutu mwenye kuhusika anapaswa kujulishwa kama iko na kipindi majuma 3 hivi mbele ya tarehe ya kipindi yake. Fomu Utumishi na Maisha ya Mukristo—Karatasi ya Mugao (S-89) inapaswa kutumiwa kwa ajili ya bipindi bya banafunzi. Mwangalizi wa Mukutano ya Utumishi na Maisha anapaswa kuhakikisha kama kopi ya programe imewekwa ku tablo ya matangazo. Baraza ya bazee inaweza kuchagua muzee ao mutumishi wa huduma mwengine ili amusaidie. Hata vile, ni bazee tu njo banapaswa kutumiwa juu kupanga bipindi byenye habiko bya banafunzi.
MUSIMAMIZI WA MUKUTANO YA UTUMISHI NA MAISHA
24. Kila juma, muzee moya atasimamia Mukutano ya Utumishi na Maisha. (Mu makutaniko yenye haina bazee bamingi, batumishi ya huduma benye biko na uwezo banaweza kuombwa basimamie mukutano.) Musimamizi anapaswa kutayarisha maneno ya utangulizi na ya kumalizia. Atatanguliza pia kila sehemu, na kulingana na hesabu ya bazee mu baraza, anaweza kupitisha sehemu fulani za mukutano, zaidi sana sehemu zenye zinaomba tu kuonyesha video bila mazungumuzo yoyote pamoya na wasikilizaji. Maelezo yake kisha sehemu fulani na mbele ya kualika sehemu ingine inapaswa kuwa ya mufupi sana. Baraza ya bazee itaamua ni bazee gani njo biko na uwezo ya kusimamia muzuri mukutano. Bazee benye batachaguliwa batakuwa banasimamia mukutano kwa kubadilishana. Kulingana na hali ya kwenu, mwangalizi wa Mukutano Utumishi na Maisha anaweza kuwa anasimamia mukutano mara mingi kuliko bazee bengine. Kama muzee fulani iko na uwezo ya kuongoza muzuri Funzo ya Biblia ya Kutaniko, inawezekana akuwe pia musimamizi wa mukutano. Lakini, inaomba pia musimamizi wa mukutano akuwe na uwezo ya kupongeza banafunzi, na kubapatia mashauri kwa upendo, kama ni lazima. Anapaswa pia kuhakikisha kama mukutano unamalizika kwa wakati. (Ona fungu ya 17 na ya 19.) Kama musimamizi anapenda, na kama kuko fasi ya kuenea ku jukwaa, munaweza kutia mikro ingine ku jukwaa juu musimamizi aitumie ili kutanguliza sehemu ya kufuata wakati ndugu mwenye atatoa ile sehemu iko naenda ku kinara (pupitre) ya musemaji. Tena, kama musimamizi anapenda, anaweza kuikala ku kiti ku jukwaa wakati ya Usomaji wa Biblia na wakati ya sehemu Tujitoe Kabisa mu Kazi ya Kuhubiri. Ile inaweza kusaidia kukomboa wakati.
MUSHAURI MUSAIDIZI
25. Kazi yake ni kushauria bazee na batumishi ya huduma kipekee, kama ni lazima, kuhusiana na migao yoyote ya ufundishaji yenye balipewa. Inaweza kuwa mugao ku Mukutano Utumishi na Maisha, hotuba ya watu wote, kuongoza funzo ya Munara wa Mulinzi, Funzo ya Biblia ya Kutaniko, ao kusoma mafungu ku mikutano.—Ona fungu ya 19.
MASOMO MU JUMBA YA PILI AO YA TATU
26. Kulingana na hesabu ya banafunzi, kutaniko inaweza kupanga banafunzi bengine bapitishe bipindi mu jumba ya pili ao jumba ya tatu. Kila jumba inapaswa kuwa na mushauri mwenye iko na uwezo wa kusimamia muzuri; na ni muzuri zaidi akuwe muzee. Kama ni lazima, hata mutumishi wa huduma mwenye iko kabisa na uwezo wa kusimamia muzuri anaweza kusimamia. Baraza ya bazee inapaswa kuamua ni nani anaweza kupewa ile daraka na kama ni lazima kubadilishana ao hapana. Mushauri anapaswa kufuata muongozo yenye kupatikana mu fungu ya 18. Kama kutaniko imepanga kukuwe jumba ya pili na jumba ya tatu, banafunzi benye biko na bipindi mule bataombwa kuenda kisha sehemu Mali ya Kiroho, ya Utajiri wa Neno ya Mungu. Batarudia mu jumba ya kwanza kisha kipindi ya mwanafunzi wa mwisho.
VIDEO
27. Video zitatumiwa mu hii mukutano. Zile video zitapatikana ku JW Library® na mutu anaweza kuziangalia kwa kutumia bitu mbalimbali ya kielektronike.
© 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
S-38-ZS 9/25