Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w12 1/9 uku. 16-17
  • Siku ya Hukumu Itakuwa Namna Gani?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Siku ya Hukumu Itakuwa Namna Gani?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Siku ya Hukumu​—Ni Nini?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
w12 1/9 uku. 16-17

Neno la Mungu Linafundisha Nini?

Siku ya Hukumu Itakuwa Namna Gani?

Habari hii inazungumuzia maulizo fulani ambayo labda umekwisha kujiuliza na inaonyesha mahali ambapo unaweza kupata majibu katika Biblia. Mashahidi wa Yehova watafurahi kukusaidia upate majibu ya maulizo hayo.

1. Siku ya Hukumu ni nini?

Kama inavyoonyeshwa kwenye picha iliyo hapa pembeni, watu wengi wanawaza kama Siku ya Hukumu watu wote watapelekwa mbele ya kiti cha ufalme cha Mungu, ili wahukumiwe kupatana na matendo yao ya zamani; wale waliofanya mambo mazuri wataenda kuishi mbinguni na wale waliofanya mambo mabaya watateseka katika moto wa mateso. Lakini, Biblia inaonyesha kama kusudi la Siku ya Hukumu ni kuokoa watu ili wasisumbuliwe tena na mambo ya ukosefu wa haki. (Zaburi 96:13) Mungu amemufanya Yesu kuwa Muamuzi atakayerudisha haki duniani.​—Soma Isaya 11:1-5; Matendo 17:31.

2. Siku ya Hukumu itarudisha haki namna gani?

Wakati Adamu, mutu wa kwanza, alimuasi Mungu kimakusudi, aliwaletea watu wote zambi, mateso, na kifo. (Waroma 5:12) Ili kutengeneza hali hiyo, Yesu atafufua mamilioni ya watu waliokufa. Kitabu cha Ufunuo kinaonyesha kama mambo hayo yatafanyika katika miaka 1 000 ya utawala wa Kristo Yesu.​—Soma Ufunuo 20:4, 11, 12.

Wale watakaofufuliwa hawatahukumiwa kupatana na mambo waliyofanya mbele ya kufa, lakini watahukumiwa kupatana na mambo watakayofanya wakati “vitabu vya kukunjwa” vinavyotajwa katika Ufunuo sura ya 20 vitafunguliwa. (Waroma 6:7) Mutume Paulo alionyesha kama kutakuwa vikundi viwili vya watu watakaofufuliwa na kupewa nafasi ya kujifunza juu ya Mungu: “Waadilifu na wasio waadilifu pia.”​—Soma Matendo 24:15.

3. Siku ya Hukumu itatimiza mambo gani?

Watu ambao walikufa bila kumujua Yehova Mungu na kumutumikia, watapewa nafasi ya kubadilika na kufanya mema. Ikiwa wanafanya hivyo, ufufuo wao utakuwa “ufufuo wa uzima.” Lakini, watu fulani kati yao watakataa kujifunza njia za Yehova. Ufufuo wao utakuwa “ufufuo wa hukumu.”​—Soma Yohana 5:28, 29; Isaya 26:10; 65:20.

Mwishoni mwa Siku ya Hukumu ya miaka 1 000, Yehova atakuwa amerudishia watu watiifu hali ya ukamilifu ambayo Adamu alipoteza. (1 Wakorintho 15:24-28) Hilo ni tumaini nzuri sana kwa watu wote watiifu! Kisha kutakuwa jaribu la mwisho wakati ambapo Mungu atamufungua Shetani Ibilisi, ambaye alikuwa amefungwa katika shimo la abiso kwa miaka 1 000. Shetani atajaribu tena kuwadanganya watu wamuache Yehova, lakini wale watakaomupinga Shetani wataishi milele duniani.​—Soma Isaya 25:8; Ufunuo 20:7-9.

4. Je, kuna siku ingine ya hukumu itakayowaletea wanadamu faida?

Biblia inatumia pia neno “siku ya hukumu” inapozungumuzia mwisho wa ulimwengu huu. Siku ingine hiyo ya hukumu itakuja kwa kushitukia kama Garika ya wakati wa Noa, ambayo iliharibu watu wabaya wote. Jambo la kufurahisha ni kwamba uharibifu wa ‘watu wasiomuogopa Mungu’ unakaribia sana. Kisha uharibifu huo, watu wazuri wataishi katika dunia mupya ambamo “uadilifu utakaa.”​—Soma 2 Petro 3:6, 7, 13.

Ili kupata habari zingine, usome ukurasa wa 213-215 wa kitabu hiki, Biblia Inafundisha Nini Hasa?, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

[Picha katika ukurasa wa 16]

“Hukumu ya mwisho,” kulingana na Gustave Doré, 1832-1883

[Picha zimetolewa na]

Muchoro wa Doré

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine