Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w15 1/5 uku. 16
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Siku ya Hukumu Itakuwa Namna Gani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Siku ya Hukumu​—Ni Nini?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 1/5 uku. 16

MAULIZO JUU YA HABARI ZA BIBLIA YANAJIBIWA

Siku ya Hukumu ni nini?

Familia yenye furaha inaungana tena kupitia ufufuo katika kipindi cha miaka elfu moja

Sababu gani siku ya hukumu itakuwa wakati wa furaha?

Wakati wa zamani, Mungu alitumia waamuzi ili kuokoa watu wake wasitendewe tena bila haki. (Waamuzi 2:18) Biblia inasema kama Siku ya Hukumu ya wakati unaokuja itakuwa wakati wa furaha. Wakati huo Yehova, Muamuzi wa dunia yote, ataokoa wanadamu ili wasitendewe tena bila haki.—Soma Zaburi 96:12, 13; Isaya 26:9.

Mungu amemuchagua Yesu ili awahukumu kwa haki watu wazima na watu waliokufa. (Matendo 10:42; 17:31) Watu wengi wamekufa bila kumujua Mungu. Katika Siku ya Hukumu, Yesu atafufua watu hao ili wapate nafasi ya kumujua Mungu wa kweli na kumupenda.—Soma Matendo 24:15.

Sababu gani Siku ya Hukumu itafanya miaka elfu moja?

Watu waliokufa watafufuliwa katika kipindi cha miaka elfu moja. (Ufunuo 20:4, 12) Watakuwa na lazima ya wakati ili waweze kujifunza sheria za Mungu na kumutii. Tofauti na mawazo ya watu wengi, Biblia inaonyesha kama watu watahukumiwa kulingana na mambo yenye watafanya kisha kufufuliwa.—Soma Waroma 6:7.

Biblia inazungumuzia siku ya hukumu yenye itatokea bila watu kuwazia mbele ya ile miaka elfu moja kuanza. Kama vile habari kubwa ya gazeti hili inaonyesha, siku hiyo inaitwa pia mwisho. Katika siku hiyo, Mungu ataharibu watu wote wenye hawamuogope, ni kusema, watu wabaya. (2 Petro 3:7) Kwa hiyo, ni lazima tuonyeshe kama tunamupenda Mungu.—Soma 2 Petro 3:9, 13.

Ili kupata habari zingine, soma ukurasa wa 213 wa kitabu hiki, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Unaweza pia kupata kitabu hiki kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine