Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w13 1/12 uku. 16
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Je, Mungu Ataleta Serikali Moja Itakayotawala Dunia Yote?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 1/12 uku. 16

Maulizo Juu Ya Habari Za Biblia Yanajibiwa

Sababu gani Kristo atarudia?

Mbele Yesu Kristo apande kuenda mbinguni katika mwaka wa 33, aliahidi kwamba atarudia. Alijifananisha na tajiri ambaye alisafiri kwa muda murefu na wakati alirudia alikuwa na mamlaka ya kutawala akiwa mufalme. Yesu atarudia ili kuwaletea wanadamu serikali nzuri.​—Soma Luka 19:11, 12.

Yesu atawaletea wanadamu serikali nzuri

Kristo atarudia katika mwili wa aina gani? Alifufuliwa akiwa mutu wa roho asiyeonekana. (1 Petro 3:18) Kisha, akaenda mbinguni na akakaa kwenye mukono wa kuume wa Mungu. (Zaburi 110:1) Miaka mingi baadaye, Yesu aliletwa mbele ya Yehova Mungu, ‘Muzee wa Siku,’ ambaye alimupatia mamlaka ya kutawala wanadamu. Kwa hiyo, Yesu hatarudia katika mwili wa kibinadamu, lakini atarudia kama Mufalme asiyeonekana.​—Soma Danieli 7:13, 14.

Yesu atafanya nini atakaporudia?

Wakati Yesu atarudia bila kuonekana pamoja na malaika zake, atawahukumu wanadamu. Ataharibu watu waovu na kuwapatia uzima wa milele wale ambao wanamukubali kuwa Mufalme.​—Soma Mathayo 25:31-33, 46.

Utawala wa Yesu akiwa Mufalme utageuza dunia hii kuwa paradiso. Atafufua watu waliokufa ili wafurahie maisha katika dunia hii itakayokuwa Paradiso.​—Soma Luka 23:42, 43.

Ili kupata habari zingine, soma ukurasa wa 73 mupaka ukurasa wa 85 wa kitabu hiki, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Unaweza kuchukua kitabu hiki kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine