Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w15 1/4 uku. 3-4
  • Sababu Gani Ujifunze Biblia?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Sababu Gani Ujifunze Biblia?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Sababu Gani Unapaswa Kupendezwa na Biblia?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Programu ya Kujifunza Biblia na Watu Wote
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Ungependa Kujua Kweli?
    Ungependa Kujua Kweli?
  • Bhayibele yi ko go Thušeng mo o ka fo yi Bala
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 1/4 uku. 3-4
Mwanaume mumoja anachunguza Biblia katika maktaba ya eneo lao

HABARI KUBWA | UNAPENDA KUJIFUNZA BIBLIA?

Sababu Gani Ujifunze Biblia?

  • Maisha iko na kusudi gani?

  • Sababu gani watu wanateseka na kufa?

  • Wakati unaokuja utakuwa namna gani?

  • Mungu ananihangaikia?

Umekwisha kujiuliza maulizo kama hayo? Ikiwa ni hivyo, hauko peke yako. Watu katika dunia yote wanafikiri sana juu ya maulizo ya maana kuhusu maisha. Unaweza kupata majibu?

Watu wengi sana wanaweza kujibia, “Ndiyo!” Sababu gani? Kwa sababu wamepata majibu yenye kusadikisha ya maulizo yao katika Biblia. Unapenda kujua mambo Biblia inasema? Ikiwa ni hivyo, utafurahi kufaidika na programu ya Mashahidi wa Yehova ya kufundisha watu Biblia bila kulipa.a

Wakati watu fulani wanaambiwa wajifunze Biblia wanasema hivi: “Sina wakati.” “Ni vigumu sana kujifunza Biblia.” “Ninaogopa kufanya mapatano na watu.” Lakini wengine wana mawazo tofauti. Wanakubali kujifunza mambo Biblia inafundisha. Ona tu mifano kidogo:

  • “Nilienda katika kanisa la Wakatoliki na la Waprotestanti, katika hekalu la Dini ya Sikh, na kwenye makao ya watawa wa dini ya Wabuda, na nilijifunza teolojia kwenye masomo ya juu. Lakini, maulizo yangu mengi juu ya Mungu hayakujibiwa. Kisha Shahidi mumoja wa Yehova alinitembelea nyumbani. Nilipendezwa sana na majibu yake yenye kutegemea Biblia, na nikakubali kujifunza Biblia.”—Gill, Uingereza.

  • “Nilikuwa na maulizo mengi juu ya maisha, lakini majibu ya walimu wa dini yangu hayakunisadikisha. Hata hivyo, Shahidi mumoja wa Yehova alijibia maulizo yangu kwa kutumia tu Biblia. Wakati aliniuliza ikiwa ninapenda kujifunza mengi zaidi, nilikubali kwa furaha.”—Koffi, Bénin.

  • “Nilipenda sana kujua ikiwa watu waliokufa wako katika hali gani. Niliamini kama watu waliokufa wanaweza kuwatendea vibaya watu walio wazima, lakini nilipenda kujua mambo Biblia inasema juu ya jambo hilo. Kwa hiyo, nilianza kujifunza Biblia na rafiki mumoja aliyekuwa Shahidi wa Yehova.”—José, Brazili.

  • “Nilijaribu kusoma Biblia lakini sikuweza kuielewa. Kisha Mashahidi wa Yehova walinitembelea na wakanifasiria waziwazi unabii mbalimbali wa Biblia. Nilipenda kujifunza mengi zaidi.”—Dennize, Meksiko.

  • “Nilikuwa ninajiuliza ikiwa Mungu ananihangaikia kabisa. Kwa hiyo, niliamua kusali kwa Mungu mwenye kuzungumuziwa katika Biblia. Siku iliyofuata Mashahidi wa Yehova waligonga kwenye mulango wangu, na nikakubali kujifunza Biblia.”—Anju, Népal.

Maelezo hayo yanatukumbusha maneno haya ya Yesu: “Wenye furaha ni wale wanaotambua uhitaji wao wa kiroho.” (Mathayo 5:3) Kwa kweli, wanadamu wanazaliwa wakiwa na uhitaji ao lazima ya kujua Mungu. Ni Mungu tu ndiye anaweza kututimizia lazima hiyo, na anafanya hivyo kupitia Neno lake, Biblia.

Sasa, funzo la Biblia linafanywa namna gani? Linaweza kukuletea faida gani? Maulizo hayo yatajibiwa katika habari yenye kufuata.

a Biblia inaonyesha kama jina la Mungu ni Yehova.

Maelezo Fulani Juu Ya Biblia

Biblia yenye kuwa wazi
  • JINA: Linatoka katika neno la Kigiriki bi·bliʹa, lenye kumaanisha “vitabu vidogo-vidogo”

  • VITABU VYENYE KUWA NDANI: Ina vitabu 39 vyenye viliandikwa katika luga ya Kiebrania (mistari fulani iliandikwa katika Kiaramu) na vitabu 27 vyenye viliandikwa katika Kigiriki

  • WAANDIKAJI: Iliandikwa na watu 40 hivi katika kipindi cha miaka 1600 hivi, kuanzia mwaka wa 1513 M.K.Y. mupaka mwaka wa 98 hivi K.K.Y.b

  • LUGA: Imetafsiriwa ikiwa nzima ao sehemu katika luga zaidi ya 2500

  • KUGAWANYWA: Inakadiriwa kuwa Biblia miliare 5 zimegawanywa, hilo linafanya Biblia ikuwe kitabu kinachogawanywa sana katika dunia

b Ufupisho M.K.Y. unamaanisha “Mbele ya Kuzaliwa kwa Yesu,” na ufupisho K.K.Y. unamaanisha “Kisha Kuzaliwa kwa Yesu.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine