Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w15 1/4 uku. 4-7
  • Programu ya Kujifunza Biblia na Watu Wote

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Programu ya Kujifunza Biblia na Watu Wote
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MAJIBU YA MAULIZO YENYE WATU WANAULIZA SANA JUU YA PROGRAMU YETU YA KUJIFUNZA NA WATU BIBLIA
  • Funzo la Biblia linaweza kufanywa wapi na wakati gani?
  • Tunaweza Kupata Wapi Majibu ya Maulizo ya Maana Sana Juu ya Maisha?
    Tunaweza Kupata Wapi Majibu ya Maulizo ya Maana Sana Juu ya Maisha?
  • Umefurahia mambo yenye umejifunza?
    Furahia Maisha Milele!—Anza Kujifunza Biblia
  • Sababu Gani Ujifunze Biblia?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Nini Njo Inaweza Kukusaidia Uendelee Kujifunza Biblia?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 1/4 uku. 4-7
Funzo la Biblia

HABARI KUBWA | UNAPENDA KUJIFUNZA BIBLIA?

Programu Ya Kujifunza Biblia Na Watu Wote

Mashahidi wa Yehova wanajulikana kwa sababu ya kazi yao ya kuhubiri waziwazi. Lakini unajua kama tuko pia na programu ya kujifunza Biblia na watu katika dunia yote?

Mwanaume mumoja anajifunza Biblia mahali anafanya kazi

Katika mwaka wa 2014, Mashahidi wa Yehova zaidi ya 8000000, katika inchi 240, waliongoza mafunzo ya Biblia karibu 9500000 kila mwezi.a Kwa kweli, hesabu ya watu wenye tunajifunza nao Biblia inapita hesabu ya wakaaji wa inchi moja-moja 140 hivi!

Ili kutimiza kazi hiyo ya kufundisha watu, Mashahidi wa Yehova wanachapisha kila mwaka karibu miliare moja na nusu ya Biblia, vitabu, magazeti, na vichapo vingine vya kusaidia watu kujifunza Biblia, katika luga 700 hivi! Kazi hiyo ya kuchapisha vichapo isiyoweza kulinganishwa inawezesha watu kujifunza Biblia katika luga yenye wanapenda.

“Sikukuwa ninapenda kujifunza kwenye masomo, lakini funzo hili lilikuwa lenye kufurahisha. Na mambo nilijifunza yalikuwa yenye kufariji sana!”—Katlego, Afrika Kusini.

“Funzo lilijibia maulizo yangu yote na maulizo mengine mengi.”—Bertha, Meksiko.

“Funzo la Biblia lilifanywa nyumbani kwangu kwa wakati nilipenda. Ningetaka kitu gani kingine!”—Eziquiel, Brazili.

“Wakati fulani funzo lilichukua dakika 15 mupaka 30, wakati mwingine lilipitisha dakika hizo, kulingana na programu yangu.”—Viniana, Australia.

“Nilijifunza bila kulipa—lilikuwa jambo la kushangaza!”—Aimé, Bénin.

“Mwalimu wangu wa Biblia alikuwa muvumilivu na mwema sana. Tulifikia kuwa marafiki wa sana.”—Karen, Irlande ya Kaskazini.

“Watu wengi wanajifunza Biblia bila kuwa Mashahidi wa Yehova.”—Denton, Uingereza.

MAJIBU YA MAULIZO YENYE WATU WANAULIZA SANA JUU YA PROGRAMU YETU YA KUJIFUNZA NA WATU BIBLIA

Funzo la Biblia linafanywa namna gani?

Tunachukua habari mbalimbali za Biblia na kisha tunachunguza maandiko yenye kuhusu habari hizo. Kwa mufano, Biblia inajibia maulizo kama haya: Mungu ni nani? Iko namna gani? Iko na jina? Anaishi wapi? Tunaweza kumukaribia? Haiko vyepesi kujua ni wapi tunaweza kutafuta majibu ya maulizo hayo katika Biblia.

Ili kusaidia watu wapate majibu ya maulizo hayo, kwa kawaida tunatumia kitabu chenye kurasa 224 kinachoitwa Biblia Inafundisha Kabisa Nini?b Kitabu hicho kilichapishwa ili kusaidia watu waelewe mafundisho ya musingi ya Biblia. Kinazungumuzia habari juu ya Mungu, Yesu Kristo, mateso ya wanadamu, ufufuo, sala, na habari zingine nyingi.

Funzo la Biblia linaweza kufanywa wapi na wakati gani?

Funzo la Biblia linaweza kufanywa mahali na wakati unapenda.

Funzo la Biblia linafanywa kwa muda gani?

Watu wengi wanapanga kujifunza Biblia kwa saa moja hivi kila juma. Lakini muda wa kujifunza unaweza kubadilika. Tutajifunza kwa muda unaopatana na programu yako. Watu fulani wanajifunza kwa dakika 10 ao 15 tu kila juma.

Inaomba kulipa feza ngapi ili kujifunza Biblia?

Hautalipa funzo na vichapo vya funzo. Hilo linapatana na agizo hili lenye Yesu alipatia wafuasi wake: ‘Mulipokea bure, mutoe bure.’—Mathayo 10:8.

Funzo la Biblia linachukua miezi ngapi?

Ni wewe utaamua ikiwa funzo litachukua miezi ngapi. Kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? kina sura 19. Unaweza kujifunza sura fulani ao sura zote kwa mwendo unaokufaa.

Nitalazimika kuwa Shahidi wa Yehova?

Hapana. Kwa sababu tunaheshimu watu, tunajua kama kila mutu iko na haki ya kuchagua mambo ataamini. Lakini, watu wenye wamejifunza mafundisho ya musingi ya Biblia wanaweza kuchukua uamuzi wenye kutegemea mambo yenye wamejifunza.

Ninaweza kupata wapi habari zaidi?

Adresi yetu ya Internete jw.org inatoa habari za kweli juu ya mambo yenye Mashahidi wa Yehova wanaamini na juu ya kazi zao.

Ninaweza kuomba funzo la Biblia namna gani?

  • Watu wenye kuomba funzo la Biblia kwa njia mbalimbali: kupitia Internete, barua, na kupitia liste ya namba za telephone katika eneo lao

    Uombe funzo kupitia Internete, kwenye adresi yetu www.jw.org.

  • Uandikie adresi yenye kuwa kwenye ukurasa wa pili wa gazeti hili.

a Kwa kawaida wanajifunza Biblia na mutu mumoja-mumoja ao na vikundi vidogo-vidogo vya watu.

b Kilichapishwa na Mashahidi wa Yehova. Vitabu zaidi ya milioni 230 vimechapishwa katika luga zaidi ya 260.

Funzo La Biblia Linasaidia Familia

Eziquiel

“Wakati bibi yangu alianza kujifunza Biblia, niliona kuwa alibadilika sana. Maisha ya familia yetu yakakuwa muzuri zaidi. Nilipenda sana kujua mambo alikuwa anajifunza, kwa hiyo nilianza pia kujifunza. Mambo nilijifunza yalinisaidia nikuwe mutu muzuri zaidi. Kujifunza Biblia kulifanya familia yetu ikuwe na umoja.”—Eziquiel.

Karen

“Kisha kuanza kujifunza Biblia, niliacha kutumia dawa za kulewesha, kunywa pombe kupita kiasi, na nilijifunza kuzuia hasira yangu. Nyumba yangu iko safi na yenye kupangwa muzuri. Ninapendezwa sana na watu wa familia yangu na ninapenda kufanya mambo ya kuwafurahisha. Mimi ni mwenye furaha sana.”—Karen.

Viniana

“Watu fulani walinisema mubaya kwa sababu nilikuwa ninajifunza Biblia. Lakini bwana yangu aliunga mukono uamuzi wangu, kwa kusema hivi: ‘Sihangaikie mambo watu wanasema. Jambo la maana kwangu ni kukuona unabadilika na kuwa mutu muzuri. Uendelee kujifunza.’ Maisha ya familia yetu yamekuwa muzuri sana!”—Viniana.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine