Tujiendeshe Kwa Namna Yenye Kustahili Ile Habari Njema
1 Tukiwa Mashahidi wa Yehova, tunatamani kuliheshimu jina la Yehova. Tunajua kwamba mwenendo wetu, usemi wetu, mvalio wetu na kunyolewa kwetu vinaweza kuwa na uvutano juu ya namna wengine wanavyoona ibada ya kweli. Hilo linaonekana hasa wakati wa mikutano yetu. Tunapaswa kuwa hakika kwamba yote yanayosemwa na kufanywa mikutanoni ni yenye kustahili habari njema na inamtukuza Yehova.—Flp. 2:4.
2 Mambo mengi ulimwengu unayopendelea kwa upande wa mavazi na kunyolewa hayakubaliki kwa Wakristo. Wahudumu wa habari njema wanapaswa kuangalia kwa makini swala hilo. Tungeweza kusoma yafuatayo katika Mnara wa Mlinzi wa Juni 1, 1989, ukurasa 20: “Nguo zetu hazihitaji kuwa za bei kubwa, lakini zinapasa kuwa safi, za kupendeza, na zenye kiasi. Viatu vyetu vinapasa kutengenezwa vyema katika sehemu vilikoharibika na viwe vyenye sura njema. Vivyo hivyo, kwenye mikutano yote, kutia na Funzo la Kitabu la Kundi, miili yetu inapasa kuwa safi, na tunapaswa kuwa maridadi na kuvalia ifaavyo.”
3 Kufika pa wakati kila mara ni wonyesho wa heshima na uangalifu unaochochewa na upendo. Inafikia kwamba mambo yasiyotazamiwa yanatuzuia kufika pa wakati kwenye mkutano. Lakini kufika nyuma kila mara kunaweza kuonyesha kwamba hatuheshimu hali ya utakatifu wa mikutano na kwamba tunazarau wajibu tulio nao wa kutosumbua wengine. Mara nyingi, wenye kufika nyuma wanapumbaza wahudhuriaji wengine na wanawazuia kutofaidika kabisa na mkutano. Kufika pa wakati kila mara kunashuhudia heshima yetu ya hisia na faida za wale wote waliopo.
4 Upendo wa jirani unapaswa kutuchochea kuangalia kutokuwa chanzo cha kupumbazisha wengine wakati wa mikutano. Kusema chini-chini, kula, kutafuna pipi, kufinyanga karatasi na kwenda na kurudi mara nyingi kusikofaa kwenye vyoo kunaweza kuwazuia wengine kukaza akili kikiki na kuzuru heshima inayostahili kwenye mahali pa ibada ya Yehova. Haifai mtu kushughulika na kazi ya kibinafsi ya kutaniko au kuzungumza na wengine isipokuwa kuna na hali ya haraka inayolazimisha ndugu watoke nafasi zao. Tofauti na hilo, wote wangepaswa kukaa na kusikiliza kwa faida yao na ya familia zao. Tabia mbaya za kukosa adabu hazina nafasi yazo katika Jumba la Ufalme, kwani “upendo . . . haujiendeshi bila adabu.”—1 Kor. 13:4, 5; Gal. 6:10, NW.
5 Jina la Yehova linasifiwa na kuheshimiwa pia kwa mwenendo mzuri wa watoto wetu wakati wa mikutano. Ni jambo la lazima kwamba wazazi wawe na jicho juu yao. Inafaa kutia watoto moyo kusikiliza na kushiriki. Wazazi wengi wanachagua nafasi ambapo wataweza kutoka kwa vyepesi ili kushughulika na watoto wao wachanga bila kusumbua wengine isivyofaa.
6 Paulo alitoa kipa-moyo kifuatacho: “Jiendesheni kwa namna yenye kustahiki ile habari njema.” (Flp. 1:27, NW) Kwa hiyo, tujikaze kuwa na adabu na heshima kwa wengine tunapohudhuria kwenye mikutano. Ushirikiano wa wote utatoa nafasi kwa “badilishano la kitia-moyo miongoni mwenu, kwa kila mmoja kupitia imani ya mwingine.”—Rum. 1:12, NW.