Tuonyeshe Heshima Kwa Mahali Pa Ibada Ya Yehova
1 Tunapoalikwa kwa mtu fulani, tunajionyesha wenye heshima kuelekea mali yake kwa kufanya kwamba tusiiharibu. Hatuvurugi pia tabia nzuri za nyumba. Je! hilo halingepaswa kuonekana hata zaidi tunapokuwa waalikwa wa Yehova? Tungepaswa kujua namna ya kujiendesha katika nyumba yake. (Zab. 15:1; 1 Tim. 3:15) Mikutano yetu ya Kikristo iwe yenye kufanyika katika Jumba la Ufalme, nyumba au jengo la watu wote, wengi zaidi kati yetu tunaonyesha sikuzote kwa ajili ya mahali petu pa ibada heshima inayostahili kwa nyumba ya Yehova, ambaye “utukufu wake ni juu ya nchi na mbingu.”—Zab. 148:13.
2 Ndugu fulani wanajionyesha kidogo wakati mwingine kuwa wasio na heshima wakati wa mikutano; ni wenye kufanya fujo au wanajiendesha kama kwamba habari inayotolewa haina mafaa. Watu wazima fulani huendelea na mazungumzo yasiyo na maana katika mlango wa kuingilia, katika sebule ya kupokelea wageni, katika vyoo au nje ya Jumba la Ufalme ingawa mikutano imekwisha kuanza. Wakati tunapoacha mtoto ashughulikie mwingine aliye mdogo zaidi, inafikia kwamba wote wawili wanaanza kucheza na hawafaidike tena na programu. Watoto walionwa wakicheza nje ya Jumba la Ufalme baada ya mkutano, wakifanya fujo kubwa na hata kupima kati yao kufanya mchezo wa kupigana karaté. Walisumbua wakati mwingine majirani na kuudhi ndugu katika jumba kwa kupanda juu ya jukwaa au kwa kukimbia-kimbia katikati ya viti na kusukuma-sukuma ndugu wazee-wazee.
3 Tusiwe Tena Wakosa-heshima: Ikiwa tunaelewa ubora na utakatifu wa ibada yetu, hatutataka bila shaka kukengeusha wahudhuriaji kwa kunongona-nongona (kusema chini-chini), kwa kula, kwa kutafuna peremende, kwa kukunja-kunja karatasi, kwa kuenda na kurudia kusiko na sababu kwenye choo au kwa kufika nyuma sikuzote kwenye mikutano. Wazazi wenye heshima na wenye shukrani wanakataza watoto wao kuchafua zulia (tapis), nguo yenye kufunika viti au kuta katika Jumba la Ufalme na nyumba mnamofanyika funzo la kitabu. Kwa upande mwingine, tunakubaliana sisi sote kwamba mwenendo wa aibu, maongezi ya kipumbavu na kufanya mizaha ya maneno machafu, iwe ya namna gani, haina nafasi hata kidogo katika mikutano yetu.—Efe. 5:4.
4 Ikiwa sikuzote tuna kusudi la mikutano yetu ya Kikristo akilini, watoto wetu na sisi wenyewe tutaonyesha bila shaka heshima inayofaa kuelekea ibada ya Yehova, mahali ambapo sisi ‘tumechagua kusimama.’—Zab. 84:10.