Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 10/96 uku. 3-6
  • Tuhubiri Habari Njema Mahali Pote

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tuhubiri Habari Njema Mahali Pote
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jinsi ya Kuhubiri Katika Eneo la Biashara
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Unaweza Kutoa Ushahidi Wakati Haukupanga Kufanya hivyo!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Jinsi ya Kuhubiri kwa Matokeo Barabarani
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Njia Mbalimbali za Kuhubiri Habari Njema
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 10/96 uku. 3-6

Tuhubiri Habari Njema Mahali Pote

1 Wakristo wa kwanza walihubiri habari njema mahali pote. Juhudi yao ilikuwa kubwa hivi kwamba miaka 30 kisha ufufuo wa Yesu Kristo, ujumbe wa Ufalme ulihubiriwa “katika kuumbwa kote chini ya mbingu.”​—Kol. 1:​23, NW.

2 Leo, watumishi wenye juhudi wa Yehova wanafuatia mradi uleule: kujulisha habari njema ya Ufalme kwa hesabu kubwa zaidi ya watu iwezekanavyo. Ni nini kinachoweza kutusaidia kufikia kusudi hilo? Watu zaidi na zaidi wanatumika kwa wakati wote na mara nyingi hawapatikani makwao tunapokuja kuwaona. Wanapokuwa hawatumiki, wanakwenda kujitembeza, kununua au wanajiburudisha. Namna gani kutangaza ujumbe wa Ufalme kwa wale wanaostahili kati yao?​—Mt. 10:11.

3 Wamoja wanaweza kutembelewa nafasi zao za kazi. Hata katika miji midogo, tunakuta maeneo ya shughuli ndani yayo watu wengi wanapitisha sehemu kubwa ya mchana wao. Katika miji mikubwa, watu wanaotumika katika maeneo ya viwanda au katika majengo makubwa za maofisi, na pia wale wanaoishi katika majengo ambayo kuingia ndani kunalindwa sana, wanapokea ushuhuda, wengi kwa mara ya kwanza. Mwisho wa juma, kati ya wale wanaotembelewa huku wakijiburudisha katika bustani ya watu wote, uwanja wa tafrija, kampingi au katika nyumba zao za mashambani, au kati ya wale wanaongoja magari au katika mtaa wa kibiashara, wamoja-wamoja wanapokea vizuri habari njema.

4 Hesabu kubwa ya wahubiri siku zote hufanya bidii ya pekee ili kutoa ushuhuda katika mahali pa watu wote, pale ambapo watu hupatikana. Kwanza kabisa, Mashahidi hao walikuwa wenye kusita-sita na wakati mwingine wenye woga, waliokuwa na zoezi ya kuhubiri kwa namna ya kawaida zaidi, nyumba kwa nyumba kwa mfano. Jinsi gani wanaitikia kwa sasa?

5 “Huduma yangu ilitiwa nguvu mpya!” alisema ndugu mmoja mwenye ujuzi. Mwingine aliongeza: “Hilo huniwezesha kubaki mwenye kukaza akili juu ya utendaji.” Painia mmoja mzee-mzee alitoa wazo hili: “Hilo liliniburudisha kiakili, kimwili na kiroho, . . . na ninasonga mbele katika kufanya maendeleo!” Mhubiri mmoja anaona kwamba anahubiri watu wengi ambao walikuwa bado hawajazungumza na Mashahidi wa Yehova hapo mbele. Vijana pia wanafurahi kushiriki katika utendaji huo wenye kufurahisha. Mmoja wao anasema hivi: “Ni jambo nzuri sana kwani ninafikia kuzungumza na watu wengi.” Mwingine anasema: “Sijaacha kamwe vitabu vingi kama hivi!” Ni maneno yanayoripotiwa kutoka katika eneo ambalo linatembelewa sana kila mara.

6 Wangalizi Wasafiri Katika Mstari wa Kwanza: Ikitambua kwamba “tamasha ya ulimwengu huu inabadilika,” Sosaiti iliomba hivi karibuni kwa wangalizi wasafiri wabadili programu yao ya kuhubiri kila juma ili kuweza kutangaza habari njema ya Ufalme kwa watu wengi zaidi iwezekanavyo. (1 Kor. 7:31) Tangu miaka mingi, wangalizi wa mzungumko wanachunga saa zao za asubuhi kwa ajili ya mahubiri ya nyumba kwa nyumba na kisha-mchana kwa ziara za kurudia na kwa mafunzo ya Biblia. Inawezekana kwamba programu hiyo iwe siku zote yenye kufaa katika maeneo fulani. Katika yale mengine, hatufanyi jambo kubwa ili kuhubiri nyumba kwa nyumba wakati wa saa fulani za asubuhi. Ikiwa ndivyo, ni mwangalizi wa mzunguko ataona labda kuwa jambo nzuri kushiriki asubuhi katika utendaji wa duka kwa duka au katika ushuhuda wa barabarani. Anaweza tena kuchukua mipango ili vikundi vidogo vitoe ushuhuda katika majengo makubwa ya afisi, mitaa ya kibiashara, nafasi za kuegeshea magari au nafasi nyingine za watu wote. Ikiwa wahubiri wanafanya matumizi mazuri ya wakati wanaotumia katika mahubiri, watu wengi wataweza kuhubiriwa.

7  Ripoti zinaonyesha kwamba marekebisho yalipokewa vizuri na wangalizi wasafiri na wahubiri pia. Mabaraza ya wazee yaliomba mwangalizi wa mzunguko kutoa mazoezi kwa wahubiri fulani fulani katika sehemu mbalimbali za utendaji ambazo zinastahili kuangaliwa mahali penu. Ni jambo lenye manufaa kwa wahubiri hao kushindikiza mwangalizi msafiri katika utendaji huo. Hata hivyo, wanaweza kwa upande wao kuzoeza wengine. (2 Tim. 2:2) Hivyo, watu wengi zaidi wanasikiliza leo kutangazwa kwa habari njema.

8 Ni wazi kwamba hamna lazima ya kungoja ziara ya mwangalizi wa mzunguko ili kujaribu mojawapo ya namna hizo nyingine za kuhubiri. Angalieni mawazo fulani ambayo mtaamua labda kuwa yenye manufaa katika eneo lenu:

9 Ushuhuda Katika Barabara: ‘Watu wako wapi?’ tunajiuliza wakati mwingine tunapohubiri katika mtaa munamoishi watu lakini ambamo watu hawapatikani asubuhi katika juma. Inawezekana kukutana na wamoja wakati wanapotoka katika shughuli zao. Je! umekwisha kujaribu kuwaona kwa kutoa ushuhuda barabarini? Aina hiyo ya huduma inaweza kuwa yenye kuzaa matunda tunapoifanya kwa namna iliyo nzuri. Badala ya kubaki nafasi ileile moja na magazeti mikononi, ni vizuri kuwafikia watu na kuanzisha mazungumzo ya kirafiki. Si lazima kutoa ushuhuda kwa wapita-njia wote. Zungumza na wale wasio haraka, wale wanaoangalia-angalia vitu kupitia vioo, walio ndani ya magari yao yanayosimamishwa au wanaongoja usafirishaji wa watu wote, kwa mfano. Inaomba kuanza kumsalimu mtu kwa urafiki na kungoja kuitikia kwake. Ikiwa yeye ni tayari kuzungumza, tumwuulize maoni yake juu ya habari inayoweza kumpendeza.

10 Wakati wa ziara katika kutaniko moja, mwangalizi msafiri alialika wahubiri sita kujiunga naye na mke wake ili kutoa ushuhuda barabarani. Matokeo yalikuwa nini? “Tulipitisha asubuhi nzuri sana! anasema. Hapakuwa na watu wasiokuwako. Tuliacha magazeti 80 na pia trakti nyingi. Tulifanya mazungumzo mengi yenye kusisimua. Mhubiri mmoja, ambaye alihubiri barabarani kwa mara ya kwanza, alisema: ‘Niko katika ukweli tangu miaka na sikuwa nawazia pembeni ya nini nilikuwa nikipita!’ Mwishoni mwa juma, magazeti yote ya ziada ambayo kutaniko ilikuwa nayo yaliangushwa.”

11 Alipokwenda katika kutaniko lifuatalo, mwangalizi msafiri uleule alipata habari kwamba wahubiri fulani walitoa ushuhuda barabarani asubuhi moja mapema, lakini hawakupata matokeo mazuri mengi. Dada mmoja alizungumza tu na watu wawili muda wa mahubiri yake, kwani wengine wote aliokutana nao walikuwa haraka kwenda kazini. Mwangalizi msafiri alishauri kwa kila mmoja kurudi katika barabara ileile nyuma kidogo asubuhi. Ni yale waliyofanya, na walibaki huko mpka saa sita. Dada ambaye aliweza kuzungumza tu na watu wawili mwanzoni mwa asubuhi alifanya kazi nzuri zaidi safari ya pili. Aliacha magazeti 31 na broshua 15, alipata jina na anwani ya watu saba na alianzisha mafunzo mawili ya Biblia! Wahubiri wengine wa kikundi hicho walipata pia matokeo yenye kutia moyo.

12 Unapokutana na mtu anayeonyesha kupendezwa, jikaze kupata jina lake, anwani yake na namba yake ya simu. Badala ya kuomba habari zote hizo ghafula, unaweza kusema: “Nilithamini sana mazungumzo haya. Je! ingewezekana kuyaendeleza kwa wakati mwingine? Au muulize: “Je! inawezekana kukutembelea kwako?” Katika njia hiyo, watu wengi wanakubali kutembelewa upya. Hakikisha kwamba una hesabu ya kutosha ya karatasi ya mwaliko kwa wale ambao wangependelea kuhudhuria kwenye mikutano.

13 Ikiwa unasema na mtu anayeonyesha kupendezwa lakini anayekaa katika eneo la kutaniko lingine, fuatisha maelezo ili kwamba ndugu wanaohusika waweze kukomaza kupendezwa. Je! ushuhuda barabarani ungewezesha kutawanya kwa matokeo habari njema katika eneo lenu? Ikiwa ndivyo, mpange mambo ili kushiriki katika ushuhuda wa barabarani kwa saa inayofaa na itakayowawezesha kugusa hesabu ya watu zaidi iwezekanavyo.

14 Ushuhuda Katika Usafirishaji wa Watu Wote: Asubuhi moja, mapainia waliamua kutoa ushuhuda kwa watu waliokuwa wakingoja basi karibu na shule moja. Walikuwa na mazungumzo mazuri, lakini tatizo moja lilijitokeza kwao. Wakati mazungumzo yalipokuwa yakiendelea, basi ilifika, jambo ambalo lilikuwa likikatiza kwa ghafula mazungumzo. Mapainia walitatua tatizo hilo kwa kupanda ndani ya basi ili kuendelea kutoa ushuhuda kwa wasafiri, huku wakienda huku na huku mjini. Walipofika kwenye kituo cha basi, mapainia walifanya safari ya kurudi huku wakiendelea kutoa ushuhuda. Baada ya safari nyingi za kwenda na kurudi, walifanya ripoti juu ya matokeo waliyopata: waliacha magazeti zaidi ya 200 na kuanzisha mafunzo ya Biblia sita! Wasafiri fulani walikubali kutoa anwani zao na namba zao za simu ili kutembelewa makwao. Juma lifuatalo, mapainia walirudi kwenye kituo cha basi na walifanya vivyo hivyo. Waliacha magazeti 164 na walianzisha funzo lipya la Biblia! Kwenye kituo kimoja, msafiri mmoja alipanda ndani ya basi na alikaa katika nafasi moja tu iliyokuwa inabaki: pembeni ya painia. Alimwangalia ndugu na akamwambia kwa kicheko: “Ninajua, una Mnara wa Mlinzi kwa ajili yangu!”

15 Wahubiri wengi wanatoa ushuhuda kwa matokeo wanapotembea katika basi, katika treni au katika ndege. Jinsi gani tunaweza kuanzisha mazungumzo pamoja na jirani? Mhubiri mmoja wa miaka 12 alianza tu usomaji wa Amkeni! katika basi, akitumaini kuamsha udadisi (kupendezwa) kwa msichana mmoja aliyekaa pembeni yake. Ndilo jambo liliweza kutokea! Msichana huyo alimuuliza kile alichokuwa akisoma, na alimjibu kwamba ilikuwa ni makala juu ya suluhisho kwa matatizo ambayo vijana wanapaswa kupambana nayo. Aliongeza kwamba makala hiyo ilimsaidia sana na kwamba yeye pia angeweza kufaidika nayo. Alikubali magazeti kwa shangwe. Mazungumzo yao yalisikilizwa na vijana wengine wawili ambao wao pia waliomba nakala za magazeti. Kufikia hapo, kiongozi wa basi alisimamisha basi pembeni ya barabara na kuuliza ni kitu gani cha kupendeza ambacho magazeti hayo yalikuwa nayo. Baada ya kuelewa, yeye pia aliyakubali. Bila shaka, yote hayo hayangeweza kutokea ikiwa kijana huyo mhubiri hakuwa na magazeti ya kutosha ya kutolea kwa wale wote walioonyesha kupendewa!

16 Ushuhuda Katika Mabustani ya Watu Wote na Katika Vituo vya Magari: Hali inapokuwa nzuri, ushuhuda katika mabustani ya watu wote na vituo vya magari ni njia nzuri sana kugusa watu. Je! umekwisha kujaribu kutoa ushuhuda kwenye kituo cha magari cha mtaa wa kibiashara? Unapofika kwenye kituo cha magari, chunguza kwa muda fulani kando-kando yako. Tafuta mtu ambaye si haraka au anayengoja katika motokaa inayosimama na jaribu kuanzisha mazungumzo ya kirafiki. Ikiwa mazungumzo yanaendelea, toa ujumbe wa Ufalme. Jikaze kuwa peke yako huku ukiwa karibu na mhubiri mwingine. Epuka kuwa na mfuko wenye kujaa mno au kuvutia uangalifu kwa namna moja au nyingine juu ya utendaji wako. Uwe mwenye kiasi. Inaweza kuwa vizuri kutobaki muda mrefu kwenye kituo cha magari na kwenda kwenye kingine. Ikiwa mtu hapendi kuzungumza nawe, umwache kwa adabu na jaribu kuzungumza na mwingine. Kwa kufanya hivyo, ndugu mmoja aliacha magazeti 90 mnamo mwezi mmoja kwa kutoa ushuhuda kwenye vituo vya magari!

17  Kuna watu wanaokwenda katika mabustani ili kupumzika, kujifurahisha au kupitisha wakati pamoja na watoto wao. Bila kuvuruga sana utendaji wao mbalimbali, tafuta uwezekano wa kutoa ushuhuda. Ndugu mmoja alianza kuzungumza na mchungaji wa bustani ya watu wote na alitambua kwamba mtu huyo alikuwa akihofia dawa za kulevya na kuhusu wakati ujao wa watoto wake. Funzo la Biblia lilianzishwa, na liliongozwa kikawaida katika bustani.

18 Ushuhuda wa Vivi Hivi Katika Mitaa ya Kibiashara: Ijapokuwa haiwezekani siku zote kuhubiri duka kwa duka kwa kufuata programu iliyopangwa katika mitaa ya kibiashara kwa sababu ya vizuizi vya mahali, wahubiri wengine wanatokeza nafasi za kutoa ushuhuda wa vivi hivi. Wanakaa kwenye mbao ya kukalia na wanaanzisha mazungumzo ya kirafiki pamoja na wale wanaosimama ili kupumzika. Wakati watu wanapoonyesha kupendezwa, wanawatolea kwa busara trakti au gazeti na wanajikaza kuchukua mipango ili kuwaona tena. Baada ya kupitisha dakika fulani kwa kutoa ushuhuda katika sehemu ya mtaa wa kibiashara, wanakwenda mahali pengine na wanazungumza na mtu mwingine. Ni wazi kwamba inafaa kuwa wangalifu ili kutovutia uangalifu wakati tunapotoa ushuhuda wa vivi hivi kwa namna hiyo.

19 Unapomsalimu mtu, anza kuzungumza kwa kirafi. Ikiwa msikilizaji wako anashiriki katika mazungumzo, muulize ulizo moja na msikilize kwa makini wakati anaposema. Pendezwa kibinafsi na yale anayosema. Umwonyeshe kwamba unapendezwa na wazo lake. Ikiwezekana, sema kwamba unakubaliana naye.

20 Dada mmoja aliweza kuzungumza kwa namna yenye kupendeza na mwanamke mmoja mzee-mzee kwa kusema kwamba hali ya maisha inakuwa ghali. Papo hapo mwanamke huyo akajibu, jambo ambalo liliwezesha mazungumzo yenye shauku. Dada aliweza kupata jina na anwani ya mwanamke huyo na alirudi kumwona katika juma hilo.

21 Mahubiri ya Duka kwa Duka: Eneo la makutaniko fulani linatia ndani mitaa yote ya maduka. Ndugu anayeshughulika na maeneo angeweza kutayarisha kadi kwa ajili ya maeneo hayo tu yenye shughuli nyingi za kibiashara. Itaonyeshwa waziwazi kwenye maeneo yote yanayotia ndani mitaa hiyo kwamba wafanya-biashara wanatembelewa kibinafsi. Katika maeneo mengine, nyumba za biashara zinaweza kutembelewa wakati uleule wa kutembelea nyumba za wakaaji. Wazee wanaweza kualika wahubiri wenye ujuzi kutembelea kikawaida maeneo ya kibiashara ili kwamba mahubiri ya duka kwa duka yasiweze kuachwa kando.

22 Ikiwa wanakuomba kushiriki katika utendaji huo kwa mara ya kwanza, njia nzuri ya ‘kuwa mwenye uhodari’ ni wewe kwenda kwanza katika maduka madogo-madogo; kisha, utakapokuwa mwenye starehe zaidi, endeleza utendaji wako katika yale yaliyo makubwa zaidi. (1 Thes. 2:2) Unapohubiri duka kwa duka, vaa kama vile mwenye kwenda kuhudhuria mkutano kwenye Jumba la Ufalme. Ikiwezekana, ingia ndani ya duka wakati hakuna mtu wa kununua anayengoja ahudumiwe. Omba kuzungumza na mkurugenzi (kiongozi) au msimamizi. Uwe mwenye shauku, na hasa zungumza kwa kifupi. Si lazima kuomba radhi. Wafanya-biashara wengi wako pale kwa kuhudumia watu wanaokuja kununua na wako tayari kukatizwa.

23 Baada ya Kumsalimu Mfanya-Biashara, Unaweza Kusema: “Wafanya-biashara wana matumizi ya wakati yenye kujaa sana hivi kwamba inakuwa vigumu kuwakuta nyumbani kwao; ni kwa sababu hiyo tunawatembelea kwenye nafasi zenu za kazi ili kuwatolea usomaji wa makala moja yenye kuchochea kufikiri.” Toa elezo moja au mawili kuhusu magazeti ya mwisho-mwisho.

24 Ikiwa Unazungumza na Mkurugenzi, Unaweza Pia Kujaribu Kusema: “Tuliona kwamba wafanya-biashara wanapenda sana kujua habari zinazopita. Namba ya mwisho ya Mnara wa Mlinzi (au ya Amkeni!) ina makala inayohusu kila mmoja wetu.” Fasiria inahusu nini na malizia kwa kusema: “Tupo hakika kwamba utathamini usomaji wayo.”

25 Ikiwa Kuna Wafanya-Kazi na Kwamba Hilo Linaonekana Kuwa Lenye Kufaa, Unaweza Kuongeza: “Je! utakubali pia nilitolee kwa kifupi kwa wafanya-kazi wako?” Ikiwa wanakukubalia hilo, usisau kwamba uliahidi kufanya hivyo kwa kifupi, na mkurugenzi atatazamia kwamba uheshima yale uliyosema. Ikiwa wafanya-kazi wanapenda kuzungumza kwa urefu zaidi, ni vizuri kwamba uenende kuwaona nyumbani kwao.

26 Hivi karibuni, katika mji moja mdogo, wahubiri walikubali kushindikiza mwangalizi wa mzunguko katika utendaji wa duka kwa duka. Mwanzoni, wamoja walikuwa wakiona woga, kwani walikuwa bado hawajaushiriki kamwe mwanzoni; lakini haraka walijisikia wenye starehe na walipendezwa na utendaji huo. Kwa muda unaopungua saa moja, walizungumza na watu 37 na waliacha magazeti 24 na broshua 4. Ndugu mmoja alionyesha kwamba kwa wakati wa kawaida haiwezikani kukutana na watu wengi hivyo mlango kwa mlango mnamo mwezi alimofanya hivyo katika duka kwa duka kwa wakati mdogo sana.

27  Tutokeze Nafasi za Kuhubiri: Yesu hakushikilia tu mahubiri ya vivi hivi. Alitawanya habari njema kila mara hilo lilipofaa. (Mt. 9:9; Lk. 19:​1-10; Yn. 4:​6-15) Angalia jinsi gani wahubiri wanatokeza nafasi za kuhubiri.

28 Wamoja wanazoea kutoa ushuhuda kwa wazazi wanaongoja watoto wao kutoka shuleni. Kwa kuwa wazazi wamoja wanakuwa pale kwa dakika yapata 20 mbele ya wakati, wana wakati wa kuanzisha mazungumzo yenye kutia moyo juu ya habari fulani ya Biblia.

29 Mapainia wengi wanajikaza kuwagusa watu wanaohusika hasa na habari fulani zinazotolewa katika magazeti yetu. Kwa mfano, dada mmoja alipata matokeo mazuri kwa kutembelea shule sita zilizo katika eneo la kutaniko lao ili kuwatolea makala mfululizo yenye kichwa: “Shule Matatani,” iliyotokea katika Amkeni! ya Desemba 22, 1995. Alikwenda pia katika huduma za msaada wa kijamii pamoja na magazeti juu ya maisha ya familia na juu ya jeuri dhidi ya watoto, na aliruhusiwa kurudi na namba nyingine ambazo zingezungumzia habari za namna hiyo. Anasema kwamba ni kwa “pekee” kuitikia alikoona katika afisi ya kazi kuhusiana na Amkeni! ya Machi 8, 1996 kuhusu ukosefu wa kazi.

30 Mwangalizi wa wilaya mmoja anaripoti kwamba anatoa mara nyingi ushuhuda wa vivi hivi pamoja na mke wake wanapokwenda kununua vitu dukani. Wanachagua saa moja ambayo duka halina watu wengi na wakati watu wanaonunua wanapotembea-tembea katika duka kwa hatua yenye starehe. Wanakuwa hivyo na mazungumzo mengi yenye kupendeza.

31 Wahubiri wengi wanapata matokeo mazuri kwa kutoa ushuhuda katika nyumba za kusafishia mavazi kwa mashini. Hawaridhiki tu kuacha magazeti mtu anapokuwa hayupo. Kusudi lao ni kutangaza habari njema kwa watu; wanajikaza hivyo kusema kibinafsi pamoja na watu wanaokuja kusafisha mavazi yao katika mashini.

32 Katika mahali fulani fulani, wahubiri wanaochaguliwa wanaruhusiwa kutoa ushuhuda katika viwanja vya ndege. Wakati mwingine walipata shangwe ya kuhubiri watu wanaosafiri ulimwenguni na wanaoishi katika nchi ambamo hakuna Mashahidi wa Yehova wengi. Wakati watu hao wanapoonyesha kupendezwa, wanawaachia trakti au magazeti.

33 Ikiwa haiwezikani, kwenye eneo la kutaniko, kutoa ushuhuda kwa wakaaji wanaokaa katika majengo ambayo kuingia ndani kunalindwa sana, wahubiri fulani walichukua zoezi la kuhubiri kwa busara wachungaji wanaofanya kazi au wakurugenzi walio ndani ya maofisi yao. Wanafanya vivyo hivyo katika majengo ya watu binafsi au yanayolindwa. Mwangalizi wa mzunguko mmoja alifuata ufundi huo na wahubiri fulani katika majengo saba. Kwa kila kipindi, walifasiria mkurugenzi kwamba hawakuruhusiwa kuona wapangaji kama wanavyofanya kikawaida, hawakupenda hata hivyo kuwakosesha habari zilizomo katika namba za mwisho za magazeti yetu. Wakurugenzi wa majengo saba walikubali kwa shangwe magazeti na waliomba pia kupata namba zifuatazo!

34 Tujikaze Kuhubiri Mahali Pote: Ili kuishi kulingana na wakfu wetu kwa Mungu, imetupasa kutambua kwamba mahubiri ya ujumbe wa Ufalme ambayo tulikabiziwa ni ya haraka. Ikiwa tunataka kuwaona watu kwa wakati unaofaa kwao, tunapaswa kutia pembeni mapendezi yetu “ili kwa vyovyote kuokoa wengine.” Watumishi wote wa Yehova waliojitoa wakfu na kubatizwa wanatamani kurudilia maneno ya Paulo, aliyesema: “Nafanya mambo yote kwa ajili ya habari njema, ili nipate kuwa mshiriki wayo pamoja na wengine.”—1 Kor. 9:22, 23, NW.

35 Paulo aliandika baadaye: “Kwa mteremo zaidi sana afadhali nijisifu kwa habari ya udhaifu wangu mwingi, ili nguvu ya Kristo ipate kama hema kubaki juu yangu. . . . Kwa maana niwapo dhaifu, ndipo niwapo mwenye nguvu nyingi.” (2 Kor. 12:​9, 10, NW) Kwa maneno mengine, hakuna mmoja kati yetu anayeweza kutimiza kazi hii kwa nguvu zake mwenyewe. Imetupasa kumwomba Yehova ili kufaidika na nguvu ya roho takatifu yake. Ikiwa tunamwomba Mungu nguvu, tunaweza kuwa hakika kwamba atajibu sala zetu. Upendo wetu kwa watu utatusukuma hivyo kutafuta uwezekano mbalimbali wa kuwahubiri habari njema mahali walipo. Mnamo juma lijalo, kwa nini kutojaribu moja kati ya madokezo yanayopendekezwa katika nyongeza hii?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine