‘Tujionyeshe Wenye Shukrani’
1 Tulipokuwa watoto, wengi wetu tulijifunza kusema “tafadhali” na “asante” wakati mtu fulani alipotuonyesha wema na upole. Paulo anatuhimiza sikuzote ‘tujionyeshe wenye shukrani,’ na tungepaswa kuwa na shukrani hasa kwa Yehova. (Kol. 3:15, 16) Lakini jinsi gani tunaweza kuonyesha shukrani yetu kwa Muumba wetu Mkuu? Ni sababu gani hasa tulizo nazo za kuwa wenye shukrani kwake?
2 Mtume Paulo aliandika: “Shukrani kwa Mungu, kwa maana yeye hutupa sisi ushindi kupitia Bwana wetu Yesu Kristo!” (1 Kor. 15:57, TUM) Kila mwaka, wakati wa Ukumbusho, tunakumbuka upendo usio na mipaka ambao Mungu na Kristo walituonyesha kwa kutoa dhabihu ya ukombozi inayotuwezesha kutumainia wakati ujao wa milele. (Yn. 3:16) Wengi wetu tulipotelewa na mpendwa wetu, pia sisi ni wenye shukrani sana kwa ajili ya ufufuo ambao Yesu aliahidi. Moyo wetu unafurika kwa shukrani wakati tunapotafakari juu ya tazamio la kuokoka mwisho wa mfumo huu, bila kuonja kifo kamwe. (Yn. 11:25, 26) Ni vigumu kupata maneno ili kuonyesha shukrani yetu kwa ajili ya baraka za ajabu ambazo tutapokea kutoka mkono wa Yehova, katika Paradiso ijayo. (Ufu. 21:4) Ni sababu gani bora kabisa tungeweza kuwa nazo za ‘kujionyesha wenye shukrani’ kwa Mungu?
3 Jinsi ya Kuonyesha Shukrani Yetu kwa Mungu: Ni jambo lenye kustahili hakika kumshukuru Yehova katika sala kwa ajili ya wema wake. (Zab. 136:1-3) Tunajisikia pia kuwa wenye kusukumwa kuonyesha shukrani yetu kwake kwa namna nyingine tena. Ni kwa furaha kwamba ‘tunamheshimu Yehova na vitu vyetu vya thamani’ ili kutegemeza kimwili kutaniko letu na kazi ya ulimwenguni pote. (Mez. 3:9) Tunategemeza kabisa kabisa wazee na tunashirikiana nao, tukionyesha hivyo shukrani yetu kwa Yehova kwa ajili ya msaada anaotutolea kwa njia yao. (1 Thes. 5:12, 13) Kila siku, tunajikaza kuwa na mwenendo wenye kunyoka unaolitukuza jina la Mungu. (1 Pt. 2:12) Shuhuda zote hizo zenye shukrani zinamfurahisha Yehova.—1 Thes. 5:18.
4 Wonyesho Wetu Bora Zaidi wa Shukrani: Kushiriki kwa nafsi yetu yote katika mahubiri ya Ufalme, kuheshimu jina la Yehova, kuonyesha shukrani yetu katika sala, kuutetea kiaminifu ukweli, mambo yote hayo yanapatikana kati ya wonyesho mbalimbali ulio bora zaidi wa shukrani kutoka moyoni ambayo tunaweza kutoa kwa Muumba wetu kwa yote aliyofanya kwa ajili yetu. Yehova anataka kwamba “watu wa namna zote waokolewe” na anafurahi kutuona tukimtolea utumishi mtakatifu unaowezesha utimizo wa mapenzi yake. (1 Tim. 2:3, 4) Ni kwa sababu hiyo wahubiri wengi walio na uwezekano wanajibu kwa mwaliko unaotolewa katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Machi kwa kuwa mapainia wasaidizi muda wa mwezi mmoja au mingi mnamo Mei na Juni. Njia bora kabisa ya sisi ‘kujionyesha wenye shukrani’ kwa Mungu ni kujitoa zaidi katika huduma. Je! sisi tutakuwa mapainia mnamo Mei na Juni?
5 Tulipokea tumaini hakika la kuishi milele. Kwa kuliona karibu na utimizo walo, tunazo sababu zaidi tena za kuendelea kila siku kumshukuru Yehova kwa shangwe.—Zab. 79:13.