Tusaidie Wengine Wapate Faraja
1 Watu wengi wamechoka kusikia kila mara habari za misiba, vita, mauaji na mateso. Faraja, ingawa hukosekana katika taarifa za habari, ni jambo ambalo wanadamu wanahitaji sana. Kumwimarisha mtu, au kumfariji, kunamaanisha kumtia nguvu na kumtolea sababu za kutumaini, kumsaidia kuvumilia jaribu fulani. Mashahidi wa Yehova ni wenye kuvalia vifaa vya kazi ili kutolea msaada kama huo. (2 Kor. 1:3, 4) Broshua zetu zenye kutegemea Biblia, ambazo tutatolea mnamo Agosti na Septemba, zina ujumbe mbalimbali wa kweli na wa faraja. (Rom. 15:4) Haya ni madokezo fulani yatakayotusaidia kuzitolea katika hali mbalimbali:
2 Jambo tofauti lenye kuogofya linaweza kututolea nafasi ya kutoa ushuhuda na kuimarisha mtu mwingine kwa maneno ya aina ifuatayo:
◼ “Wakati mambo kama hayo yanapotokea, wamoja wanajiuliza ikiwa kwelikweli Mungu yuko, na ikiwa ndiyo, ikiwa anatujali. Unafikiri nini? [Tuache mtu ajibu.] Mojawapo ya namna ya kujua ikiwa kuna Mungu ni kutumikisha kanuni inayojulikana vizuri.” Tusome Waebrania 3:4. Tuonyeshe mambo mengine yanayotuzunguka na ambayo kwa vyovyote yaliumbwa. Kisha tuendelee: “Nina broshua moja ambayo bila shaka utaiona kuwa yenye kuimarisha. Ni yenye kichwa cha habari Je! Kweli Mungu Anatujali? [Tusome maulizo ya jalada.] Inatoa ushuhuda mbalimbali wenye kuthibitika, si tu kwamba Mungu yuko, lakini pia kwamba atakomesha hivi karibuni hali zote zisizo za haki tunazopata leo. Je! ungependa kuisoma?” Tuagane baadaye kwa ajili ya ziara ya kurudia.
3 Wakati wa ziara ya kurudia, tungeweza kusema:
◼ “Tulizungumza juu ya ushuhuda wa kuwako kwa Mungu na nilikuachia broshua Je! Kweli Mungu Anatujali? Uliona labda wazo hilo kwenye ukurasa 7. [Tuonyeshe picha na tufanye muhtasari wa fungu 15.] Huo ni mfano tu kati ya mifano mingine ili kuonyesha kwamba hakika kuna Mungu anayetujali. [Tusome fungu 27 la ukurasa 9.] Funzo la kibinafsi la Biblia linaniwezesha kupambana na matatizo ya maisha ya kila siku kwa kuwa linatoa maoni ya Mungu juu ya mambo.” Tumpendekeze mtu kumuonyesha jinsi ya kujifunza.
4 Mahubiri kwa njia ya simu kwa msaada wa broshua “Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai? Wewe Waweza Kulipataje?” Tungeweza kujijulisha na kusema:
◼ “Ninakuita kwa ajili ya ujumbe wa maana kwa sababu siwezi kukutembelea kibinafsi.” Tusome fungu la kwanza la ukurasa wa 4 wa broshua, kwa sauti ya kawaida, kana kwamba tulikuwa mbele ya mtu. Tumuulize maoni yake na tumwache ajibu. “Nina Biblia yangu wazi kwenye Isaya 45:18. Andiko hilo linaonyesha kwamba dunia iliumbwa kwa ajili yetu. Je! ninaweza kukusomea lenyewe?” Kisha, tufasirie kusudi la broshua hiyo na tuulize ikiwa tunaweza kumletea nakala moja.
5 Wakati wa kuita kunakofuata kwenye simu, tungeweza kujaribu ufundi huu ili kuanzisha funzo:
◼ “Ningependa kuendeleza mazungumzo yetu ya nyuma kwa mfano moja unaoonyesha kwa nani inafaa kutafuta majibu juu ya kusudi la uhai. [Tueleze mafungu 1 na 2 ya ukurasa 6 wa broshua Kusudi la Uhai.] Ufunuo 4:11 linafasiria kwamba Yehova Mungu ndiye Muumba wetu. [Tusome andiko.] Hakika alikuwa na sababu ya kutuumba. Watu wengi ambao walipenda kujua sababu hiyo walianza kujifunza Neno lililoandikwa la Mungu, Biblia. Ningependa kukutolea nafasi ya kujifunza lenyewe.” Tufasirie jinsi mafunzo ya Biblia ya bure ya nyumbani yanavyoendeshwa na tuagane kukutana ili kuanzisha funzo.
6 Kukaribia watu kwa vyepesi na kutazamia mema kungeweza kuwaimarisha watu waliofiwa na mtu fulani mpendwa:
◼ “Ninashiriki katika utumishi wa peupe kwa manufaa ya wote wale waliofiwa na mtu fulani mpendwa. Hakika ni mojawapo ya mambo yaliyo magumu zaidi kushindana nayo. Ni kwa sababu hiyo broshua yenye kichwa cha habari Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa. . . ilitayarishwa. Imekwisha kusaidia mamilioni ya watu. Ningependa kukuonyesha yale kinasema juu ya ahadi moja ya Yesu Kristo yenye kupendeza sana. [Tusome fungu la tano la ukurasa 26, kutia ndani Yohana 5:21, 28, 29.] Angalia picha hii, kwenye ukurasa 29: inamaanisha ufufuo wa Lazaro uliofanyiwa na Yesu kama unavyoelezwa katika Evanjeli mbalimbali. Ikiwa unapendezwa na usomaji wa broshua hii yenye kuimarisha, ningefurahi kukuachia yenyewe.”
7 Wakati wa ziara ya kurudia, tungeweza kuonyesha tena picha kwenye ukurasa 29 wa broshua “Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa. . . ,” na kusema:
◼ “Mara ya mwisho, tulizungumzia ufufuo wa Lazaro. [Tusome maneno ya maandishi meusi kwenye ukurasa 28 na tuchunguze mawazo yanayoelezwa chini ya kichwa kidogo cha habari “Je! Kweli Hilo Lilitukia?”] Ikiwa moyo wako unajitahidi kufikia kuamini kwamba utaweza kumuona tena siku fulani mtu aliyekufa, uniruhusu tafadhali nikusaidie kupata wewe pia tumaini la ufufuo.” Tupendekeze baadaye funzo la Biblia.
8 Basi na tufanye yote tuwezayo mnamo miezi ijayo ili kumwiga Yesu na “kuwafariji wote wanaoomboleza.”—Is. 61:2.