Je! Tutafanya Hilo Tena?
Mwito Mwingine Kwa Mapainia Wasaidizi—Sehemu 1
1 Je! tutafanya hilo tena? Je! tutakuwa mapainia katika majira ya Ukumbusho? Huduma Yetu ya Ufalme ya Machi 1997 ilivuta uangalifu wetu kupitia kichwa: “Tutafute Mapainia Wasaidizi 100 000.” Tulikuwa hakika kwamba ungechukua mwito huo kwa uzito. Wakati ripoti ya utumishi ya Aprili 1997 ilipokusanywa, tulikuwa wenye furaha kujua kwamba watu 3 965 (122 Burundi, 444 Congo-Brazzaville na 3 399 Congo-Kinshasa) walijiandikisha katika utumishi wa painia msaidizi, na jambo hilo ingawa vita. Tukiongeza kwenye hesabu hiyo wale mapainia wa kawaida 5 339 na wale mapainia wa pekee 86 waliotoa ripoti mwezi huo, tunaona kwamba karibu asilimia 16 (Burundi: asilimia 12; Congo-Brazzaville: asilimia 21) ya wahubiri walikuwa katika utumishi wa painia. Je! tutafanya hilo tena katika majira haya ya Ukumbusho?
2 Tunawasifu kwa shauku wale waliofanya jitihada ya ziada ili kuongeza utumishi wao wa shambani mnamo Aprili iliyopita. Kwa wazi, nyinyi nyote mlisukumwa na upendo usio na ubinafsi kwa Yehova Mungu na kwa jirani. (Lk. 10:27; 2 Pet. 1:5-8) Wahubiri katika hali mbalimbali walipanga mambo yao vizuri kwa ajili ya kuwa mapainia wasaidizi. Katika kutaniko moja, wahubiri 51 walipainia pamoja katika mwezi uleule, kutia ndani wengi kati ya wazee, mama mmoja aliyekuwa na mtoto wa kike wa miezi 15, dada aliyeacha kazi yake na kupata kazi ya nusu-wakati ili kumwezesha kupainia, na dada mzee-mzee ambaye alikuwa hajapainia kamwe kabla ya hapo. Mwangalizi wa mzunguko aliandika: “Jitihada kubwa mno katika kazi ya kuhubiri ni yenye kufanyika. . . . Si kwamba tu hili lina matokeo juu ya eneo lakini makutaniko ni yenye kufurika kwa shauku. Ndugu ni wenye furaha kupata kujuana vizuri zaidi na vilevile kupata matokeo mazuri katika huduma.”
3 Vijana pia hawakuachwa nyuma mnamo Aprili iliyopita. Mhubiri asiyebatizwa mwenye umri wa miaka 13 alikuwa amefikiria kimbele wakati ambapo angeonyesha wakfu wake kwa Yehova. Baada ya yeye kubatizwa katika Februari, aliandika kuhusu tamaa yake ya kuwa painia msaidizi mnamo Machi: “Nikiwa sikuwa na kitu cha kunizuia tena, nilijaza mara moja ombi langu. . . . Mambo yaliyoonwa mengi ya ajabu tuliyofurahia yasingekuwa halisi kamwe usingekuwa ule mwaliko wenu wenye upendo wa kupainia. Mimi ni mwenye shukrani kwa Yehova kuona nimekuwa na pendeleo hili la kuwa miongoni mwa wale 100 000 walioitikia.” Amejiwekea mradi wa kufanya hilo tena.
4 Labda ulikuwa miongoni mwa wale 3 965 waliojishughulisha katika utendaji wa painia msaidizi mnamo Aprili iliyopita, au wale 6 721 mnamo Mei, au tena wale 8 685 mnamo Juni. Je! utafanya hilo tena mwaka huu? Ikiwa haukuwa na uwezo wa kupainia mnamo Aprili iliyopita, je! ungeweza kufanya hilo mwaka huu? Je! tunaweza kuzidi 8 260, hesabu ya wale waliokuwa mapainia wasaidizi mnamo Juni 1997 (au 141 waliokuwa mapainia Burundi mnamo Agosti 1997; 444 mnamo Aprili huko Congo-Brazzaville)? Hiyo ilikuwa hesabu kubwa zaidi ya mapainia wasaidizi iliyofikiwa katika eneo letu kwa ujumla.
5 Kaza Fikira Juu ya Aprili na Mei: Mwaka huu, Ukumbusho utakuwa Siku ya Posho, Aprili 11, ukifanya Aprili kuwa mwezi bora wa kuzidisha utendaji katika huduma. (2 Kor. 5:14, 15) Katika siku 11 za kwanza, tutakuwa waangalifu kwa kualika watu wenye kupendezwa wengi iwezekanavyo kuhudhuria Ukumbusho. Ikiwa unapanga kuwa painia msaidizi, tafadhali toa ombi lako mapema sana kabla ya siku unayotamani kuanza.—1 Kor. 14:40.
6 Kwa kuwa mwezi wa Mei una miisho-juma mitano yenye kuenea, wahubiri wenye kuenda shuleni au wale wanaofanya kazi ya kimwili ya wakati wote wanaweza kuona kuwa rahisi kuwa mapainia wasaidizi mwezi huo. Kwa kuratibu saa kumi katika utumishi wa shambani kila moja ya misho-juma hiyo mitano, ungehitaji kuratibu tu saa 10 za ziada katika mwezi ili kufikia saa 60 zinazoombwa.
7 Mnamo Aprili na Mei, tutakuwa wenye kutolea nakala za Mnara wa Mlinzi na Amkeni! kama toleo la vichapo. Hilo lingetia moyo hata wengi wetu kupanua utumishi na kupainia. Kwa nini tunasema hivyo? Magazeti ni rahisi kutoa (bei imepunguzwa) na ni yenye kufurahisha kutumika nayo katika huduma. Yanafaa katika pande zote za utumishi: mahubiri ya nyumba kwa nyumba na duka kwa duka, vilevile katika kukaribia watu barabarani, kwenye vituo vya basi, katika mashamba ya wanyama na katika vikao vingine vya vivi hivi. Jambo la maana zaidi, Mnara wa Mlinzi na Amkeni! hutetea kweli za Ufalme. Yanavuta uangalifu kwenye utimizo wa unabii wa Biblia, yakionyesha kwamba Ufalme wa Mungu unatawala. Yanagusa pia maisha ya wasomaji wayo kwa kushughulika vema na mahitaji halisi ya watu. Ikiwa tunafikiri juu namna maisha yetu yalivyoguswa na magazeti hayo yenye thamani, tutasukumwa kushiriki kuyagawa kwa wingi iwezekanavyo mnamo Mei na Juni.
8 Ripoti zinaonyesha kwamba makutaniko mengi yamerundika stoki kubwa za magazeti. Tuonyeshe kwamba tunathamini wakati na mali vinavyotumiwa kwa utowaji wayo na tusiyaache yachakae. Tukumbuke pia kwamba mamilioni ya watu wanyofu wanahitaji magazeti hayo ili kujua ukweli. (Yn. 8:31, 32) Pia tunatia moyo wale wote wanaohusika, zaidi waangalizi wa utumishi, watumishi wa huduma wanaohusika na magazeti na viongozi kwenye mafunzo ya kitabu, wachukue uongozi kuhusiana na kumaliza stoki hizo. Tujitahidi kufanya hivyo huku tukitumika kama vile mapainia wasaidizi.
9 Katika kutayarisha utendaji huo wenye kuzidishwa wa magazeti, utafaidika kwa kurudilia makala haya: “Mnara wa Mlinzi na Amkeni!—Majarida ya Wakati Ufaao Yenye Kweli” (Mnara wa Mlinzi wa Januari 1, 1994), na “Tutayarishe Utoaji Wetu Wenyewe wa Magazeti” (Huduma Yetu ya Ufalme ya Novemba 1996).
10 Wazee Hutoa Kielelezo: Ili kusaidia wale wahubiri wengi waliopainia mnamo Aprili iliyopita, wazee katika kutaniko moja walitoa Siku ya Posho moja katika mwezi kama vile siku ya pekee ya utumishi kwa kutaniko lote. Mipango ilichukuliwa ili kukutana mara sita tofauti tofauti katika mchana, ikitolea wote katika kutaniko nafasi ya kushiriki katika aina mbalimbali za kutoa ushahidi. Hilo lilitia ndani kutoa ushahidi kwa wafanya-biashara, kutoa ushahidi barabarani, kuhubiri nyumba kwa nyumba, kufanya ziara za kurudia, kuandika barua, na kutoa ushahidi kwa njia ya simu. Itikio lilikuwa lenye kutokeza: wahubiri 117 walishiriki katika utumishi wa shambani siku hiyo. Jumla ya saa 521 zilipitishwa katika huduma na angusho la magazeti, broshua na vitabu 617! Msisimuko wa Siku ya Posho hiyo uliendelea hadi Siku ya Yenga iliyokuwa na hudhurio kubwa sana kwenye Mkutano wa Watu wote na funzo la Mnara wa Mlinzi.
11 Kwenye kila Mkutano wa Utumishi mnamo Aprili na Mei, kutaniko lingepaswa kukumbushwa juu ya wakati na mahali ambapo mikutano kwa ajili ya utumishi itafanyika katika juma lijalo, hasa ikiwa mipango ya ziada inachukuliwa zaidi ya ile inayopangwa kikawaida. Mapainia wa kawaida na wahubiri wengine wasiokuwa mapainia wasaidizi wanatiwa moyo kutegemeza mipango hiyo ya kikundi kwa kadiri hali yao inavyoruhusu. (Itaendeleshwa katika chapa ya Mei.)
[Box on page 5]
Je! Unaweza Kuwa Painia Msaidizi?
“Hata uwe una hali gani za kibinafsi, kama umebatizwa, una hali nzuri ya kiadili, unaweza kufanya mpango utimize takwa la kutumia kila mwezi saa 60 katika huduma ya shambani na unaamini ungeweza kutumika kuwa painia-msaidizi mwezi mmoja au zaidi, wazee wa kundi watafurahi kufikiria ombi lako la pendeleo hili la utumishi.”—Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu, ukurasa 114.
[Examples on page 7]
Programu Za Painia Msaidizi
Kielelezo cha Namna ya Kupanga Saa 15 za Utumishi wa Shambani Kila Juma
Asubuhi—Siku ya Kwanza Hadi Siku ya Posho
Siku ingine yoyote inaweza kutiwa mahali pa siku ya Yenga
SikuWakatiSaa
Siku ya KwanzaAsubuhi2:30
Siku ya PiliAsubuhi2:30
Siku ya TatuAsubuhi2:30
Siku ya NneAsubuhi2:30
Siku ya TanoAsubuhi2:30
Siku ya PoshoAsubuhi2:30
Jumla Saa:15
Siku Mbili za Mchana Mzima
Haidhuru siku gani mbili za juma zinaweza kuchaguliwa
SikuWakatiSaa
Siku ya TatuMchana Mzim̀a7:30
Siku ya PoshoMchana Mzima7:30
Jumla Saa:15
Jioni Mbili na Mwisho-Juma
Haidhuru jioni gani mbili za siku za juma zinaweza kuchaguliwa
SikuWakatiSaa
Siku ya KwanzaJioni1:30
Siku ya TatuJioni1:30
Siku ya PoshoMchana Mzima8
Siku ya YengaNusu ya Mchana4
Jumla Saa:15
Siku za Juma Kisha Mchana-Kati na Siku ya Posho
Siku ingine yoyote inaweza kutiwa mahali pa Siku ya Yenga
SikuWakatiSaa
Siku ya KwanzaKisha Mchana-Kati2
Siku ya PiliKisha Mchana-Kati2
Siku ya TatuKisha Mchana-Kati2
Siku ya NneKisha Mchana-Kati2
Siku ya TanoKisha Mchana-Kati2
Siku ya PoshoMchana Mzima5
Jumla Saa:15
Programu Yangu ya Kibinafsi
Amua juu ya hesabu ya saa kwa kila wakati
SikuWakatiSaa
Siku ya Kwanza
Siku ya Pili
Siku ya Tatu
Siku ya Nne
Siku ya Tano
Siku ya Sita
Siku ya Yenga
Jumla Saa:15