Majibu Kwa Maulizo Yenu
◼ Tunaweza kufanya nini ili kuboresha matokeo ya mikutano yetu?
Wengine wanaweza kuwa na mwelekeo wa kuhisi kwamba wazee na watumishi wa huduma peke yao ndiyo huwa na daraka kwa ajili ya mafanikio ya mikutano ya kutaniko kwa kuwa wanaiongoza na kushughulika na sehemu nyingi zaidi. Kwa kweli, kila mmoja wetu anaweza kuchangia kibinafsi ili mikutano iwe yenye kupendeza na yenye kufaidisha. Tunaweza kufanya mikutano iwe yenye matokeo zaidi kwa njia kumi zifuatazo:
Tujitayarishe Kimbele. Wakati tunajitayarisha vizuri, mikutano inavuta kupendezwa kwetu. Wakati kila mmoja wetu anafanya hilo, mikutano inakuwa yenye kupendeza zaidi na yenye kujenga zaidi. Tuhudhurie Kikawaida. Hudhurio la juu zaidi ni lenye kutia moyo kwa kila mmoja mwenye kuwako, ikitia nguvu uthamini wetu kuelekea ulazima wa kuhudhuria. Tufike kwa wakati. Ikiwa sisi ni wenye kukaa kabla ya programu kuanza, tunaweza kujiunga katika wimbo wa kwanza na sala na hivyo kupata faida kamili kutokana na mikutano. Tunapokea hatua kwa hatua kitabu cha nyimbo katika lugha za kienyeji, jambo linaloongezwa kwenye chapa katika Kifaransa, Kiluba, Kirundi na Otetela. Tunatumaini kukipata katika lugha nyingine. Tangu wakati kitabu cha nyimbo kitakapopatikana katika lugha inayotumiwa na kutaniko, itakuwa vizuri kwamba kutaniko lote liimbe katika lugha ya kienyeji badala ya kwamba sehemu moja ya wahudhuriaji iimbe katika lugha moja na sehemu nyingine katika lugha nyingine. (Rom. 15:6; 1 Kor. 14:23, 33) Tuje tukiwa na vifaa vyote. Kwa kuleta Biblia yetu na vichapo (au kichapo) vinavyotumiwa wakati wa mikutano, tunaweza kufuata na kuelewa vizuri zaidi yale yanayozungumziwa. Tuepuke vikengeusha-fikira. Tunaweza kusikia vema wakati tunapoketi mbele. Kusemezana kwa sauti ya chini pia kwenda na kurudi kwenye choo kunaweza kusababisha sisi na wengine tukose mkazo wa fikira. Tuwe washiriki. Wakati wengi wetu huinua mikono na kutoa maelezo, wengi hutiwa moyo na kujengwa kwa wonyesho wa imani. Tutoe maelezo mafupi. Hili linatolea wengi kadiri iwezekanavyo nafasi ya kushiriki. Tunaweza kutoa maelezo yetu mafupi yenye kuhusiana tu na habari tunayojifunza. Tutimize migawo. Tukiwa wanafunzi katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi au washiriki kwenye Mkutano wa Utumishi, tujitayarishe vema, turudilie kipindi kimbele, na tusijaribu kuepa. Tupongeze washiriki. Tuambie wengine namna tunavyothamini sana jitihada zao. Hilo linawajenga na kuwasukuma kufanya hata zaidi wakati ujao. Tutiane moyo. Salamu zenye fadhili na maneno yenye kujenga, kabla na baada ya mikutano, zinaongeza kwenye furaha na faida tunazopata kutokana na kuhudhuria mikutano.