Waangalizi Wanaoongoza —Kiongozi Wa Funzo La Mnara Wa Mlinzi
1 Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova ndilo andalio kubwa la “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” kwa ajili ya kutupa chakula cha kiroho “kwa wakati ufaao.” (Mt. 24:45) Mzee anayeongoza Funzo la Mnara wa Mlinzi analo daraka kubwa kama vile mwalimu hodari anayetoa kielelezo chema katika maisha ya Kikristo.—Rom. 12:7; Yak. 3:1.
2 Ili kufundisha kwa matokeo, kiongozi wa Funzo la Mnara wa Mlinzi anapaswa kufanya jitihada ya kweli katika kutayarisha kila juma. Anafanya hivyo kwa sala na kwa makini. Kupendezwa kwake sana na kutaniko huonekana katika jitihada yake ya kweli ya kugusa mioyo yetu kwa kutumia habari inayochunguzwa. Yeye anakaza fikira juu ya mambo makuu ya somo na anatusaidia tuone jinsi mambo hayo yanavyohusiana na kichwa cha makala.
3 Matayarisho yake yenye kina hutia ndani kuchunguza maandiko kimbele ili ajue jinsi yanavyotumika. Yeye anaweka Neno la Mungu pa nafasi ya kwanza [W 4fore—to the fore] kwa kutia moyo kutaniko litumie vizuri Biblia wakati wa funzo. Nukta kubwa inapokuwa haikuzungumziwa katika maelezo ya kutaniko au matumizi ya andiko kuu yanaposahauliwa, yeye huuliza ulizo la pekee la ziada ili atokeze habari hiyo. Kwa kufanya hivyo, anatusaidia tufikie mikataa sahihi na kujua jinsi ya kutumia yale tunayojifunza katika maisha yetu.
4 Kiongozi wa Funzo la Mnara wa Mlinzi hujitahidi hatua kwa hatua kufanya uwezo wake mwenyewe wa kufundisha uwe bora. Yeye hatoi maelezo kupita kiasi lakini anatutia moyo tutoe maelezo—katika maneno yetu wenyewe, kwa kifupi, na kwa kufaa [W 1point—to the point]. Anaweza pengine kutukumbusha kwamba mtu wa kwanza anayetoa maelezo kuhusu fungu anapaswa kutoa jibu fupi, la moja kwa moja la ulizo lililochapwa katika gazeti. Maelezo ya ziada ya wasikilizaji yanaweza kuvuta uangalifu juu ya matumizi ya maandiko, hoja zenye kutegemeza wazo, au matumizi yenye manufaa ya habari. Kiongozi wa Funzo la Mnara wa Mlinzi hufanya kazi ili aamshie kila mmoja tamaa ya kushiriki kwa kuchochea utayarishaji wa binafsi na wa familia.
5 Kama watu ‘waliofundishwa na BWANA,’ tunathamini “zawadi [zikiwa] wanadamu,” kama vile kiongozi wa Funzo la Mnara wa Mlinzi, “wafanyao kazi kwa bidii katika . . . kufundisha.”—Isa. 54:13; Efe. 4:8, 11; 1 Tim. 5:17.