Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
1. Tutaanza kujifunza broshua Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo? wakati gani, na hilo litatusaidia namna gani?
1 Kuanzia juma tokea tarehe 28 Mwezi wa 10, kwenye Funzo la Biblia la Kutaniko tutajifunza broshua Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo? Broshua hiyo mupya ilitolewa kwenye Mukusanyiko wa Wilaya wenye kichwa “Linda Moyo Wako!” Kusudi la broshua hiyo ni kuelekeza wanafunzi wa Biblia kwenye tengenezo la Yehova. Kujifunza broshua hiyo kutatusaidia tupendezwe zaidi na pendeleo letu la kuwa katika tengenezo la Yehova, na pia kutatusaidia tufahamu vizuri broshua hiyo ya lazima kwa ajili ya mahubiri.—Zab. 48:13.
2. Broshua Mapenzi ya Yehova itaongozwa namna gani kwenye Funzo la Biblia la kutaniko?
2 Namna Broshua Hiyo Itakavyoongozwa: Ndugu atakayeongoza funzo atahitaji kukadiria wakati ili kila somo liongozwe kwa wakati uleule. Broshua hiyo ina masomo 28; ndugu atakayeongoza atafanya utangulizi wa kila somo kwa kusoma ulizo linalofanyiza kichwa cha somo. Kisha, atamuomba musomaji asome fungu la kwanza. Kisha, atauliza ulizo ambalo atakuwa ametayarisha kwa ajili ya fungu la kwanza. Kisha hapo, kila fungu linaloanza kwa maandishi mazito meusi litasomwa na kuzungumuziwa. Kisha usomi wa kila fungu linaloanza kwa maandishi mazito meusi, ndugu atakayeongoza ataomba wasikilizaji waeleze namna fungu hilo linavyojibu ulizo linalofanyiza kichwa cha somo. Wasikilizaji wanaweza pia kutoa maelezo kuhusu picha nyingi zilizo katika broshua hiyo. Maandiko ya musingi yanapaswa kusomwa kadiri wakati unavyoruhusu. Mbele ya kuzungumuzia somo linalofuata, ndugu atakayeongoza atauliza maulizo yaliyo chini ya ukurasa ili kujikumbusha. Ikiwa kuna kisanduku “Ikiwa Unapenda Kujua Zaidi,” itaomba kisomwe, kisha ndugu atawaomba wasikilizaji waeleze namna mwanafunzi wa Biblia anavyoweza kufaidika kwa kufuata mapendekezo yaliyo katika kisanduku hicho. Wakati ukiruhusu, ndugu anayeongoza anaweza kutumia kichwa cha somo kuwa ulizo la kujikumbusha. Tukumbuke kwamba si lazima kufuata hatua hizo tunapomusaidia mwanafunzi wa Biblia.
3. Namna gani tunaweza kufaidika kabisa na funzo la broshua hiyo?
3 Ili ufaidike kabisa na funzo hilo, ujitayarishe vizuri. Ujikaze kutoa maelezo. Wakati wa funzo, fikiria kwa nini habari munayojifunza itawasaidia wanafunzi wa Biblia. Acheni basi funzo la broshua hiyo mupya litupatie ufundi wa kuwasaidia wengine wajiunge nasi katika kufanya mapenzi ya Mungu ili wao pia wawe na tumaini la kuishi milele.—1 Yoh. 2:17.