Maoni kuhusu Vidio La Bible: une force dans votre vie
Katika kujibu maulizo yafuatayo, onyesha maoni yako yenye kutoka moyoni kuhusu ujumbe unaopatikana katika vidio hii. (1a) Ni nini kilichowezesha mamilioni ya watu wabadili maisha yao ili kuyafanya yawe bora? (Ebr. 4:12) (1b) Ni nini kinachohitajiwa ili mtu afikie uwezo huo na kuutumikisha katika maisha yake? (2) Ni maandiko gani ya Biblia yaliyotajwa ili kusaida wenzi wa ndoa (a) wafanye kupashana habari kwao kuwe bora (b) wazuie hasira yao? (3) Maoni ya Kikristo kuhusu ndoa hufanyaje maisha ya familia yawe bora? (Efe. 5:28, 29) (4) Yehova ametoaje mfano mkamilifu katika kutolea watoto yale mambo matatu ambayo wote wanayataka na wanayahitaji, nao wazazi wanawezaje kufanya hivyohivyo leo? (Mk. 1:9-11) (5) Kwa nini wazazi wanapaswa kibinafsi kufundisha watoto wao Biblia, na ni nini kinachoonyesha kwamba ukawaida unahitajiwa katika kufanya hivyo? (Kum. 6:6, 7) (6) Wazazi wanawezaje kufanya funzo la familia liwe lenye kupendeza? (7) Zaidi ya funzo la Biblia, ni jambo jingine gani ambalo Neno la Mungu linachochea wazazi kutolea watoto wao? (8) Shauri la Biblia linawezaje kusaidia familia iokoke kiuchumi? (9) Wakati zinapotumiwa, ni kanuni gani za Kimaandiko zinazosaidia kupunguza matatizo ya kiafya? (10) Kanuni za Neno la Mungu zimefanyaje maisha yako mwenyewe yawe tofauti? (11) Kwa nini kutazama vidio hii kunaweza kutia moyo mtu fulani unayemtembelea katika huduma akubali funzo la Biblia la nyumbani?