Tusaidie Wale ‘Walio na Mwelekeo Unaofaa’
1 Kila mtu ana mwelekeo uliotia mizizi katika moyo wake wa mfano. (Mt. 12:35) Biblia inasema kuhusu mtu ambaye “moyo wake una mwelekeo wa kupigana.” (Zab. 55:21) Wengine wana “mwelekeo wa ghadhabu.” (Met. 29:22) Lakini kuna pia wale ‘walio na mwelekeo unaofaa kwa ajili ya uzima wa milele.’ (Mdo. 13:48) Katika siku yetu, Yehova anakusanya kwake watu hao wenye mwelekeo unaofaa. (Hag. 2:7) Tunawezaje kuwasaidia wapate kuwa waabudu wa Yehova?
2 Rudi kwa Kudhamiria: Kuwa na mtazamo wenye kufaa kuhusu kufanya ziara za kurudia ni jambo la maana sana ili tutimize utume wetu wa kufanya wanafunzi. (Mt. 28:19, 20) Je, tunafanya haraka kufuatia kupendezwa tunakopata? Je, tunarudilia wale wote waliokubali vichapo au wanaoonyesha kupendezwa na habari njema? Je, tunadumu katika jitihada zetu za kuwasaidia wakomae kiroho? Kwa kuwa maisha yanahusika, tunapaswa kutafuta kukomaza kupendezwa kote tunakopata.
3 Unapokuwa bado unakumbuka mazungumzo uliyokuwa nayo na mtu mwenye kupendezwa, chukua wakati wa kuandika jina lake na anwani yake. Andika habari mliyozungumzia, maandiko yaliyosomwa, na kichapo ulichomwachia. Baadaye, azimia kurudi mapema zaidi iwezekanavyo.
4 Jinsi ya Kufanya Ziara ya Kuridia: Unapofanya ziara ya kurudia, inafaa kuwa mwenye shauku na mwenye urafiki na kuonyesha kwamba unapendezwa kibinafsi na mwenye nyumba. Fanya mazungumzo yawe mepesi na yenye kutegemea Maandiko. Tayarisha habari ya kibiblia yenye kupendeza mtakayozungumzia, na mwishoni mwa ziara, tokeza ulizo linaloweza kujibiwa kwenye ziara ijayo. Ni vizuri zaidi kuepuka ubishi usiofaa kuhusu maoni yasiyo ya kimaandiko ambayo mwenye nyumba anaweza kutoa. Jitahidi kuzungumzia mambo ambayo juu ya hayo mnakubaliana.—Kol. 4:6.
5 Kufanya ziara za kurudia kunaomba jitihada, lakini dhawabu ni zenye kutosheleza. Painia mmoja huko Japani alijiwekea mradi wa kufanya ziara zaidi za kurudia kila mwezi. Akaanza kuchukua maandishi kuhusu wale wote aliokutana nao katika mahubiri ya nyumba kwa nyumba, na baada ya siku saba, akawatembelea tena. Alitayarisha kikamili yale ambayo angesema na akatimiza huduma yake akiwa na uhakika kamili kuhusu ujumbe aliopeleka. Kwenye moja ya ziara zake, aliweza kuanza kujifunza na mtu ambaye alikuwa amemwambia: “Nimekuwa sikuzote nikiwafukuza ninyi. Hii ndiyo mara yangu ya kwanza kusikiliza.” Udumifu wenye upendo wa painia ulileta matokeo. Kufikia mwisho wa mwezi alikuwa akiripoti mafunzo kumi ya Biblia.
6 Hali za watu ni zenye kubadilika daima. (1 Kor. 7:31) Wakati mwingine inaomba kujaribu mara nyingi ili kupata mtu mwenye kupendezwa nyumbani. Kwa kufanya ziara za kurudia kwa kudhamiria, tunaweza kusaidia wale walio na mwelekeo unaofaa watembee katika barabara inayoongoza kwenye uzima.—Mt. 7:13, 14.
[Study Questions]
1. Yehova anakusanya nani kwake katika siku yetu?
2. Ni nini kinachohusika katika kutimiza utume wetu wa kufanya wanafunzi?
3. Tunapaswa kufanya nini baada ya kuzungumza na mtu fulani katika huduma?
4. Tunawezaje kufanya ziara za kurudia zenye matokeo?
5. Painia mmoja alifanya jitihada gani, naye alipata matokeo gani?
6. Kwa nini tunapaswa kudumu katika kufanya ziara za kurudia?