Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Jan. 15
“Kwa kuwa leo, kutotimiza ahadi ni jambo la kawaida sana, inakuwa vigumu kwa watu wengi kumtumaini mtu yeyote. Je, unafikiri kuna yeyote yule ambaye tunaweza kutumaini ahadi zake? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Yoshua 23:14.] Gazeti hili linaonyesha jinsi tunavyoweza kutumaini ahadi za Mungu zinazoandikwa katika Biblia.”
Amkeni! Jan. 22
“Tazama jinsi jina la pekee la Mungu linavyoonekana katika lugha ya Kiebrania. [Onyesha jalada.] Watu fulani wanaamini sana kwamba jina hilo halipaswi kamwe kutamkwa kwa sauti kubwa. Wengine wanalitumia bila kusita. Toleo hili la Amkeni! linazungumzia ubishi huo. Linazungumzia pia jinsi tunavyoweza kumjua Mungu kwa jina.” Soma Zaburi 83:18.
Mnara wa Mlinzi Feb. 1
“Wengi kati yetu wanajaribu kutunza afya ya kimwili. Lakini, uchunguzi wa siku hizi unaonyesha kwamba hali yetu ya kiroho inakuwa na matokeo pia juu ya afya yetu njema. Je, unafikiri kwamba hilo linawezekana? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Mathayo 5:3.] Toleo hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia jinsi tunavyoweza kutosheleza mahitaji yetu ya kiroho.”
Amkeni! Feb. 8
“Leo, maisha ya watu wengi ni yenye shughuli sana, nao wanahitaji kupumzika vya kutosha. Huenda utakubaliana na maneno haya yaliyoandikwa zaidi ya miaka 3,000 iliyopita. [Soma Mhubiri 4:6. Kisha acha mtu ajibu.] Toleo hili la Amkeni! linatoa habari yenye kusaidia kuhusu jinsi ya kutambua na kupambana na tatizo la kutolala vya kutosha.”