Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Jan. 15
“Katika miaka ya karibuni, watu wamependezwa sana na malaika. Je, umekwisha kujiuliza ikiwa malaika ni nani na jinsi gani wana uvutano juu ya maisha yetu? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Zaburi 34:7.] Gazeti hili linazungumzia yale ambayo Biblia inasema kuhusu kazi za malaika—kazi za wakati uliopita, za wakati huu, na za wakati ujao.”
Amkeni! Jan.
“Mashauri ni yenye kupatikana leo kuhusu karibu kila jambo. Unafikiri kwamba tunaweza kutumainia mashauri hayo yote? [Acha mtu ajibu. Kisha soma 2 Timotheo 3:16.] Gazeti hili la Amkeni! linaonyesha kwa nini tunaweza kutumaini Biblia kuwa chanzo chenye kutegemeka cha hekima inayotumika.” Kazia makala inayoanzia kwenye ukurasa wa 18.
Mnara wa Mlinzi Feb. 1
“Sisi sote tunahitaji fedha ili kuishi. Lakini, je, wewe pia unakubali kwamba kuna uhitaji wa kujiepusha na hatari inayotajwa hapa? [Soma 1 Timotheo 6:10, na acha mtu ajibu.] Toleo hili la Mnara wa Mlinzi linatusaidia kutambua mitego fulani ya kawaida ya utajiri wa kimwili na linazungumzia jinsi ya kuepuka mitego hiyo.”
Amkeni! Feb.
“Wengi wetu wenye kuwa na washiriki wa jamaa na marafiki walio wazeewazee hujiuliza jinsi tunavyoweza kuwasaidia ili wapambane na matatizo ya uzee. Sivyo? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linapendekeza mambo tunayoweza kufanya ili uzee usionekane kuwa jambo lenye kulemea zaidi. Linaeleza pia jinsi unabii huu utatimizwa.” Soma Ayubu 33:25.