Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 6/04 uku. 4
  • Funzo la Kitabu la Kutaniko—Kwa Nini Tunalihitaji

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Funzo la Kitabu la Kutaniko—Kwa Nini Tunalihitaji
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jinsi Mpango wa Funzo la Kitabu la Kutaniko Unavyotusaidia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Jinsi Waangalizi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko Wanavyoonyesha Kupendezwa Kibinafsi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Namna ya Kufaidika na Kikundi Chenu cha Mahubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Saidia Mwangalizi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko Lako
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 6/04 uku. 4

Funzo la Kitabu la Kutaniko—Kwa Nini Tunalihitaji

1 Katika mwaka wa 1895, vikundi vya funzo vya wanafunzi wa Biblia, kama Mashahidi wa Yehova walivyokuwa wakiitwa wakati huo, vikaja kujulikana kuwa Vikundi vya Mapambazuko kwa Ajili ya Funzo la Biblia. Mabuku ya Mapambazuko ya Mileani (ya Kiingereza) yakaanza kutumiwa kwa ajili ya funzo. Baadaye, mikutano hiyo ikaanza kuitwa Vikundi vya Kiberoya kwa Ajili ya Funzo la Biblia. (Mdo. 17:11) Mara kwa mara kikundi kidogo kilikutana katika makao ya watu binafsi wakati wa jioni uliofaa kikundi. Hivyo ndivyo mpango wa Funzo la Kitabu la Kutaniko ulivyoanzishwa.

2 Kitia-Moyo na Msaada: Kwa kuwa vikundi vya funzo la kitabu vimekusudiwa kuwa vidogo, wale wanaohudhuria wana nafasi kubwa ya kufanya onyesho la imani yao kupitia maelezo wanayotoa. Mpango huo unatokeza “ubadilishanaji wa kitia-moyo . . . , kila mmoja kupitia imani ya mwingine.”—Rom. 1:12.

3 Kuchunguza namna mwangalizi wa funzo la kitabu anavyofundisha kunaweza kutusaidia ‘kutumia sawasawa neno la kweli.’ (2 Tim. 2:15) Angalia jinsi anavyokazia Maandiko yaliyo msingi wa habari. Ikiwa inafaa, kulingana na kichapo kinachotumiwa, anaweza kukazia mambo makuu anapofanya ukaguzi wa kumalizia, akitumia tu Biblia. Mfano wake mzuri unaweza kutusaidia tuboreshe namna yetu ya kufundisha katika huduma ya Kikristo.—1 Kor. 11:1.

4 Zaidi ya kuongoza funzo kila juma, mwangalizi wa funzo la kitabu anachukua uongozi katika kueneza evangeli. Akishirikiana na mwangalizi wa utumishi, anafanya mipango inayofaa kwa ajili ya utumishi wa shambani. Anajaribu kusaidia washiriki wote wa kikundi kutimiza daraka lao la Kikristo la kuhubiri habari njema na kufanya wanafunzi.—Mt. 28:19, 20; 1 Kor. 9:16.

5 Mwangalizi wa funzo la kitabu anahangaikia hali njema ya kiroho ya kila mmoja katika kikundi. Anaonyesha hangaiko hilo kwenye mikutano ya kutaniko na anapotumika na wengine katika utumishi wa shambani. Anatumia tena nafasi mbalimbali anapotembelea ndugu nyumbani kwao ili kuwatia moyo kiroho. Wote wanapaswa kujisikia kuwa wamepokewa vizuri wanapomuendea mwangalizi wa funzo la kitabu ili kupata msaada wa kiroho, wakati wowote wanapokuwa na uhitaji.—Isa. 32:1, 2.

6 Tuimarishane: Katika inchi ambako utendaji wa watu wa Mungu unawekewa mipaka, ndugu wanakutana katika vikundi vidogovidogo mara kwa mara. Ndugu mmoja anakumbuka: “Ingawa utendaji wetu wa Kikristo ulikuwa umepigwa marufuku, ilipowezekana tulifanya mikutano ya kila juma tukiwa vikundi vyenye watu wapatao 10 mpaka 15. Tuliimarishwa kiroho kwenye mikutano hiyo, kutokana na usomaji wetu wa Biblia na ushirika wa baada ya mikutano. Tulilinganisha mambo yaliyompata kila mmoja wetu, na tukaja kutambua kwamba sote tulipambana na mambo yaleyale.” (1 Pet. 5:9) Vivyo hivyo, nasi tuimarishane kwa kutegemeza kikamili mpango wa Funzo la Kitabu la Kutaniko.—Efe. 4:16.

[Maulizo ya Funzo]

1. Mpango wa Funzo la Kitabu la Kutaniko ulianzishwaje?

2. Tunawezaje ‘kubadilishana kitia-moyo’ kwenye funzo la kitabu?

3, 4. Mpango wa funzo la kitabu unatusaidiaje kutimiza huduma yetu?

5. Ni msaada gani wa kibinafsi unaopatikana kupitia funzo la kitabu?

6. (a) Ndugu zetu katika inchi fulani wameimarishanaje kwa kukutana katika vikundi vidogovidogo? (b) Wewe kibinafsi umefaidikaje na mpango wa funzo la kitabu?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine