Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Ago. 15
“Leo, watu wanatafuta mashauri kutoka vyanzo vingi kuhusu ndoa na jinsi ya kulea watoto. Je, unafikiri mashauri yaliyo bora zaidi yanaweza kupatikana wapi? [Acha mtu ajibu.] Toleo hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia mashauri fulani yenye hekima kuhusu maisha ya familia, mashauri yanayotolewa na Muumba wa wanadamu.” Soma Zaburi 32:8.
Amkeni! Ago. 22
“Unafikiri ni jambo lenye maana kadiri gani kwa baba kushughulikia maisha ya watoto wao? [Acha mtu ajibu.] Toleo hili la Amkeni! linazungumzia tatizo lenye kuongezeka kuhusu baba wasiokuwapo nyumbani. Linaeleza pia jinsi baba wanavyoweza kuwa na uvutano mzuri juu ya watoto wao.” Soma Methali 13:1.
Mnara wa Mlinzi Sept. 1
“Sisi sote tunataka kuwa wenye furaha. Je, unafikiri kwamba mambo yanayotajwa hapa yanaweza kweli kuleta furaha? [Soma Mathayo 5:4a, 6a, 10a. Kisha acha mtu ajibu.] Gazeti hili linaeleza maana ya yale maneno yenye kujulikana sana kutokana na Mahubiri ya Mlimani na linazungumzia jambo lingine linalohitajiwa ili kuwa na furaha.”
Amkeni! Sept. 8
“Inakadiriwa kwamba mtu mmoja kati ya wanne atapatwa na ugonjwa wa akili wakati fulani katika maisha yake. Wengi kati yetu wanajua mtu anayesumbuliwa na ugonjwa huo. [Fungua kwenye makala.] Makala hii inatoa mapendekezo yenye kusaidia kuhusu yale tunayoweza kufanya ikiwa mtu fulani tunayempenda anapatwa na hali hiyo.”