Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Ago. 15
“Baada ya msiba wa kufiwa, wengi wanajiuliza jambo linalotokea mtu anapokufa. Je, unafikiri kwamba inawezekana kuelewa kifo? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linaeleza yale ambayo Biblia inasema kuhusu hali ya wafu. Inazungumzia pia ahadi ya Mungu ya kufufua wapendwa wetu waliokufa.” Soma Yohana 5:28, 29.
Amkeni! Ago. 22
“Je, ulijua kwamba utalii (tourisme) umekuwa ndilo shirika la kwanza ulimwenguni? [Acha mtu ajibu.] Kuongezeka kwa utalii kumeleta faida na matatizo. Gazeti hili linazungumzia faida na hasara ya utalii wa kisasa. Linatoa pia mapendekezo fulani yanayofaa kwa ajili ya wale wanaofanya utalii (touristes) kutoka mataifa mbalimbali.”
Mnara wa Mlinzi Sept. 1
“Katika ulimwengu wa leo, uaminifu ni sifa nzuri ambayo inatukuzwa mara nyingi lakini watu hawaitumii maishani. Je, maisha hayangekuwa bora zaidi ikiwa watu wengi zaidi wangelikuwa kama rafiki anayezungumziwa hapa? [Soma Methali 17:17. Kisha acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia faida zinazotokana na kuwa mwaminifu kwa familia yetu na marafiki zetu.”
Amkeni! Sept. 8
“Labda umewahi kustaajabishwa na ushirikiano unaopatikana katika maumbile. [Onyesha moja ya mifano inayotajwa katika makala.] Ni jambo la kusikitisha kwamba hatuoni ushirikiano zaidi kati ya wanadamu, sivyo? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia jinsi Mungu atakavyoleta hivi karibuni amani na upatano hapa duniani.” Soma Isaya 11:9.