Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Nov. 15
“Karibu kila mtu anatamani kuwa na afya nzuri na maisha marefu. Lakini, ikiwa hilo lingewezekana, je, ungependa kuishi milele? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Yohana 17:3.] Gazeti hili linazungumzia ahadi ya Biblia ya uzima wa Milele. Linazungumzia pia jinsi maisha yatakavyokuwa wakati ahadi hiyo itakapotimia.”
Amkeni! Nov. 22
“Mnamo miaka 20 iliyopita, maendeleo mengi yamefanywa katika kuelewa na kutunza UKIMWI. Hata hivyo, bado watu wengi wanaelezwa habari zisizo za kweli. [Onyesha kisanduku “Hekaya Kuhusu UKIMWI,” na acha mtu atoe maelezo.] Gazeti hili linazungumzia jinsi wazazi wanavyoweza kulinda watoto wao.” Soma Kumbukumbu la Torati 6:6, 7.
Mnara wa Mlinzi Des. 1
“Alama moja inayotofautisha wanadamu na wanyama ni uwezo wa kupambanua mema na mabaya. Jambo la kuhuzunisha ni kwamba watu wengi wanafanya mambo mabaya. Wewe unafikiri ni kwa nini? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Yeremia 17:9 au Ufunuo 12:9.] Gazeti hili linazungumzia kile kinachoweza kutusaidia kujua na kufanya yaliyo mema.”
Amkeni! Des. 8
“Maendeleo ya kitekinolojia hayajabadili mahitaji ya msingi ya mwanadamu ya kuwa na marafiki. Lakini, je, umetambua kwamba mabadiliko katika jamii yanaweza kufanya iwe vigumu leo kuwa na marafiki wa karibu? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Methali 18:24.] Gazeti hili linazungumzia jinsi tunavyoweza kufanya ili kuwa na marafiki na kuendeleza urafiki wa kweli.”