Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
MNARA WA MLINZI Des. 15
“Wakati huu wa mwaka, watu wengi wanafikiri kuhusu kuzaliwa kwa Yesu. Je, umekwisha kujiuliza yeye alikomalia katika familia ya aina gani? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Luka 2:51, 52.] Toleo hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia mambo halisi tunayoweza kujifunza kutokana na simulizi la Biblia kuhusu malezi ya Yesu.”
Amkeni! Des. 22
“Sisi sote tunatamani kuona watoto wetu wakiishi maisha yenye furaha na yenye mafanikio. Unafikiri watoto wanahitaji nini zaidi ili kupambana na ulimwengu wa sasa wenye mikazo? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Methali 22:6.] Toleo hili la Amkeni! linazungumzia mambo ambayo watoto wanahitaji na jinsi wazazi wanavyoweza kutimiza mahitaji hayo.”
MNARA WA MLINZI Jan. 1
“Watu wengi wanatamani amani duniani. Je, unafikiri kwamba tutapata kuona utimizo wa maneno haya? [Soma Zaburi 46:9. Kisha acha mtu ajibu.] Toleo hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia jinsi hilo litakavyotimizwa na kwa nini tunaweza kutumaini ahadi ya Mungu kuhusu ulimwengu usio na vita.”
Amkeni! Jan. 8
“Ulimwenguni pote, mamilioni ya watu wanataabishwa na magonjwa ya hisia, kama vile kushuka moyo na hisia zinazobadilika-badilika. Muumba wetu anahangaikia sana watu kama hao. [Soma Zaburi 34:18.] Gazeti hili linazungumzia jinsi wale wanaougua wanavyoweza kusaidiwa. Linaonyesha pia ahadi ya Biblia kwamba karibuni magonjwa yote yataondolewa.”