Ni Aina Gani ya Matunzo ya Kiganga Iliyo Bora Zaidi?
Dr. Michael Rose, aliye mganga msimamizi, alisema hivi: “Mgonjwa yeyote anayefanyiwa upasuaji bila kutiwa damu ndiye anayepata matunzo bora zaidi.” Ni namna gani mbalimbali za matunzo na dawa zinazoweza kutumiwa mahali pa damu? Unahitaji kujua mambo hayo ili kuchukua maamuzi yanayolingana na ujuzi huo wakati wa matunzo na upasuaji. Tazama video Pas de sang : la médecine relève le défi. Kisha, tumia maulizo yafuatayo ili kuona kama unaelewa vizuri mambo hayo.—Tangazo: Kwa kuwa video hii ina vipindi vifupi vyenye kuonyesha upasuaji, wazazi watatumia hekima ili kuamua ikiwa watoto wadogo watatazama video hii.
(1) Ni sababu gani kubwa inayofanya Mashahidi wa Yehova wasikubali kutiwa damu mishipani? (2) Kuhusu matunzo ya kiganga, Mashahidi wa Yehova wanatamani nini? (3) Ni haki gani ambayo wagonjwa wanayo? (4) Kwa nini kuchagua aina ya matunzo isiyoomba kutumia damu ni jambo lenye akili na linaloonyesha kwamba mtu anahangaikia afya yake? (5) Ni mambo gani mawili ambayo waganga wanapaswa kufanya kwa haraka ikiwa mgonjwa anapoteza damu nyingi sana? (6) Kuna kanuni gani ine za aina ya matunzo isiyoomba kutumia damu? (7) Namna gani waganga wanaweza (a) kupunguza kuvuja kwa damu, (b) kuchunga chembe nyekundu za damu, (c) kufanya mwili uzae damu, na (d) kupata tena damu iliyopotezwa? (8) Eleza aina za matunzo zinazoitwa (a) mchanganyiko wa chembe-damu na (b) kuokoa chembe za damu. (9) Utapenda kupata habari gani kuhusu aina yoyote ya matunzo isiyoomba kutumia damu? (10) Je, inawezekana kufanya upasuaji mkubwa na mgumu bila kutia mtu damu? (11) Ni maendeleo gani mazuri ambayo ni yenye kuonekana sasa katika mambo ya kiganga?
Kukubali aina fulani za matunzo zinazoonyeshwa katika video hiyo ni jambo la kila mtu kuamua peke yake akiongozwa na zamiri yenye kufundishwa na Biblia. Je, umekwisha kuamua ni matunzo gani yasiyoomba kutumia damu ambayo utakubali kwa ajili yako mwenyewe na kwa ajili ya watoto wako? Unapaswa pia kujulisha watu wa jamaa yako kuhusu maamuzi yako na sababu zinazofanya uyachukue.—Ona “Maswali Kutoka kwa Wasomaji” katika Mnara wa Mlinzi wa 15/06/04, na wa 15/10/2000.