Je, Unajua Maamuzi Yako?
Katika hospitali nyingi ulimwenguni, wagonjwa wengi wanafanyiwa sasa upasuaji bila kutiwa damu. Je, unajua vizuri mambo ambayo waganga wanajua kuhusiana na kutunzwa bila kutiwa damu? Unahitaji kujua mambo hayo ili kuchukua maamuzi yenye hekima kuhusiana na matunzo na upasuaji. Tazama video Pas de sang : la médecine relève le défi. Kisha, fikiria katika sala mambo ambayo ulijifunza kwa kutumia maulizo yaliyo hapa chini.—Tangazo: Kwa kuwa video hii ina vipindi vifupi vyenye kuonyesha upasuaji, wazazi watatumia hekima ili kuamua ikiwa watoto wadogo watatazama video hii ao hapana.
(1) Ni sababu gani kubwa inayofanya Mashahidi wa Yehova wasikubali kutiwa damu mishipani? (2) Kuhusiana na matunzo ya kiganga, Mashahidi wa Yehova wanataka nini? (3) Wagonjwa wana haki ya kufanya nini? (4) Kwa nini kukubali dawa nyingine badala ya damu ao ufundi fulani mwingine wa kiganga ni jambo lenye akili na linaloonyesha kwamba mutu anahangaikia afya yake? (5) Ni mambo gani mawili ya lazima ambayo waganga wanapaswa kufanya kwa haraka ikiwa mgonjwa anapoteza damu nyingi sana? (6) Kuna kanuni gani ine za matunzo isiyoomba kutumia damu? (7) Namna gani waganga wanaweza (a) kupunguza kuvuja kwa damu, (b) kuchunga chembe nyekundu za damu, (c) kufanya mwili uzae damu, na (d) kupata tena damu iliyopotezwa? (8) Eleza ufundi wa kiganga unaoitwa (a) mchanganyiko wa chembe-damu (hémodilution) na (b) kuokoa chembe za damu (récupération du sang épanché). (9) Utapenda kupata habari gani kuhusu dawa nyingine inayoweza kutumiwa badala ya damu ao ufundi fulani wa kiganga? (10) Je, inawezekana kufanya upasuaji mkubwa na mgumu bila kutia mutu damu mishipani? (11) Ni maendeleo gani mazuri yanayoonekana sasa katika mambo ya kiganga?
Kukubali aina fulani za matunzo zinazoonyeshwa katika video hiyo ni jambo ambalo kila mutu anapaswa kujiamulia peke yake akiongozwa na zamiri iliyozoezwa na Biblia. Je, umekwisha kuamua ni matunzo gani yasiyoomba kutumia damu ao ufundi gani wa kiganga ambao utakubali kwa ajili yako mwenyewe na kwa ajili ya watoto wako na kisha ujaze kadi ya kiganga DPA (Instructions médicales)? Ili upate habari kamili kuhusu jambo hili, rudilia kwa uangalifu “Maswali Kutoka kwa Wasomaji” katika Mnara wa Mlinzi wa tarehe 15/06/04, na wa tarehe 15/10/2000. Kisha tumia karatasi za maulizo na majibu za nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya mwezi wa 11, 2006, iliyo na kichwa “Ninaona Namna Gani Sehemu za Damu na Namna Mbalimbali za Matunzo Zinazoomba Kutumia Damu Yangu Mwenyewe?” Karatasi hizo zitakusaidia kufanya maamuzi yako mwenyewe kuhusu mambo unayoweza kukubali ao kukataa. Mwishowe, andika bila makosa kwenye kadi yako ya kiganga DPA mambo yaleyale yanayohusu maamuzi yako. Watu unaotumainia (personnes de confiance) ambao wanaandikwa kwenye kadi ya kiganga DPA na washiriki wa familia wowote wasio Mashahidi wanapaswa kujulishwa mambo yote kuhusu maamuzi yako.