Kujikaza Ili Kufanya Mengi Katika Utumishi Wetu
1 Mtume Paulo aliwashauria Wakristo watembee katika njia ya Mungu na ‘waendelee kufanya hivyo kwa ukamili zaidi.’ (1 Thes. 4:1) Hilo linamaanisha nini kwetu? Jambo moja ni kwamba tunapaswa kuendelea kutafuta njia za kufanya mengi katika utumishi wetu kwa Mungu, tukijikaza sikuzote ‘kutimiza kwa ukamili huduma yetu.’—2 Tim. 4:5.
2 Ni Nini Kinachotuchochea: Ni nia yetu ya kumtumikia zaidi Muumba wetu ndiyo inatuchochea tujikaze kufanya mengi katika utumishi wetu. Tunataka kukomaa kiroho na kutafuta njia za kufanya utumishi wetu uwe mzuri zaidi. Kujipangia programu nzuri na kuwa na nia inayofaa kutatusaidia kutimiza miradi inayohusiana na utumishi wetu kwa Mungu.—Zab. 1:1, 2; Flp. 4:6; Ebr. 10:24, 25.
3 Inaomba kuwa na roho ya kutoa na ya kujitoa ili kufanya kazi nyingi katika utumishi wetu. Tunaweza kukomalisha roho hiyo kwa kufikiria sana katika sala mfano wa Yesu. (Mt. 20:28) Yesu alipata furaha nyingi kwa kutumikia wengine katika utumishi wake. (Mdo. 20:35) Tunaweza kumwiga Yesu kwa kupendezwa na wengine na kuwa waangalifu kutambua nafasi zinazopatikana ili kujikaza kufanya mengi katika utumishi wetu.—Isa. 6:8.
4 Daraka la Wazazi: Wazazi wanaweza kutia nia ya kutumikia wengine ndani ya watoto wao wanapokuwa wangali wachanga. Watoto watatambua kwamba washiriki wa familia ni wenye bidii na ni wenye kutumika sana ili kupanua utumishi wao. Alipotumika na baba ya mama yake katika kazi za kutaniko, ndugu mmoja alichochewa kujikaza ili kufanya mengi alipokuwa bado kijana. Alipoona bidii na furaha ambayo baba ya mama yake alikuwa nayo, hilo lilimchochea kutafuta nafasi za kuwatumikia ndugu zake. Sasa yeye anatumikia akiwa mtumishi wa huduma katika kutaniko.
5 Ndugu Wanahitajiwa: “Ikiwa mwanamume yeyote anajitahidi kufikia . . . , yeye anatamani kazi njema.” (1 Tim. 3:1) Maneno hayo yanatia moyo ndugu wajikaze kuwa na sifa zenye kustahili ili kupata madaraka zaidi katika tengenezo la Yehova. Si lazima mtu apate ujuzi wa pekee ao awe na uwezo wa pekee aliozaliwa nao ili kufanya hivyo. Ndugu anayejikaza kufanya mengi atatafuta kwanza Ufalme na kuwa mwenye bidii katika utumishi. (Mt. 6:33; 2 Tim. 4:5) Atajikaza kuwa mfano mzuri kwa wengine.
6 Ulimwenguni Pote: Yehova ni mwenye kuharakisha kazi ya kukusanya watu. (Isa. 60:22) Ni lazima sana wale wote wanaofuata mfano wa Yesu wafanye mengi zaidi katika utumishi wao, wakifanya hivyo kwa uharaka. Ripoti ya ulimwenguni pote inaonyesha kwamba watu 248,327 walibatizwa katika mwaka wa utumishi wa 2006. Ni kama vile watu zaidi ya 680 walibatizwa kila siku! Sisi wote na tuendelee kutafuta njia za kufanya kazi nyingi zaidi katika utumishi wetu.