Broshua Mpya ya Kutolea Watu!
1. Tutatolea watu kichapo gani katika mwezi wa 11, na kilichapishwa kwa kusudi gani?
1 Kwenye Mkusanyiko wa Wilaya wa 2009 wenye kichwa “Muendelee Kukesha!,” tulitangaziwa kutokea kwa broshua mpya yenye kichwa Biblia—Ina Ujumbe Gani? Katika mwezi wa 11 makutaniko ya ulimwenguni pote yatatolea watu broshua hiyo kwa mara ya kwanza. Namna gani watu katika eneo letu watafaidika na broshua hiyo? Watu wengi, zaidi sana wale walio katika makanisa yasiyo ya Kikristo, hawajui mengi kuhusu Biblia. Broshua hiyo inafasiria kwenye ukurasa wa 3 kwamba ilichapichwa ili kusaidia watu waelewe ‘kwa kifupi Biblia.’
2. Namna gani tunaweza kutolea watu broshua hii?
2 Jinsi ya Kuitolea Watu: Tunaweza kusema hivi: “Tulipenda kupata maoni yako kuhusu maneno haya. [Soma 2 Timotheo 3:16.] Watu wengi tunaozungumza nao wanakubali maneno hayo; wengine wanafikiri kwamba Biblia ni kitabu tu kizuri kama vitabu vingine. Unafikiri nini kuhusu Biblia? [Acha mutu ajibu.] Iwe tunafundishwa nini katika dini yetu, kuna faida kabisa za kuchunguza Biblia sisi wenyewe. [Soma fungu la utangulizi kwenye sehemu ya juu ya ukurasa wa 3.] Unaposoma ujumbe wenye kusisimua wa Biblia ulio katika broshua hii, utaona jambo fulani lenye kupendeza: Biblia ina kichwa kikuu kimoja na ujumbe mmoja.”
3. Ni utoaji gani mwingine ambao tunaweza kutumia, zaidi sana katika eneo ambamo watu wanapatikana katika dini zisizo za Kikristo?
3 Unapohubiri katika eneo ambalo lina watu wasio Wakristo, unaweza kusema: “Tulipenda kupata mawazo yako kuhusu yale yanayosemwa hapa katika Maandiko (ao katika kitabu hiki kitakatifu). [Soma Zaburi 37:11.] Unawaza dunia itakuwa namna gani wakati unabii huu utatimia? [Acha mutu ajibu.] Hii ni moja kati ya tumaini na faraja ambayo watu wa mahali pote na dini zote wanaweza kupata kutoka katika Biblia.” Soma fungu la utangulizi kwenye sehemu ya juu ya ukurasa wa 3, na utolee mutu broshua.
4. Namna gani tunaweza kutumia broshua ili kuanzisha funzo la Biblia?
4 Anzisha Funzo la Biblia: Tunaporudi tunaweza kumkumbusha msikilizaji kuhusu mazungumzo yetu ya kwanza na kuzungumzia fungu moja ao mafungu mawili kutoka habari tunayozungumzia, tukitumia maulizo mwishoni mwa sehemu tuliyochagua. Ao ikiwa tunataka kupendekeza funzo katika kitabu Biblia Inafundisha, tunaweza kusoma pamoja naye ukurasa wa mwisho wa broshua, kisha tumtolee kitabu, na kumuomba achague sura ya kitabu ambayo inampendeza, kisha tutachunguza pamoja naye fungu moja ao mafungu mawili ya kitabu. Sisi wote na tushiriki kabisa katika kutolea watu broshua hii katika mwezi wa 11!