Tuonyeshe Kabisa Kwamba Sisi Ni Wenye Shukrani Tutafanya Ukumbusho Tarehe 17 mwezi wa 4
1. Kama mtunga-zaburi, tunajisikia namna gani zaidi sana katika kipindi hiki cha Ukumbusho?
1 Kwa sababu ya matendo mengi ya Yehova ya rehema na ya wokovu, mtunga-zaburi aliuliza hivi: “Nitamlipa Yehova nini kwa ajili ya faida zake zote kwangu?” (Zab. 116:12) Leo, watumishi wa Mungu wana sababu nyingi hata zaidi za kuwa wenye shukrani. Miaka mingi kisha kuandikwa kwa maneno haya yaliyoongozwa na roho ya Mungu, Yehova alitolea wanadamu zawadi kubwa zaidi yaani, ukombozi. Tunapojitayarisha kukumbuka kifo cha Kristo tarehe 17 mwezi wa 4, tuna sababu nzuri za kuonyesha kwamba sisi ni wenye shukrani.—Kol. 3:15.
2. Ni sababu gani zinazofanya tuwe wenye shukrani kwa ajili ya ukombozi?
2 Baraka Zinazotokana na Ukombozi: Kupitia ukombozi, tunaweza ‘kusamehewa zambi zetu.’ (Kol. 1:13, 14) Hilo linatusaidia tumwabudu Yehova tukiwa na zamiri safi. (Ebr. 9:13, 14) Tunaweza kusema na Yehova kwa uhuru tunapomkaribia katika sala. (Ebr. 4:14-16) Wale wanaojizoeza imani katika ukombozi wanatazamia kabisa kupata uzima wa milele!—Yoh. 3:16.
3. Namna gani tunaweza kuonyesha kwamba tunamshuru Yehova kwa kututolea zawadi ya ukombozi?
3 Jinsi ya Kuonyesha Shukrani Yetu: Njia moja ya kuonyesha shukrani kabisa ni kusoma kila siku maandiko ya Biblia yanayopendekezwa kwa ajili ya Ukumbusho na kutafakari kuhusu maandiko hayo. Mnara wa Mlinzi wa tarehe 1 mwezi wa 2, 2011, una habari yenye kichwa ‘Je, Umejitayarisha kwa Ajili ya Siku ya Maana Zaidi ya Mwaka?’ habari hiyo iliandikwa ili kutusaidia tujitayarishe kwa ajili ya siku hiyo. Tunaweza pia kumwambia Yehova kwa njia ya sala yenye kutoka moyoni kwamba tunaona ukombozi kuwa wa maana sana. (1 The. 5:17, 18) Kuhuzuria Ukumbusho ili kuonyesha kwamba tunatii amri ya Yesu, kunaonyesha kwamba sisi ni wenye shukrani. (1 Kor. 11:24, 25) Zaidi ya hilo, tunaweza kuiga upendo mkubwa wa Yehova kwa kualika watu wengi iwezekanavyo ili waje kuhuzuria Ukumbusho pamoja nasi.—Isa. 55:1-3.
4. Azimio letu linapaswa kuwa nini?
4 Watu wa Yehova wenye shukrani hawataona Ukumbusho kama tu mkutano wa kawaida. Ni mkutano wa maana zaidi wa mwaka! Kwa kuwa Ukumbusho unakaribia, azimio letu liwe kama lile la mtunga-zaburi aliyeandika: “Mbariki Yehova, Ee nafsi yangu, wala usiyasahau matendo yake yote.”—Zab. 103:2.