Tumshukuru Mungu kwa Ajili ya Zawadi Kubwa Zaidi Aliyotutolea
1. Kwa nini sisi ni wenye shukrani hasa kwa Yehova?
1 Kati ya ‘zawadi njema’ nyingi za Yehova, zabihu ya ukombozi aliyotoa Mwana wake mpendwa, ndiyo zawadi iliyo kubwa zaidi. (Yak. 1:17) Inafanya iwezekane kwetu kupata baraka nyingi, kutia ndani msamaha wa zambi zetu. (Efe. 1:7) Sisi ni wenye shukrani kila siku kwa sababu ya zawadi hiyo. Wakati wa kipindi cha Ukumbusho, tunachukua hasa wakati wa kufikiri sana juu ya zawadi hiyo ya maana sana.
2. Namna gani tunaweza kusaidia familia yetu na sisi wenyewe kuonyesha shukrani kwa ajili ya zabihu ya ukombozi?
2 Saidia Familia Yako: Ili kusaidia familia yako ionyeshe shukrani, katika majuma yatakayotangulia kipindi cha Ukumbusho cha tarehe 30 mwezi wa 3, munaweza kutumia wakati wa Ibada ya Familia ya mangaribi ili kuzungumzia habari kuhusu fidia ao zabihu ya ukombozi. Pia, musome sehemu ya Biblia iliyopendekezwa kwa ajili ya Ukumbusho kila siku mkiwa familia. Kila mutu kipekee afikiri sana jinsi zabihu ya ukombozi ilimletea faida na jinsi ilimsaidia kuwa na maoni mazuri juu ya Yehova, yeye mwenyewe, wengine, na juu ya wakati ujao. Pia, mtaona kuwa jambo lenye faida kuanza kufanya mazoezi ya kuimba nyimbo mbili zitakazotumiwa wakati wa Ukumbusho, ikiwa kitabu kipya cha nyimbo kimepatikana.—Zab. 77:12.
3. Namna gani tunaweza kuonyesha shukrani yetu?
3 Jinsi ya Kuonyesha Shukrani: Kuonyesha shukrani kwa ajili ya zabihu ya ukombozi kutatuchochea tuwafundishe wengine kuhusu Yehova na upendo mkubwa alioonyesha kwa kumtuma Mwana wake. (Zab. 145:2-7) Katika mwezi wa tatu, wa ine, na wa tano, familia nyingi zinaonyesha shukrani yao kwa kufanya mipango ili mshiriki mmoja wa familia awe painia msaidizi. Ikiwa labda hilo halitawezekana, je, mnaweza ‘kununua wakati’ ili kushiriki sana katika mahubiri? (Efe. 5:16) Pia, kuonyesha shukrani kutatuchochea kuwasaidia wengine wahuzurie Ukumbusho pamoja nasi. (Ufu. 22:17) Anza kuandika majina ya wale utakaoalika kwenye Ukumbusho, yaani, watu wanaopendezwa uliozungumza nao, wanafunzi wa Biblia, washiriki wa familia, wafanyakazi wenzako, majirani, na ushiriki sana katika kampanye ya kuwagawia watu mwaliko kwenye Ukumbusho.
4. Namna gani tunaweza kutumia kwa hekima kipindi cha Ukumbusho?
4 Kipindi cha Ukumbusho kinatutolea nafasi nyingine za kuonyesha Yehova kwamba tunapendezwa sana na zawadi aliyotolea wanadamu. Acheni basi tutumie kipindi cha Ukumbusho ili kuongeza na kuonyesha shukrani yetu kwa ajili ya zabihu ya ukombozi na ‘utajiri wote usiopimika wa Kristo.’—Efe. 3:8.