Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 7/11 uku. 1
  • Muwe ‘Wenye Huruma’

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Muwe ‘Wenye Huruma’
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Iga Huruma ya Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
  • Kazi Yetu ya Kuhubiri Ni Kazi Inayoonyesha Sifa ya Huruma
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Onyesha Huruma “Watu wa Namna Zote”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
  • Uko Tayari Kwa Ajili ya Taabu Kubwa?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2011
km 7/11 uku. 1

Muwe ‘Wenye Huruma’

1. Ni jambo gani ambalo watu wanahitaji sana leo?

1 Leo, kupita wakati mwingine wowote katika historia ya wanadamu, watu wengi kabisa wanahitaji sana msaada wenye huruma. Katika ulimwengu hali zimeharibika sana na hilo linafanya watu wawe wenye kukosa furaha, wenye kushuka moyo, na kukosa tumaini. Mamilioni ya watu wanahitaji msaada, na sisi Wakristo tunaweza kuonyesha kwamba tunahangaikia kikweli majirani zetu. (Mt. 22:39; Gal. 6:10) Namna gani tunaweza kuonyesha kwamba tunawahangaikia?

2. Ni njia gani nzuri zaidi tunayoweza kutumia ili kuonyesha huruma?

2 Kazi Inayoonyesha Huruma: Mungu ndiye chanzo cha faraja ya kweli na ya milele. (2 Kor. 1:3, 4) Yehova anatusihi tumuige kwa kuwa wenye ‘huruma,’ na ametutolea kazi ya kupelekea majirani zetu habari njema ya Ufalme. (1 Pet. 3:8) Kwa kuwa Ufalme wa Mungu ndilo tumaini la pekee kwa wanadamu, kufanya yote tuwezayo ili kuwajulisha wengine jambo hilo, ndiyo njia nzuri zaidi ya kuwafariji wale “waliovunjika moyo.” (Isa. 61:1) Kwa sababu Yehova anaonea watu wake huruma, hivi karibuni ataondoa uovu na kuleta ulimwengu mpya wenye haki.—2 Pet. 3:13.

3. Namna gani tunaweza kuwaona watu jinsi Yesu alivyowaona?

3 Tuwaone Watu Jinsi Yesu Alivyowaona: Hata wakati alipokuwa akihubiria mkutano mkubwa, Yesu alikuwa akifikiria kila mutu kipekee. Aliwafundisha akifikiria mahitaji ya kiroho ya kila mmoja wao. Walikuwa kama kondoo bila mchungaji wa kuwaongoza. Moyo wa Yesu uliguswa na mambo aliyoona, na hilo lilimchochea kuwafundisha kwa uvumilivu. (Marko 6:34) Kuwaona watu jinsi Yesu alivyowaona kutatuchochea kuonyesha huruma ya kweli kwa mutu mmoja mmoja. Hilo litaonekana katika namna yetu ya kusema na pia ishara za uso wetu. Tutaweka kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza, na tutachagua maneno yetu ili kuzungumza na kila mutu tukifikiria mahitaji ao mahangaiko yake.—1 Kor. 9:19-23.

4. Kwa nini tunapaswa kujivika huruma?

4 Watu wengi kutoka mataifa yote wanakubali ujumbe wa Ufalme na wanapendezwa kuona jinsi tunavyowahangaikia. Kwa kuendelea kujivika huruma, tutamfurahisha Yehova, Mungu wetu mwenye huruma, na kumletea heshima.—Kol. 3:12.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine