Muwe ‘Wenye Huruma’
1. Ni jambo gani ambalo watu wanahitaji sana leo?
1 Leo, kupita wakati mwingine wowote katika historia ya wanadamu, watu wengi kabisa wanahitaji sana msaada wenye huruma. Katika ulimwengu hali zimeharibika sana na hilo linafanya watu wawe wenye kukosa furaha, wenye kushuka moyo, na kukosa tumaini. Mamilioni ya watu wanahitaji msaada, na sisi Wakristo tunaweza kuonyesha kwamba tunahangaikia kikweli majirani zetu. (Mt. 22:39; Gal. 6:10) Namna gani tunaweza kuonyesha kwamba tunawahangaikia?
2. Ni njia gani nzuri zaidi tunayoweza kutumia ili kuonyesha huruma?
2 Kazi Inayoonyesha Huruma: Mungu ndiye chanzo cha faraja ya kweli na ya milele. (2 Kor. 1:3, 4) Yehova anatusihi tumuige kwa kuwa wenye ‘huruma,’ na ametutolea kazi ya kupelekea majirani zetu habari njema ya Ufalme. (1 Pet. 3:8) Kwa kuwa Ufalme wa Mungu ndilo tumaini la pekee kwa wanadamu, kufanya yote tuwezayo ili kuwajulisha wengine jambo hilo, ndiyo njia nzuri zaidi ya kuwafariji wale “waliovunjika moyo.” (Isa. 61:1) Kwa sababu Yehova anaonea watu wake huruma, hivi karibuni ataondoa uovu na kuleta ulimwengu mpya wenye haki.—2 Pet. 3:13.
3. Namna gani tunaweza kuwaona watu jinsi Yesu alivyowaona?
3 Tuwaone Watu Jinsi Yesu Alivyowaona: Hata wakati alipokuwa akihubiria mkutano mkubwa, Yesu alikuwa akifikiria kila mutu kipekee. Aliwafundisha akifikiria mahitaji ya kiroho ya kila mmoja wao. Walikuwa kama kondoo bila mchungaji wa kuwaongoza. Moyo wa Yesu uliguswa na mambo aliyoona, na hilo lilimchochea kuwafundisha kwa uvumilivu. (Marko 6:34) Kuwaona watu jinsi Yesu alivyowaona kutatuchochea kuonyesha huruma ya kweli kwa mutu mmoja mmoja. Hilo litaonekana katika namna yetu ya kusema na pia ishara za uso wetu. Tutaweka kazi ya kuhubiri pa nafasi ya kwanza, na tutachagua maneno yetu ili kuzungumza na kila mutu tukifikiria mahitaji ao mahangaiko yake.—1 Kor. 9:19-23.
4. Kwa nini tunapaswa kujivika huruma?
4 Watu wengi kutoka mataifa yote wanakubali ujumbe wa Ufalme na wanapendezwa kuona jinsi tunavyowahangaikia. Kwa kuendelea kujivika huruma, tutamfurahisha Yehova, Mungu wetu mwenye huruma, na kumletea heshima.—Kol. 3:12.