Je, Unaweza ‘Kuvuka Uingie Makedonia’?
1. Ni jambo gani lililowachochea Paulo na wenzake kwenda Makedonia?
1 Karibu na mwaka wa 49 W.K., mtume Paulo aliondoka Siria ya Antiokia na kuanza safari yake ya pili ya umisionari. Alipenda kwenda kuhubiri Efeso na miji mingine katika Azia Ndogo. Lakini, roho ya Mungu ilimwomba ‘avuke kuingia Makedonia’ kuliko kwenda katika miji aliyokusudia kuhubiria. Yeye na wenzake walikubali kwa furaha, na kwa hiyo walikuwa na pendeleo la kuanzisha kutaniko la kwanza katika eneo hilo. (Mdo. 16:9, 10; 17:1, 2, 4) Leo, katika maeneo mengi ulimwenguni kuna lazima kabisa ya wavunaji wengi. (Mt. 9:37, 38) Je, unaweza kwenda huko ili kusaidia?a
2. Kwa nini watu fulani hawafikirie kwa uzito kuhamia katika inchi ya kigeni?
2 Labda unapenda kuwa misionari kama Paulo lakini haujafikiria kwa uzito kuhamia katika inchi ya kigeni. Labda, hauna uwezo wa kwenda kwenye masomo ya Gileadi kwa sababu ya miaka yako ao kwa kuwa wewe ni dada asiyeolewa ao una watoto ambao awajakomaa. Labda unafikiri kwamba hauwezi kuhamia katika inchi ya kigeni kwa sababu itakuomba ujifunze luga nyingine. Ao labda uko mgeni katika inchi unamopatikana kwa sababu za kifeza na kwa hiyo unasita kuhama. Hata hivyo, kisha kufikiria jambo hilo katika sala, huenda ukaona kwamba sababu hizo haziwezi kukuzuia kuhamia katika inchi ya kigeni mahali palipo na lazima ya wahubiri.
3. Kwa nini mazoezi ya umisionari si jambo linalotakiwa kwanza ili mutu aweze kupata matokeo mazuri kwa kuhubiri katika inchi ya kigeni?
3 Je, Ni Lazima Mutu Apate Kwanza Mazoezi ya Umisionari? Ni nini iliyosaidia mtume Paulo na wenzake kupata matokeo mazuri? Walimtegemea Yehova na roho takatifu yake. (2 Kor. 3:1-5) Kwa hiyo, hata ikiwa hali zako hazikuruhusu kupata mazoezi ya umisionari, unaweza kupata matokeo mazuri kwa kuhubiri katika inchi ya kigeni. Kumbuka pia kwamba tayari unaendelea kupata mazoezi kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na Mkutano wa Utumishi. Na ikiwa una mradi wa kwenda kwenye masomo ya Gileadi ao masomo mengine yanayotoa mazoezi kama masomo ya Gileadi, kuhamia kwako katika inchi nyingine ili kuonja utumishi wa misionari, kutakusaidia katika mambo mengi mazuri ambayo unaweza kutumia baadaye ikiwa unakubaliwa kwenda kwenye Gileadi ao kwenye masomo mengine kama Gileadi.
4. Kwa nini ndugu wenye kuzeeka hawapaswi kufikiri kwamba hawawezi kuhamia katika inchi nyingine ili kuhubiri?
4 Ndugu Wenye Kuzeeka: Ndugu wenye kuzeeka wanaokomaa kiroho na walio na afya nzuri kwa kiasi fulani wanaweza pia kuwa msaada mkubwa katika inchi zilizo na uhitaji. Je, umekwisha kuacha kazi yako ya kimwili kwa sababu umezeeka? Wengine ambao wanalipwa feza za pansio wanaweza kuwa na uwezo wa kuishi katika inchi tajiri ambako garama zao, kutia ndani garama za matunzo ya kiganga, ni chini zaidi kuliko jinsi ilivyo katika inchi yao.
5. Eleza jambo ambalo ndugu aliyeacha kazi kwa sababu ya uzee aliyehamia katika inchi ya kigeni alijionea.
5 Ndugu mmoja aliyeacha kazi kwa sababu ya uzee katika inchi moja ya Kingereza, ambaye ni mzee wa kutaniko na painia, alihamia katika eneo fulani ambako waturiste wanapenda sana katika sehemu ya Mashariki ya Azia ili kusaidia kikundi kimoja cha wahubiri 9 wanaosema Kingereza. Kikundi hicho kilihubiria wageni 30,000 wanaoishi katika eneo hilo. Katika miaka miwili watu 50 walikuwa wakihuzuria mikutano. Ndugu aliandika: “Kuhamia hapa kumeniletea baraka nyingi ambazo nilikuwa sijapata hata kidogo. Wakati hauniruhusu nieleze baraka zote ambazo nimepata!”
6. Eleza mambo ambayo dada mmoja asiyeolewa aliyehamia katika inchi iliyokuwa na uhitaji mkubwa alijionea.
6 Dada Wasioolewa: Yehova ametumia dada kwa namna ya ajabu ili kueneza habari njema katika inchi zilizo na uhitaji mkubwa. (Zab. 68:11) Dada mmoja kijana alikuwa na mradi wa kuhubiri katika inchi ya kigeni, lakini wazazi wake walikuwa wanamwogopea sana. Kwa hiyo akachagua inchi iliyokuwa na usalama katika hali ya siasa na ya feza, akaandikia biro ya tawi ya inchi hiyo, biro hiyo ikamutolea habari alizohitaji. Aliishi miaka sita katika inchi hiyo na alipata baraka nyingi. Aliandika hivi: “Katika inchi yangu singepata mafunzo mengi ya Biblia kama hapa. Lakini, kutumikia mahali ambapo kuna uhitaji mkubwa kulinisaidia niwe na mafunzo mengi ya Biblia na kuongeza uwezo wangu wa kufundisha.”
7. Eleza mambo ambayo familia moja iliyohamia katika inchi ya kigeni ilijionea.
7 Familia: Ikiwa muna watoto, je, hilo linawazuia kabisa kuhamia katika inchi ya kigeni ili kuhubiri zaidi? Familia moja yenye watoto wawili, mmoja alikuwa na miaka 8 na mwengine miaka 10, iliamua kuhama. Mama aliandika hivi: “Sisi ni wenye shukrani kwa kuwa watoto wetu wanakomalia hapa, wanashirikiana na mapainia wa pekee na misionari. Tumebarikiwa sana kwa kumutumikia Yehova mahali ambapo kuna uhitaji mkubwa.”
8. Je, inawezekana kutumikia katika inchi ya kigeni bila kujifunza luga nyingine? Eleza.
8 Wasiwasi Kuhusu Luga: Je, wazo la kwamba utajifunza luga ya kigeni linakuzuia usihamie katika inchi ya kigeni? Huenda luga yako inazungumuzwa katika inchi nyingine zilizo na uhitaji mkubwa wa wahubiri wa Ufalme. Mume mmoja na muke wake wanaosema Kingereza walihamia katika inchi fulani inayozungumza luga ya Kiespanyole ambako kuna wageni wengi wanaosema Kingereza. Kisha kupokea habari kutoka biro ya tawi kuhusu makutaniko fulani ya Kingereza yaliyo na uhitaji, walichagua kutaniko moja na kulitembelea mara mbili. Waliporudi nyumbani, walipunguza garama zao za mwezi, na kuchunga feza za kutumia kwa mwaka mmoja. Walipokuwa tayari kuhama, ndugu katika eneo hilo waliwasaidia kupata nyumba ya bei chini.
9, 10. Wale waliotoka katika inchi yao na kuhamia katika inchi nyingine wanapaswa kufikiria nini, na kwa nini?
9 Wale Waliotoka Katika Inchi Yao: Je, ulihamia katika inchi fulani, labda mbele ujifunze kweli? Labda kuna uhitaji mkubwa wa wavunaji katika inchi ulikozaliwa. Je, unaweza kufikiria kurudi ili kusaidia? Itakuwa rahisi kwako kupata kazi na makao kuliko mutu wa inchi nyingine. Labda unazungumza tayari luga inayozungumuzwa katika inchi yako. Zaidi ya hilo, labda watu watapenda kukusikiliza unapotoa ujumbe wa Ufalme kuliko mgeni.
10 Mwanaume mmoja alitoka Albania na kwenda Italia kama mkimbizi, akapata kazi nzuri, na akaanza kutumia familia yake feza huko Albania. Kisha kujifunza kweli, alianza kufundisha Kialbania kikundi fulani cha mapainia wa pekee wa Italia waliopewa mgawo wa kwenda Albania ili kusaidia mahali ambapo kulikuwa uhitaji mkubwa. Ndugu huyo aliandika hivi: “Walikuwa wakienda katika eneo nilikotoka. Hawajue luga inayosemwa huko lakini walifurahia sana kwenda huko. Nilizaliwa na kukomalia Albania na ninasema Kialbania. Ninafanya nini hapa Italia?” Ndugu huyo aliamua kurudi Albania ili kusaidia kueneza habari njema. Anasema: “Je, ninahuzunika kuacha kazi na feza katika Italia? Sihuzunike hata kidogo! Nilipata kazi inayostahili kabisa katika Albania. Kwa maoni yangu, kazi ya maana sana na inayoleta furaha yenye kudumu ni kumtumikia Yehova kwa moyo wote!”
11, 12. Wale wanaofikiria kuhamia katika inchi ya kigeni wanapaswa kufanya nini?
11 Utafanya Nini Ikiwa Una Mradi Huo? Mbele ya kwenda Makedonia, Paulo na wenzake walikusudia kusafiri upande wa kusini, lakini “walikatazwa na roho takatifu,” kwa hiyo wakarudi upande wa kaskazini. (Mdo. 16:6) Walipokaribia Bithinia, Yesu aliwazuia. (Mdo. 16:7) Yehova, kupitia Yesu, anaendelea kuongoza kazi ya kuhubiri. (Mt. 28:20) Kwa hiyo, ikiwa unafikiria kuhamia katika inchi ya kigeni, omba Yehova katika sala ili akuongoze.—Luka 14:28-30; Yak. 1:5; ona kisanduku “Namna Gani Unaweza Kujua Ikiwa Inchi Unayofikiria Ina Uhitaji.”
12 Omba wazee na Wakristo wengine wenye kukomaa wakutolee maelezo kuhusu mahali unapoweza kutumikia vizuri. (Met. 11:14; 15:22) Soma habari ambazo tumechapisha kuhusu kutumikia katika inchi ya kigeni na pia tafuta kujua mengi kuhusu inchi yoyote unayofikiria. Je, unaweza kusafiri katika inchi hiyo inayokufurahisha na kufanya siku fulani huko? Ikiwa unapenda kabisa kuhamia katika inchi nyingine, unaweza kuandikia biro ya tawi ya inchi hiyo ili kupata habari zaidi, ukitumia adresi iliyo katika Kitabu cha Mwaka cha sasa. Lakini, kuliko kutuma barua yako mara moja kwenye biro ya tawi, uitolee kwanza wazee wa kutaniko lenu, ambao wataongeza maelezo fulani mbele ya kuituma.—Ona Kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova, ukurasa wa 111-112.
13. Biro ya tawi itakusaidia namna gani, lakini daraka lako ni nini?
13 Biro ya tawi itakutolea habari zinazofaa kuhusu inchi hiyo ili kukusaidia uamue, lakini Biro haitakutolea feza, nyumba, viza, ao makaratasi mengine ya kisheria ili kukutegemeza. Hayo ni mambo ambayo unapaswa kufikiria sana mbele ya kuhama. Zaidi ya hilo, ni wewe utakayezungumza na ma ambassade ili kupata habari kuhusu viza na makaratasi ya kukuruhusu utumike katika inchi hiyo. Wale wanaohama wanapaswa kuwa na uwezo wa kujigaramia na kutimiza mambo ambayo leta inaomba.—Gal. 6:5.
14. Unapaswa kuwa mwangalifu kuhusiana na jambo gani unapotembelea ao kuhamia katika inchi ambako kazi yetu inakatazwa?
14 Inchi Ambako Kazi Yetu Inakatazwa: Katika inchi fulani ndugu na dada wa huko wanafanya mambo yote kwa siri. (Mt. 10:16) Wahubiri wanaotembelea katika inchi kama hizo ao wanaohamia huko wanaweza, bila kujua, kuhubiri waziwazi na hivyo kutia kazi yetu na usalama wa ndugu katika hatari. Ikiwa una mradi wa kuhamia katika inchi kama hiyo, unaweza kuandikia biro ya tawi ya inchi yenu kupitia baraza la wazee mbele ya kuchukua mipango ya kuhamia huko.
15. Namna gani wale ambao hawana uwezekano wa kuhama wanaweza kupanua utumishi wao mahali walipo?
15 Ikiwa Hauwezi Kuhama: Ikiwa hauwezi kuhamia katika inchi nyingine, usivunjike moyo. Labda ‘mlango mkubwa mwengine unaoongoza kwenye utendaji’ ni wenye kufunguliwa mbele yako. (1 Kor. 16:8, 9) Huenda Mwangalizi wa mzunguko wenu anaweza kujua sehemu fulani isiyo mbali sana na makao yenu iliyo na uhitaji. Labda unaweza kusaidia katika kikundi fulani cha karibu kinachotumia luga ya kigeni. Ao unaweza kupanua kazi yako ya kuhubiri katika kutaniko unamopatikana sasa. Hata iwe hali zako ziko namna gani, jambo la maana ni kuabudu kwa nafsi yote.—Kol. 3:23.
16. Tutatenda namna gani kuelekea wale wanaotaka kuhamia katika inchi ya kigeni?
16 Je, unajua Mkristo mwenye kukomaa kiroho aliye na mradi wa kutumikia katika inchi ya kigeni? Basi umutegemeze na kumutia moyo! Siria ya Antiokia, ilikuwa muji wa tatu kwa ukubwa katika Roma (kisha Roma na Aleksandria), hata hivyo mtume Paulo aliondoka na kuacha muji huo. Kwa kuwa eneo lao lilikuwa kubwa, inaelekea kwamba kutaniko la Antiokia, lilihitaji msaada wa Paulo na walihuzunika sana wakati alipoondoka. Hata hivyo, Biblia haisemi kwamba ndugu wa huko walimvunja moyo Paulo ili asiwaache. Inaelekea kwamba kuliko kujifikiria tu, walikumbuka kwamba “shamba ni ulimwengu.”—Mt. 13:38.
17. Tuna sababu gani za kufikiria ‘kuvuka kuingia Makedonia’?
17 Paulo na wenzake, walibarikiwa sana kwa kukubali mwaliko wa kuvuka kuingia Makedonia. Walipokuwa huko Filipi, muji wa Makedonia, walimpata Lidia, na “Yehova akafungua wazi moyo wake asikilize kwa makini mambo yaliyokuwa yakisemwa na Paulo.” (Mdo. 16:14) Wazia jinsi Paulo na misionari wenzake walivyofurahi wakati Lidia na watu wote wa nyumba yake walipobatizwa! Katika inchi nyingi, kuna watu wenye mioyo inayofaa kama moyo wa Lidia ambao hawajapata ujumbe wa Ufalme. Ikiwa ‘unavuka kuingia Makedonia’ utafurahi kuwapata na kuwasaidia watu hao.
[Maelezo ya chini]
a Maagizo na vitia-moyo vilivyo katika habari hii, vinaweza kusaidia ndugu wenye kukomaa kiroho katika inchi yetu ya Congo wanaofikiria kuhamia katika maeneo ya mbali ao majimbo mengine walikozaliwa. Katika inchi hii ya Congo kuna uhitaji mkubwa wa wafanyakazi katika sehemu nyingi. Wahubiri fulani wanaopatikana katika majimbo mengine, wanaweza kufikiria kurudia katika majimbo walikozaliwa ili kusaidia. Labda wengine wanasema luga inayozungumuzwa mahali ambako kuna uhitaji mkubwa wa ndugu wenye kukomaa kiroho, wanaweza pia kuhamia huko ili kusaidia. Hata ikiwa mutu harudi katika jimbo lake la kuzaliwa, katika jimbo anamopatikana kunaweza kuwa uhitaji katika mzunguko jirani.
[Sanduku katika ukurasa wa 5]
Namna Gani Unaweza Kujua Ikiwa Inchi Unayofikiria Ina Uhitaji
• Chunguza Kitabu cha Mwaka cha sasa. Tafuta kujua kila mhubiri katika inchi hiyo anapaswa kuhubiria watu wangapi.
• Tumia Index ili kutafuta habari na mambo yaliyoonwa kutoka inchi hiyo.
• Zungumza na wahubiri ambao wamekwisha kutembelea ao kuishi katika inchi hiyo.
• Ikiwa unafikiria inchi fulani ambako unaweza kuhubiri katika luga yako ya kuzaliwa, tafuta habari za inchi hiyo huku na huku, kama vile kwenye Internet, ili kuona hesabu ya watu katika inchi hiyo wanaozungumza luga yako.